< 1 Солуњанима 3 >

1 Зато не могући више трпети наумисмо сами остати у Атини,
Kwa hivyo tulipokuwa hatuwezi kuvumilia zaidi, tuliamua tubaki Athene peke yetu.
2 И посласмо Тимотија, брата свог и слугу Божијег, и помагача свог у јеванђељу Христовом, да вас утврди и утеши у вери вашој;
Tukamtuma Timotheo ambaye ni ndugu yetu na mtumishi mwenzetu wa Mungu katika kuieneza Injili ya Kristo, aje kuwaimarisha na kuwatia moyo katika imani yenu,
3 Да се нико не смете у овим невољама; јер сами знате да смо на то одређени.
ili mtu yeyote asifadhaishwe na mateso haya. Mnajua vyema kwamba tumewekewa hayo mateso.
4 Јер кад бејасмо код вас казасмо вам напред да ћемо падати у невоље, које и би, и знате.
Kwa kweli, tulipokuwa pamoja nanyi tuliwaambia mara kwa mara kwamba tutateswa na imekuwa hivyo kama mjuavyo.
5 Тога ради и ја не могући више трпети послах да познам веру вашу, да вас како не искуша кушач, и да узалуд не буде труд наш.
Kwa sababu hii nilipokuwa siwezi kuvumilia zaidi, nilimtuma mtu ili nipate habari za imani yenu. Niliogopa kwamba kwa njia fulani yule mjaribu asiwe amewajaribu, nasi tukawa tumejitaabisha bure.
6 А сад кад дође Тимотије к нама од вас и јави нам вашу веру и љубав, и да имате добар спомен о нама свагда, желећи нас видети, као и ми вас,
Lakini sasa Timotheo ndiyo tu amerejea kwetu kutoka kwenu na ameleta habari njema kuhusu imani yenu na upendo wenu. Ametuambia kwamba siku zote mnatukumbuka kwa wema na kwamba mna shauku ya kutuona kama vile sisi tulivyo na shauku ya kuwaona ninyi.
7 Зато се утешисмо, браћо, вама у свакој жалости и невољи својој вашом вером;
Kwa hiyo, ndugu zetu, katika dhiki na mateso yetu yote tumefarijika kwa sababu ya imani yenu.
8 Јер смо ми сад живи кад ви стојите у Господу.
Sasa kwa kuwa hakika tunaishi, kwa kuwa ninyi mmesimama imara katika Bwana.
9 Јер какву хвалу можемо дати Богу за вас, за сваку радост којом се радујемо вас ради пред Богом својим?
Je, tutawezaje kumshukuru Mungu kiasi cha kutosha kwa ajili yenu, kutokana na furaha tuliyo nayo mbele za Mungu wetu kwa sababu yenu?
10 Дан и ноћ молимо се Богу преизобилно да видимо лице ваше, и да испунимо недостатак вере ваше.
Usiku na mchana tunaomba kwa bidii ili tupate kuwaona tena na kujaza kile kilichopungua katika imani yenu.
11 А сам Бог и Отац наш и Господ наш Исус Христос да управи пут наш к вама.
Basi Mungu wetu na Baba yetu mwenyewe na Bwana wetu Yesu atengeneze njia ya sisi kuja kwenu.
12 А вас Господ да умножи, и да имате изобилну љубав један к другом и к свима, као и ми к вама.
Bwana na auongeze upendo wenu na kuuzidisha kati yenu na kwa wengine wote, kama vile tulivyo na upendo mwingi kwenu.
13 Да би се утврдила срца ваша без кривице у светињи пред Богом и Оцем нашим, за долазак Господа нашег Исуса Христа са свима светима Његовим. Амин.
Tunamwomba Mungu aimarishe mioyo yenu ili msiwe na lawama katika utakatifu mbele za Mungu wetu aliye Baba yetu wakati wa kuja kwake Bwana Yesu pamoja na watakatifu wote.

< 1 Солуњанима 3 >