< 1 Солуњанима 3 >

1 Зато не могући више трпети наумисмо сами остати у Атини,
Mwishowe hatukuweza kuvumilia zaidi. Basi, tuliamua kubaki kule Athene peke yetu,
2 И посласмо Тимотија, брата свог и слугу Божијег, и помагача свог у јеванђељу Христовом, да вас утврди и утеши у вери вашој;
na kumtuma kwenu ndugu yetu Timotheo, ambaye ni mfanyakazi mwenzetu kwa ajili ya Mungu katika kuhubiri Habari Njema ya Kristo. Tulimtuma ili awaimarisheni na kuwafarijini,
3 Да се нико не смете у овим невољама; јер сами знате да смо на то одређени.
kusudi imani ya mtu yeyote miongoni mwenu isije ikafifia kwa sababu ya taabu hizo. Ninyi mnajua kwamba tunapaswa kupata mateso.
4 Јер кад бејасмо код вас казасмо вам напред да ћемо падати у невоље, које и би, и знате.
Maana, tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwaambieni kwamba tutateswa; na kama mjuavyo ndivyo ilivyotukia.
5 Тога ради и ја не могући више трпети послах да познам веру вашу, да вас како не искуша кушач, и да узалуд не буде труд наш.
Ndio maana nilimtuma Timotheo kwenu. Sikuweza kungoja zaidi, na hivyo nilimtuma nipate habari za imani yenu. Isije ikawa labda Mshawishi aliwajaribuni na kazi yote tuliyofanya miongoni mwenu imepotea bure!
6 А сад кад дође Тимотије к нама од вас и јави нам вашу веру и љубав, и да имате добар спомен о нама свагда, желећи нас видети, као и ми вас,
Sasa Timotheo amekwisha rudi, naye ametupa habari za kufurahisha kuhusu imani na upendo wenu. Ametuarifu kwamba mnatukumbuka daima, na kwamba mna hamu ya kutuona sisi kama nasi tulivyo na hamu ya kuwaoneni.
7 Зато се утешисмо, браћо, вама у свакој жалости и невољи својој вашом вером;
Basi, habari za imani yenu zimetutia moyo katika taabu na mateso yetu yote,
8 Јер смо ми сад живи кад ви стојите у Господу.
kwani sasa tunaishi kweli ikiwa ninyi mnasimama imara katika kuungana na Bwana.
9 Јер какву хвалу можемо дати Богу за вас, за сваку радост којом се радујемо вас ради пред Богом својим?
Sasa twaweza kumshukuru Mungu wetu kwa ajili yenu. Tunamshukuru kwa furaha tuliyo nayo mbele yake kwa sababu yenu.
10 Дан и ноћ молимо се Богу преизобилно да видимо лице ваше, и да испунимо недостатак вере ваше.
Tunazidi kumwomba Mungu usiku na mchana kwa moyo wetu wote ili atupatie fursa ya kuwaoneni uso kwa uso ili tuweze kurekebisha chochote kilichopungua katika imani yenu.
11 А сам Бог и Отац наш и Господ наш Исус Христос да управи пут наш к вама.
Tunamwomba Mungu, Baba yetu mwenyewe, na Bwana wetu Yesu atutayarishie njia ya kuja kwenu.
12 А вас Господ да умножи, и да имате изобилну љубав један к другом и к свима, као и ми к вама.
Bwana awawezeshe ninyi kupendana na kuwapenda watu wote zaidi na zaidi, kama vile sisi tunavyowapenda ninyi.
13 Да би се утврдила срца ваша без кривице у светињи пред Богом и Оцем нашим, за долазак Господа нашег Исуса Христа са свима светима Његовим. Амин.
Hivyo ataiimarisha mioyo yenu, nanyi mtakuwa wakamilifu na watakatifu mbele ya Mungu na Baba yetu wakati Bwana wetu Yesu atakapokuja pamoja na wote walio wake.

< 1 Солуњанима 3 >