< Ponovljeni Zakon 25 >

1 Kad je raspra meðu ljudima, pa doðu na sud da im sude, tada pravoga neka opravdaju a krivoga neka osude.
Iwapo kutakuwa na malumbano kati ya wanaume na wakaenda mahakamani, na waamuzi wakawahukumu, basi watamwachilia mtakatifu na kumhukumu muovu.
2 I ako krivi zaslužuje boj, tada sudija neka zapovjedi da ga povale i biju pred njim, na broj prema krivici njegovoj.
Iwapo mwanamume mwenye hatia anastahili kupigwa, basi muamuzi atamfanya alale chini na kupigwa mbele zake kwa idadi iliyoamriwa kulingana na kosa lake.
3 Do èetrdeset udaraca neka zapovjedi da mu udare, ne više, da se ne bi poništio brat tvoj u tvojim oèima, kad bi mu se udarilo više udaraca.
Muamuzi anaweza kumpatia mapigo arobaini, lakini hapaswi kuvuka idadi hiyo; kwa maana akivuka idadi hiyo na kumpiga kwa mapigo mengi zaidi, basi Muisraeli mwenzako atakuwa kaaibishwa mbele ya macho yenu.
4 Nemoj zavezati usta volu kad vrše.
Haupaswi kumfunga punda wako pua na mdomo anapokuwa akilima shamba lako.
5 Kad braæa žive zajedno pa umre jedan od njih bez djece, onda žena umrloga da se ne uda iz kuæe za drugoga; brat njegov neka otide k njoj i uzme je za ženu i uèini joj dužnost djeversku.
Iwapo kaka wanaishi pamoja na mmoja wao akafariki bila kuwa na mwana, basi mke wa marehemu hatakiwi kuolewa na mtu nje ya familia. Badala yake, kaka yake mumewe anapaswa kulala naye na kumchukua kuwa mke wake na kutekeleza wajibu wa kaka wa mume kwake.
6 I prvi sin kojega ona rodi neka se nazove imenom brata njegova umrloga, da ne pogine ime njegovo u Izrailju.
Hii ni kwamba mtoto wa kwanza atakayezaliwa arithi chini ya jina la kaka yake mwanamume aliyefariki, ili jina lake lisiangamie ndani ya Israeli.
7 Ako li onaj èovjek ne bi htio uzeti snahe svoje, onda snaha njegova neka doðe na vrata pred starješine, i reèe: neæe djever moj da podigne bratu svojemu sjemena u Izrailju, neæe da mi uèini dužnosti djeverske.
Lakini kama mwanamume hataki kumchukua mke wa kaka yake awe wake, basi mke wa kaka yake anapaswa kwenda malangoni mpaka kwa wazee na kusema, “Kaka wa mume wangu amekataa kuwajibika kwa niaba ya jina la kaka yake humu Israeli; hataki kufanya wajibu wa kaka wa mume kwangu”.
8 Tada neka ga dozovu starješine mjesta onoga i razgovore se s njim; pa ako se on upre i reèe: neæu da je uzmem;
Kisha wazee wa mji wake wanapaswa kumuita na kuzungumza naye. Lakini tuseme atasisitiza na kusema, “Sitaki kumchukua”.
9 Onda neka pristupi k njemu snaha njegova pred starješinama, i neka mu izuje obuæu s noge njegove i pljune mu u lice, i progovorivši neka reèe: tako valja da bude èovjeku koji neæe da zida kuæe brata svojega.
Basi mke wa kaka yake anatakiwa kuja kwake mbele ya wazee, kumvua ndara zake miguuni mwake, na kumtemea usoni. Anapaswa kumjibu na kusema, “Hivi ndivyo kinachofanyika kwa mwanamume asiyetaka kujenga nyumba ya kaka yake”.
10 I on neka se zove u Izrailju: dom bosoga.
Jina lake Israeli litaitwa, “Nyumba ya mtu aliyevuliwa ndara zake”.
11 Ako bi se svadili ljudi, jedan s drugim, pa bi došla žena jednoga da otme muža svojega iz ruke drugoga koji ga bije, i pruživši ruku svoju uhvatila bi ga za mošnice,
Iwapo wanamume wamepigana wao kwa wao, na mke wa mmoja wao kaja kumkomboa mumewe dhidi ya yule aliyempiga, naye akanyosha mkono wake na kumshika sehemu za siri,
12 Otsijeci joj ruku; neka ne žali oko tvoje.
basi unapaswa kuukata mkono yake; jicho lako halipaswi kuwa na huruma.
13 Nemoj imati u torbi svojoj dvojaku mjeru, veliku i malu.
Haupaswi kuwa na mizani ya uzito tofauti katika mfuko wako, mkubwa na mdogo.
14 Nemoj imati u kuæi svojoj dvojaku efu, veliku i malu.
Hautakiwi kuwa na vipimo tofauti ndani ya nyumba yako, vikubwa na vidogo.
15 Mjera potpuna i prava neka ti je; efa potpuna i prava neka ti je, da bi ti se produljili dani tvoji u zemlji koju ti daje Gospod Bog tvoj.
Unatakiwa kuwa na uzito kamili na wa haki; unatakiwa kuwa na vipimo kamili na vya haki, ili siku zako ziwe ndefu katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anakupatia.
16 Jer je gad pred Gospodom Bogom tvojim ko god èini tako, ko god èini krivo.
Kwa maana wote wanaofanya vitu hivi, wote wanaovunja haki, ni chukizo kwa Yahwe Mungu wako.
17 Opominji se šta ti je uèinio Amalik na putu kad iðaste iz Misira,
Kumbuka ni jambo gani Amaleki alichofanya kwako barabarani ulipokuwa ukitoka Misri,
18 Kako te doèeka na putu i pobi na kraju sve umorne koji iðahu za tobom, kad si bio sustao i iznemogao, i ne boja se Boga.
jinsi alivyokutana na wewe barabarani na kuwashambulia kati yenu kwa nyuma, wale waliokuwa wamelegea nyuma, mlipokuwa dhaifu na kuchoka, hakumheshimu Mungu.
19 Zato kad te Gospod Bog tvoj smiri od svijeh neprijatelja tvojih unaokolo u zemlji koju ti daje Gospod Bog tvoj da je naslijediš, tada zatri spomen Amaliku pod nebom; ne zaboravi.
Kwa hiyo, Yahwe Mungu wako atakapowapa pumziko kutoka kwa maadui zako kila sehemu, katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anawapatia kumiliki kama urithi, hautakiwi kusahau kuwa unapaswa kufuta kumbukumbu ya Waamaleki chini ya mbingu.

< Ponovljeni Zakon 25 >