< ลูก: 19 >

1 ยทา ยีศุ รฺยิรีโหปุรํ ปฺรวิศฺย ตนฺมเธฺยน คจฺฉํสฺตทา
Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
2 สกฺเกยนามา กรสญฺจายินำ ปฺรธาโน ธนวาเนโก
Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 ยีศุ: กีทฺฤคิติ ทฺรษฺฏุํ เจษฺฏิตวานฺ กินฺตุ ขรฺวฺวตฺวาโลฺลกสํฆมเธฺย ตทฺทรฺศนมปฺราปฺย
Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
4 เยน ปถา ส ยาสฺยติ ตตฺปเถ'เคฺร ธาวิตฺวา ตํ ทฺรษฺฏุมฺ อุฑุมฺพรตรุมารุโรหฯ
Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
5 ปศฺจาทฺ ยีศุสฺตตฺสฺถานมฺ อิตฺวา อูรฺทฺธฺวํ วิโลกฺย ตํ ทฺฤษฺฏฺวาวาทีตฺ, เห สกฺเกย ตฺวํ ศีฆฺรมวโรห มยาทฺย ตฺวทฺเคเห วสฺตวฺยํฯ
Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.”
6 ตต: ส ศีฆฺรมวรุหฺย สาหฺลาทํ ตํ ชคฺราหฯ
Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
7 ตทฺ ทฺฤษฺฏฺวา สรฺเวฺว วิวทมานา วกฺตุมาเรภิเร, โสติถิเตฺวน ทุษฺฏโลกคฺฤหํ คจฺฉติฯ
Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, “Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi.”
8 กินฺตุ สกฺเกโย ทณฺฑายมาโน วกฺตุมาเรเภ, เห ปฺรโภ ปศฺย มม ยา สมฺปตฺติรสฺติ ตทรฺทฺธํ ทริเทฺรโภฺย ทเท, อปรมฺ อนฺยายํ กฺฤตฺวา กสฺมาทปิ ยทิ กทาปิ กิญฺจิตฺ มยา คฺฤหีตํ ตรฺหิ ตจฺจตุรฺคุณํ ททามิฯ
Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, “Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne.”
9 ตทา ยีศุสฺตมุกฺตวานฺ อยมปิ อิพฺราหีม: สนฺตาโน'ต: การณาทฺ อทฺยาสฺย คฺฤเห ตฺราณมุปสฺถิตํฯ
Yesu akamwambia, “Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
10 ยทฺ หาริตํ ตตฺ มฺฤคยิตุํ รกฺษิตุญฺจ มนุษฺยปุตฺร อาคตวานฺฯ
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea.”
11 อถ ส ยิรูศาลม: สมีป อุปาติษฺฐทฺ อีศฺวรราชตฺวสฺยานุษฺฐานํ ตไทว ภวิษฺยตีติ โลไกรนฺวภูยต, ตสฺมาตฺ ส โศฺรตฺฤภฺย: ปุนรฺทฺฤษฺฏานฺตกถามฺ อุตฺถาปฺย กถยามาสฯ
Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
12 โกปิ มหาโลฺลโก นิชารฺถํ ราชตฺวปทํ คฺฤหีตฺวา ปุนราคนฺตุํ ทูรเทศํ ชคามฯ
Hivyo akawaambia, “Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
13 ยาตฺรากาเล นิชานฺ ทศทาสานฺ อาหูย ทศสฺวรฺณมุทฺรา ทตฺตฺวา มมาคมนปรฺยฺยนฺตํ วาณิชฺยํ กุรุเตตฺยาทิเทศฯ
Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
14 กินฺตุ ตสฺย ปฺรชาสฺตมวชฺญาย มนุษฺยเมนมฺ อสฺมากมุปริ ราชตฺวํ น การยิวฺยาม อิมำ วารฺตฺตำ ตนฺนิกเฏ เปฺรรยามาสุ: ฯ
Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
15 อถ ส ราชตฺวปทํ ปฺราปฺยาคตวานฺ เอไกโก ชโน พาณิเชฺยน กึ ลพฺธวานฺ อิติ ชฺญาตุํ เยษุ ทาเสษุ มุทฺรา อรฺปยตฺ ตานฺ อาหูยาเนตุมฺ อาทิเทศฯ
“Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
16 ตทา ปฺรถม อาคตฺย กถิตวานฺ, เห ปฺรโภ ตว ตไยกยา มุทฺรยา ทศมุทฺรา ลพฺธา: ฯ
Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
17 ตต: ส อุวาจ ตฺวมุตฺตโม ทาส: สฺวลฺเปน วิศฺวาโสฺย ชาต อิต: การณาตฺ ตฺวํ ทศนคราณามฺ อธิโป ภวฯ
Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
18 ทฺวิตีย อาคตฺย กถิตวานฺ, เห ปฺรโภ ตไวกยา มุทฺรยา ปญฺจมุทฺรา ลพฺธา: ฯ
Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
19 ตต: ส อุวาจ, ตฺวํ ปญฺจานำ นคราณามธิปติ รฺภวฯ
Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
20 ตโตนฺย อาคตฺย กถยามาส, เห ปฺรโภ ปศฺย ตว ยา มุทฺรา อหํ วสฺเตฺร พทฺธฺวาสฺถาปยํ เสยํฯ
“Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
21 ตฺวํ กฺฤปโณ ยนฺนาสฺถาปยสฺตทปิ คฺฤหฺลาสิ, ยนฺนาวปสฺตเทว จ ฉินตฺสิ ตโตหํ ตฺวตฺโต ภีต: ฯ
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
22 ตทา ส ชคาท, เร ทุษฺฏทาส ตว วาเกฺยน ตฺวำ โทษิณํ กริษฺยามิ, ยทหํ นาสฺถาปยํ ตเทว คฺฤหฺลามิ, ยทหํ นาวปญฺจ ตเทว ฉินทฺมิ, เอตาทฺฤศ: กฺฤปโณหมิติ ยทิ ตฺวํ ชานาสิ,
Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
23 ตรฺหิ มม มุทฺรา พณิชำ นิกเฏ กุโต นาสฺถาปย: ? ตยา กฺฤเต'หมฺ อาคตฺย กุสีเทน สารฺทฺธํ นิชมุทฺรา อปฺราปฺสฺยมฺฯ
Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
24 ปศฺจาตฺ ส สมีปสฺถานฺ ชนานฺ อาชฺญาปยตฺ อสฺมาตฺ มุทฺรา อานีย ยสฺย ทศมุทฺรา: สนฺติ ตไสฺม ทตฺตฯ
Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
25 เต โปฺรจุ: ปฺรโภ'สฺย ทศมุทฺรา: สนฺติฯ
Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
26 ยุษฺมานหํ วทามิ ยสฺยาศฺรเย วทฺธเต 'ธิกํ ตไสฺม ทายิษฺยเต, กินฺตุ ยสฺยาศฺรเย น วรฺทฺธเต ตสฺย ยทฺยทสฺติ ตทปิ ตสฺมานฺ นายิษฺยเตฯ
Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 กินฺตุ มมาธิปติตฺวสฺย วศเตฺว สฺถาตุมฺ อสมฺมนฺยมานา เย มม ริปวสฺตานานีย มม สมกฺษํ สํหรตฯ
Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu.”
28 อิตฺยุปเทศกถำ กถยิตฺวา โสคฺรค: สนฺ ยิรูศาลมปุรํ ยเยาฯ
Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
29 ตโต ไพตฺผคีไพถนียาคฺรามโย: สมีเป ไชตุนาเทฺรรนฺติกมฺ อิตฺวา ศิษฺยทฺวยมฺ อิตฺยุกฺตฺวา เปฺรษยามาส,
Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 ยุวามมุํ สมฺมุขสฺถคฺรามํ ปฺรวิไศฺยว ยํ โกปิ มานุษ: กทาปิ นาโรหตฺ ตํ ครฺทฺทภศาวกํ พทฺธํ ทฺรกฺษฺยถสฺตํ โมจยิตฺวานยตํฯ
akawaambia: “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
31 ตตฺร กุโต โมจยถ: ? อิติ เจตฺ โกปิ วกฺษฺยติ ตรฺหิ วกฺษฺยถ: ปฺรเภรตฺร ปฺรโยชนมฺ อาเสฺตฯ
Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye.”
32 ตทา เตา ปฺรริเตา คตฺวา ตตฺกถานุสาเรณ สรฺวฺวํ ปฺราปฺเตาฯ
Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33 ครฺทภศาวกโมจนกาเล ตตฺวามิน อูจุ: , ครฺทภศาวกํ กุโต โมจยถ: ?
Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?”
34 ตาวูจตุ: ปฺรโภรตฺร ปฺรโยชนมฺ อาเสฺตฯ
Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”
35 ปศฺจาตฺ เตา ตํ ครฺทภศาวกํ ยีโศรนฺติกมานีย ตตฺปฺฤษฺเฐ นิชวสนานิ ปาตยิตฺวา ตทุปริ ยีศุมาโรหยามาสตุ: ฯ
Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36 อถ ยาตฺรากาเล โลกา: ปถิ สฺววสฺตฺราณิ ปาตยิตุมฺ อาเรภิเรฯ
Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 อปรํ ไชตุนาเทฺรรุปตฺยกามฺ อิตฺวา ศิษฺยสํฆ: ปูรฺวฺวทฺฤษฺฏานิ มหากรฺมฺมาณิ สฺมฺฤตฺวา,
Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38 โย ราชา ปฺรโภ รฺนามฺนายาติ ส ธนฺย: สฺวรฺเค กุศลํ สรฺโวฺวจฺเจ ชยธฺวนิ รฺภวตุ, กถาเมตำ กถยิตฺวา สานนฺทมฺ อุไจรีศฺวรํ ธนฺยํ วกฺตุมาเรเภฯ
wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”
39 ตทา โลการณฺยมธฺยสฺถา: กิยนฺต: ผิรูศินสฺตตฺ ศฺรุตฺวา ยีศุํ โปฺรจุ: , เห อุปเทศก สฺวศิษฺยานฺ ตรฺชยฯ
Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”
40 ส อุวาจ, ยุษฺมานหํ วทามิ ยทฺยมี นีรวาสฺติษฺฐนฺติ ตรฺหิ ปาษาณา อุไจ: กถา: กถยิษฺยนฺติฯ
Yesu akawajibu, “Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti.”
41 ปศฺจาตฺ ตตฺปุรานฺติกเมตฺย ตทวโลกฺย สาศฺรุปาตํ ชคาท,
Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
42 หา หา เจตฺ ตฺวมเคฺร'ชฺญาสฺยถา: , ตวาสฺมินฺเนว ทิเน วา ยทิ สฺวมงฺคลมฺ อุปาลปฺสฺยถา: , ตรฺหฺยุตฺตมมฺ อภวิษฺยตฺ, กินฺตุ กฺษเณสฺมินฺ ตตฺตว ทฺฤษฺเฏรโคจรมฺ ภวติฯ
akisema: “Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 ตฺวํ สฺวตฺราณกาเล น มโน นฺยธตฺถา อิติ เหโต รฺยตฺกาเล ตว ริปวสฺตฺวำ จตุรฺทิกฺษุ ปฺราจีเรณ เวษฺฏยิตฺวา โรตฺสฺยนฺติ
Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
44 พาลไก: สารฺทฺธํ ภูมิสาตฺ กริษฺยนฺติ จ ตฺวนฺมเธฺย ปาษาไณโกปิ ปาษาโณปริ น สฺถาสฺยติ จ, กาล อีทฺฤศ อุปสฺถาสฺยติฯ
Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa.”
45 อถ มเธฺยมนฺทิรํ ปฺรวิศฺย ตตฺรตฺยานฺ กฺรยิวิกฺรยิโณ พหิษฺกุรฺวฺวนฺ
Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
46 อวทตฺ มทฺคฺฤหํ ปฺรารฺถนาคฺฤหมิติ ลิปิราเสฺต กินฺตุ ยูยํ ตเทว ไจราณำ คหฺวรํ กุรุถฯ
akisema, “Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.”
47 ปศฺจาตฺ ส ปฺรตฺยหํ มเธฺยมนฺทิรมฺ อุปทิเทศ; ตต: ปฺรธานยาชกา อธฺยาปกา: ปฺราจีนาศฺจ ตํ นาศยิตุํ จิเจษฺฏิเร;
Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
48 กินฺตุ ตทุปเทเศ สรฺเวฺว โลกา นิวิษฺฏจิตฺตา: สฺถิตาสฺตสฺมาตฺ เต ตตฺกรฺตฺตุํ นาวกาศํ ปฺราปุ: ฯ
lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.

< ลูก: 19 >