< romiNaH 9 >

1 ahaM kA nchid kalpitAM kathAM na kathayAmi, khrIShTasya sAkShAt satyameva bravImi pavitrasyAtmanaH sAkShAn madIyaM mana etat sAkShyaM dadAti|
Nasema ukweli mtupu; nimeungana na Kristo nami sisemi uongo. Dhamiri yangu ikiongozwa na Roho Mtakatifu inanithibitishia jambo hili pia.
2 mamAntaratishayaduHkhaM nirantaraM khedashcha
Nataka kusema hivi: nina huzuni kubwa na maumivu yasiyopimika moyoni mwangu
3 tasmAd ahaM svajAtIyabhrAtR^iNAM nimittAt svayaM khrIShTAchChApAkrAnto bhavitum aichCham|
kwa ajili ya watu wangu, walio damu moja nami! Kama ingekuwa kwa faida yao, ningekuwa radhi kulaaniwa na kutengwa na Kristo.
4 yatasta isrAyelasya vaMshA api cha dattakaputratvaM tejo niyamo vyavasthAdAnaM mandire bhajanaM pratij nAH pitR^ipuruShagaNashchaiteShu sarvveShu teShAm adhikAro. asti|
Hao ndio watu wa Israeli ambao Mungu aliwateua wawe watoto wake, akawashirikisha utukufu wake; aliagana nao, akawapa Sheria yake, imani ya kweli na ahadi zake.
5 tat kevalaM nahi kintu sarvvAdhyakShaH sarvvadA sachchidAnanda Ishvaro yaH khrIShTaH so. api shArIrikasambandhena teShAM vaMshasambhavaH| (aiōn g165)
Wao ni wajukuu wa mababu, naye Kristo, kadiri ya ubinadamu wake, ametoka katika ukoo wao. Mungu atawalaye juu ya yote, na atukuzwe milele! Amina. (aiōn g165)
6 Ishvarasya vAkyaM viphalaM jAtam iti nahi yatkAraNAd isrAyelo vaMshe ye jAtAste sarvve vastuta isrAyelIyA na bhavanti|
Sisemi kwamba ahadi ya Mungu imebatilika; maana si watu wote wa Israeli ni wateule wa Mungu.
7 aparam ibrAhImo vaMshe jAtA api sarvve tasyaiva santAnA na bhavanti kintu ishAko nAmnA tava vaMsho vikhyAto bhaviShyati|
Wala, si wazawa wote wa Abrahamu ni watoto wake wa kweli. Ila, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Wazao wake watatokana na Isaka.”
8 arthAt shArIrikasaMsargAt jAtAH santAnA yAvantastAvanta eveshvarasya santAnA na bhavanti kintu pratishravaNAd ye jAyante taeveshvaravaMsho gaNyate|
Nido kusema, wale waliozaliwa kimaumbile ndio watoto wa Mungu, bali wale waliozaliwa kutokana na ahadi ya Mungu ndio watakaoitwa watoto wake.
9 yatastatpratishrute rvAkyametat, etAdR^ishe samaye. ahaM punarAgamiShyAmi tatpUrvvaM sArAyAH putra eko janiShyate|
Maana ahadi yenyewe ni hii: “Nitakujia wakati maalum, naye Sara atapata mtoto.”
10 aparamapi vadAmi svamano. abhilAShata IshvareNa yannirUpitaM tat karmmato nahi kintvAhvayitu rjAtametad yathA siddhyati
Tena si hayo tu ila pia Rebeka naye alipata mapacha kwa baba mmoja, yaani Isaka, babu yetu.
11 tadarthaM ribkAnAmikayA yoShitA janaikasmAd arthAd asmAkam ishAkaH pUrvvapuruShAd garbhe dhR^ite tasyAH santAnayoH prasavAt pUrvvaM ki ncha tayoH shubhAshubhakarmmaNaH karaNAt pUrvvaM
Lakini, ili Mungu aonekane kwamba anao uhuru wa kuchagua, hata kabla wale ndugu hawajazaliwa na kabla hawajaweza kupambanua jema na baya,
12 tAM pratIdaM vAkyam uktaM, jyeShThaH kaniShThaM seviShyate,
Rebeka aliambiwa kwamba yule mtoto wa kwanza atamtumikia yule wa nyuma. Hivyo uchaguzi wa Mungu unategemea jinsi anavyoita mwenyewe, na si matendo ya binadamu.
13 yathA likhitam Aste, tathApyeShAvi na prItvA yAkUbi prItavAn ahaM|
Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Yakobo nilimpenda, lakini Esau nilimchukia.”
14 tarhi vayaM kiM brUmaH? IshvaraH kim anyAyakArI? tathA na bhavatu|
Basi, tuseme nini? Je, Mungu amekosa haki? Hata kidogo!
15 yataH sa svayaM mUsAm avadat; ahaM yasmin anugrahaM chikIrShAmi tamevAnugR^ihlAmi, ya ncha dayitum ichChAmi tameva daye|
Maana alimwambia Mose: “Nitamhurumia mtu yeyote ninayetaka kumhurumia; nitamwonea huruma mtu yeyote ninayetaka.”
16 ataevechChatA yatamAnena vA mAnavena tanna sAdhyate dayAkAriNeshvareNaiva sAdhyate|
Kwa hiyo, yote hutegemea huruma ya Mungu, na si bidii au mapenzi ya mtu.
17 phirauNi shAstre likhati, ahaM tvaddvArA matparAkramaM darshayituM sarvvapR^ithivyAM nijanAma prakAshayitu ncha tvAM sthApitavAn|
Maana Maandiko Matakatifu yasema hivi kwa Farao: “Nilikufanya mfalme ili kwa njia yako, uwezo wangu ujulikane, na jina langu litangazwe popote duniani.”
18 ataH sa yam anugrahItum ichChati tamevAnugR^ihlAti, ya ncha nigrahItum ichChati taM nigR^ihlAti|
Ni wazi, basi, kwamba Mungu humhurumia yeyote anayetaka kumhurumia, na akipenda kumfanya mtu awe mkaidi, hufanya hivyo.
19 yadi vadasi tarhi sa doShaM kuto gR^ihlAti? tadIyechChAyAH pratibandhakatvaM karttaM kasya sAmarthyaM vidyate?
Labda utaniuliza: “Ikiwa mambo yako hivyo, Mungu anawezaje kumlaumu mtu? Nani awezaye kuyapinga mapenzi yake?”
20 he Ishvarasya pratipakSha martya tvaM kaH? etAdR^ishaM mAM kutaH sR^iShTavAn? iti kathAM sR^iShTavastu sraShTre kiM kathayiShyati?
Lakini, ewe binadamu, u nani hata uthubutu kumhoji Mungu? Je, chungu chaweza kumwuliza mfinyanzi wake: “Kwa nini umenitengeneza namna hii?”
21 ekasmAn mR^itpiNDAd utkR^iShTApakR^iShTau dvividhau kalashau karttuM kiM kulAlasya sAmarthyaM nAsti?
Mfinyanzi anaweza kuutumia udongo apendavyo na kufinyanga vyungu viwili kwa udongo uleule; kimoja kwa matumizi ya heshima, na kingine kwa matumizi ya kawaida.
22 IshvaraH kopaM prakAshayituM nijashaktiM j nApayitu nchechChan yadi vinAshasya yogyAni krodhabhAjanAni prati bahukAlaM dIrghasahiShNutAm Ashrayati;
Hivyo ndivyo ilivyo kwa Mungu. Alitaka kuonyesha ghadhabu yake na kujulisha uwezo wake, Basi, alikuwa na saburi sana, akiwavumilia wale ambao walikuwa lengo la ghadhabu yake, ambao walistahili kuangamizwa.
23 apara ncha vibhavaprAptyarthaM pUrvvaM niyuktAnyanugrahapAtrANi prati nijavibhavasya bAhulyaM prakAshayituM kevalayihUdinAM nahi bhinnadeshinAmapi madhyAd
Alitaka pia kudhihirisha wingi wa utukufu wake ambao alitumiminia sisi tulio lengo la huruma yake; sisi ambao alikwisha kututayarisha kuupokea utukufu wake.
24 asmAniva tAnyAhvayati tatra tava kiM?
Maana sisi ndio hao aliowaita, si tu kutoka miongoni mwa Wayahudi bali pia kutoka kwa watu wa mataifa mengine.
25 hosheyagranthe yathA likhitam Aste, yo loko mama nAsIt taM vadiShyAmi madIyakaM| yA jAti rme. apriyA chAsIt tAM vadiShyAmyahaM priyAM|
Maana ndivyo asemavyo katika kitabu cha Hosea: “Wale waliokuwa Si watu wangu nitawaita: Watu wangu! Naye Sikupendi ataitwa: Mpenzi wangu!
26 yUyaM madIyalokA na yatreti vAkyamauchyata| amareshasya santAnA iti khyAsyanti tatra te|
Na pale walipoambiwa: Ninyi si wangu hapo wataitwa: Watoto wa Mungu hai.”
27 isrAyelIyalokeShu yishAyiyo. api vAchametAM prAchArayat, isrAyelIyavaMshAnAM yA saMkhyA sA tu nishchitaM| samudrasikatAsaMkhyAsamAnA yadi jAyate| tathApi kevalaM lokairalpaistrANaM vrajiShyate|
Naye nabii Isaya, kuhusu Israeli anapaaza sauti: “Hata kama watoto wa Israeli ni wengi kama mchanga wa pwani, ni wachache tu watakaookolewa;
28 yato nyAyena svaM karmma pareshaH sAdhayiShyati| deshe saeva saMkShepAnnijaM karmma kariShyati|
maana, Bwana ataitekeleza upesi hukumu yake kamili juu ya ulimwengu wote.”
29 yishAyiyo. aparamapi kathayAmAsa, sainyAdhyakShapareshena chet ki nchinnodashiShyata| tadA vayaM sidomevAbhaviShyAma vinishchitaM| yadvA vayam amorAyA agamiShyAma tulyatAM|
Ni kama Isaya alivyosema hapo awali: “Kama Bwana Mwenye Nguvu asingalituachia baadhi ya watoto wa Israeli, tungalikwisha kuwa kama Sodoma, tungalikwisha kuwa ma Gomora.”
30 tarhi vayaM kiM vakShyAmaH? itaradeshIyA lokA api puNyArtham ayatamAnA vishvAsena puNyam alabhanta;
Basi, tuseme nini? Ni hivi: watu wa mataifa ambao hawakutafuta kukubaliwa kuwa waadilifu, wamekubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani,
31 kintvisrAyellokA vyavasthApAlanena puNyArthaM yatamAnAstan nAlabhanta|
hali watu wa Israeli waliokuwa wakitafuta Sheria iletayo kukubaliwa kuwa waadilifu, hawakuipata.
32 tasya kiM kAraNaM? te vishvAsena nahi kintu vyavasthAyAH kriyayA cheShTitvA tasmin skhalanajanake pAShANe pAdaskhalanaM prAptAH|
Kwa nini? Kwa sababu walitegemea matendo yao badala ya kutegemea imani. Walijikwaa juu ya jiwe la kujikwaa
33 likhitaM yAdR^isham Aste, pashya pAdaskhalArthaM hi sIyoni prastarantathA| bAdhAkAra ncha pAShANaM paristhApitavAnaham| vishvasiShyati yastatra sa jano na trapiShyate|
kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: “Tazama! Naweka huko Sioni jiwe likwazalo, mwamba utakaowafanya watu waanguke. Mtu atakayemwamini yeye aliye hilo jiwe, hataaibishwa!”

< romiNaH 9 >