< lUkaH 7 >

1 tataH paraM sa lokAnAM karNagocare tAn sarvvAn upadezAn samApya yadA kapharnAhUmpuraM pravizati
Baada ya Yesu kumaliza kila kitu alichokuwa anasema kwa watu waliomsikiliza, akaingia Kapernaumu.
2 tadA zatasenApateH priyadAsa eko mRtakalpaH pIDita AsIt|
Mtumwa fulani wa akida, aliyekuwa wa thamani sana kwake, alikuwa mgonjwa sana na alikuwa karibu ya kufa.
3 ataH senApati ryIzo rvArttAM nizamya dAsasyArogyakaraNAya tasyAgamanArthaM vinayakaraNAya yihUdIyAn kiyataH prAcaH preSayAmAsa|
Lakini akiwa amesikia kuhusu Yesu, yule Akida alimtuma kiongozi wa kiyahudi, kumwomba aje kumwokoa mtumwa wake ili asife.
4 te yIzorantikaM gatvA vinayAtizayaM vaktumArebhire, sa senApati rbhavatonugrahaM prAptum arhati|
Walipofika karibu na Yesu, walimsihi kwa bidii na kusema, “anastahili kwamba unapaswa kufanya hivi kwa ajili yake,
5 yataH sosmajjAtIyeSu lokeSu prIyate tathAsmatkRte bhajanagehaM nirmmitavAn|
kwa sababu analipenda taifa letu, na ndiye aliyejenga sinagogi kwa ajili yetu”.
6 tasmAd yIzustaiH saha gatvA nivezanasya samIpaM prApa, tadA sa zatasenApati rvakSyamANavAkyaM taM vaktuM bandhUn prAhiNot| he prabho svayaM zramo na karttavyo yad bhavatA madgehamadhye pAdArpaNaM kriyeta tadapyahaM nArhAmi,
Yesu akaendelea na safari yake pamoja nao. lakini kabla hajaenda mbali na nyumba, afisa mmoja aliwatuma marafiki zake kuzungumza naye. “Bwana, usijichoshe mwenyewe kwa sababu mimi sistahili wewe kuingia kwenye dari yangu.
7 kiJcAhaM bhavatsamIpaM yAtumapi nAtmAnaM yogyaM buddhavAn, tato bhavAn vAkyamAtraM vadatu tenaiva mama dAsaH svastho bhaviSyati|
Kwa sababu hii sikufikiria hata mimi mwenyewe kuwa ninafaa kuja kwako, lakini sema neno tu na mtumishi wangu atapona.
8 yasmAd ahaM parAdhInopi mamAdhInA yAH senAH santi tAsAm ekajanaM prati yAhIti mayA prokte sa yAti; tadanyaM prati AyAhIti prokte sa AyAti; tathA nijadAsaM prati etat kurvviti prokte sa tadeva karoti|
Kwani mimi pia ni mtu niliyewekwa kwenye mamlaka na nina askari chini yangu. Husema kwa huyu “Nenda” na huenda, na kwa mwingine, “Njoo” naye huja, na kwa mtumishi wangu 'Fanya hiki', na yeye hufanya”.
9 yIzuridaM vAkyaM zrutvA vismayaM yayau, mukhaM parAvartya pazcAdvarttino lokAn babhASe ca, yuSmAnahaM vadAmi isrAyelo vaMzamadhyepi vizvAsamIdRzaM na prApnavaM|
Yesu aliposikia haya alishangaa, na kuwageukia makutano waliokuwa wanamfuata na kusema.”Nawaambia, hata katika Israeli, sijawahi kuona mtu mwenye imani kuu kama huyu.
10 tataste preSitA gRhaM gatvA taM pIDitaM dAsaM svasthaM dadRzuH|
Kisha wale waliokuwa wametumwa walirudi nyumbani na kumkuta mtumishi akiwa mzima.
11 pare'hani sa nAyInAkhyaM nagaraM jagAma tasyAneke ziSyA anye ca lokAstena sArddhaM yayuH|
fulani baada ya haya, ilitokea kuwa Yesu alikuwa anasafiri kwenda mji ulioitwa Naini. wanafunzi wake wakaenda pamoja naye wakiambana na umati wa watu.
12 teSu tannagarasya dvArasannidhiM prApteSu kiyanto lokA ekaM mRtamanujaM vahanto nagarasya bahiryAnti, sa tanmAturekaputrastanmAtA ca vidhavA; tayA sArddhaM tannagarIyA bahavo lokA Asan|
Alipofika karibu na Lango la jiji tazama, mtu aliyekufa alikuwa amebebwa, na ni mtoto wa pekee kwa mama yake. aliyekuwa mjane, na umati wa wawakilishi kutoka kwenye jiji walikuwa pamoja naye.
13 prabhustAM vilokya sAnukampaH kathayAmAsa, mA rodIH| sa samIpamitvA khaTvAM pasparza tasmAd vAhakAH sthagitAstamyuH;
Alipomwona, Bwana akamsogelea kwa huruma kubwa sana juu yake na akamwambia, “Usilie”.
14 tadA sa uvAca he yuvamanuSya tvamuttiSTha, tvAmaham AjJApayAmi|
Kisha akasogea mbele akaligusa jeneza ambalo walibebea mwili, na wale waliobeba wakasimama akasema “Kijana nasema amka”
15 tasmAt sa mRto janastatkSaNamutthAya kathAM prakathitaH; tato yIzustasya mAtari taM samarpayAmAsa|
Mfu akainuka na kukaa chini na akaanza kuongea. Kisha Yesu akamkabidhi kwa mama yake.
16 tasmAt sarvve lokAH zazaGkire; eko mahAbhaviSyadvAdI madhye'smAkam samudait, Izvarazca svalokAnanvagRhlAt kathAmimAM kathayitvA IzvaraM dhanyaM jagaduH|
Kisha hofu ikawajaa wote. wakaendelea kumtukuza Mungu wakisema “Nabii mkuu ameinuliwa miongoni mwetu” na “Mungu amewaangalia watu wake”
17 tataH paraM samastaM yihUdAdezaM tasya caturdiksthadezaJca tasyaitatkIrtti rvyAnaze|
Hizi habari njema za Yesu zilienea Yudea yote na kwa mikoa yote ya jirani.
18 tataH paraM yohanaH ziSyeSu taM tadvRttAntaM jJApitavatsu
Wanafunzi wa Yohana walimwamwambia mambo haya yote.
19 sa svaziSyANAM dvau janAvAhUya yIzuM prati vakSyamANaM vAkyaM vaktuM preSayAmAsa, yasyAgamanam apekSya tiSThAmo vayaM kiM sa eva janastvaM? kiM vayamanyamapekSya sthAsyAmaH?
Ndipo Yohana akawaita wawili wa wanafunzi wake na kuwatuma kwa Bwana kusema “Wewe ndiye yule ajaye, au kuna mtu mwingine tumtazamie?
20 pazcAttau mAnavau gatvA kathayAmAsatuH, yasyAgamanam apekSya tiSThAmo vayaM, kiM saeva janastvaM? kiM vayamanyamapekSya sthAsyAmaH? kathAmimAM tubhyaM kathayituM yohan majjaka AvAM preSitavAn|
Walipofika karibu na Yesu hawa wakasema, “Yohana mbatizaji ametutuma kwako kusema, 'Wewe ni yule ajaye au kuna mtu mwingine tumtazamie?”
21 tasmin daNDe yIzUrogiNo mahAvyAdhimato duSTabhUtagrastAMzca bahUn svasthAn kRtvA, anekAndhebhyazcakSuMSi dattvA pratyuvAca,
kwa wakati huo aliowaponya watu wengi kutoka katika magonjwa na mateso, kutoka kwa roho wachafu, na kwa watu wenye upofu aliwapa kuona.
22 yuvAM vrajatam andhA netrANi khaJjAzcaraNAni ca prApnuvanti, kuSThinaH pariSkriyante, badhirAH zravaNAni mRtAzca jIvanAni prApnuvanti, daridrANAM samIpeSu susaMvAdaH pracAryyate, yaM prati vighnasvarUpohaM na bhavAmi sa dhanyaH,
Yesu akajibu na kusema kwao. “Baada ya kuwa mmekwenda mlikotoka mtamjulisha Yohana mlichokiona na kukisikia. Wenye upofu wanapokea kuona na viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakasika, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa na kuwa hai tena, masikini wanaambiwa habari njema.
23 etAni yAni pazyathaH zRNuthazca tAni yohanaM jJApayatam|
Na mtu ambaye hataacha kuniamini mimi kwa sababu ya matendo yangu amebarikiwa”.
24 tayo rdUtayo rgatayoH sato ryohani sa lokAn vaktumupacakrame, yUyaM madhyeprAntaraM kiM draSTuM niragamata? kiM vAyunA kampitaM naDaM?
Baada ya wale waliotumwa na Yohana kurudi walikotoka, Yesu akaanza kusema kwa makutano juu ya Yohana, “Mlikwenda nje kuona nini, mwanzi ukiwa unatikiswa na upepo?
25 yUyaM kiM draSTuM niragamata? kiM sUkSmavastraparidhAyinaM kamapi naraM? kintu ye sUkSmamRduvastrANi paridadhati sUttamAni dravyANi bhuJjate ca te rAjadhAnISu tiSThanti|
lakini mlikwenda nje kuona nini, mtu aliyevaa vizuri? tazama watu wale wanaovaa mavazi ya kifalme na kuishi maisha ya starehe wako kwenye nafasi za wafalme.
26 tarhi yUyaM kiM draSTuM niragamata? kimekaM bhaviSyadvAdinaM? tadeva satyaM kintu sa pumAn bhaviSyadvAdinopi zreSTha ityahaM yuSmAn vadAmi;
lakini mnakwenda nje kuona nini, Nabii? Ndiyo, ninasema kwenu na zaidi sana kuliko nabii.
27 pazya svakIyadUtantu tavAgra preSayAmyahaM| gatvA tvadIyamArgantu sa hi pariSkariSyati| yadarthe lipiriyam Aste sa eva yohan|
Huyu ndiye aliyeandikiwa, “Tazama, namtuma mjumbe wangu mbele ya macho yenu, atakeyeandaa njia kwa ajili yangu,
28 ato yuSmAnahaM vadAmi striyA garbbhajAtAnAM bhaviSyadvAdinAM madhye yohano majjakAt zreSThaH kopi nAsti, tatrApi Izvarasya rAjye yaH sarvvasmAt kSudraH sa yohanopi zreSThaH|
Nasema kwenu, kati ya wale waliozaliwa na mwanamke, hakuna mkuu kama Yohana, lakini mtu asiye muhimu sana atakayeishi na Mungu mahali alipo yeye, atakuwa mkuu kuliko Yohana.”
29 aparaJca sarvve lokAH karamaJcAyinazca tasya vAkyAni zrutvA yohanA majjanena majjitAH paramezvaraM nirdoSaM menire|
Na watu wote waliposikia haya pamoja na watoza ushuru, walitangaza kuwa Mungu ni mwenye Haki. Walikuwepo kati yao wale waliobatizwa kwa ubatizo wa Yohana.
30 kintu phirUzino vyavasthApakAzca tena na majjitAH svAn pratIzvarasyopadezaM niSphalam akurvvan|
Lakini mafarisayo na wataalamu wa sheria za kiyahudi, ambao hawakubatizwa na yeye walikataa hekima za Mungu kwa ajili yao wenyewe.
31 atha prabhuH kathayAmAsa, idAnIntanajanAn kenopamAmi? te kasya sadRzAH?
Tena naweza kuwalinganisha na nini watu wa kizazi hiki? Wakoje hasai?
32 ye bAlakA vipaNyAm upavizya parasparam AhUya vAkyamidaM vadanti, vayaM yuSmAkaM nikaTe vaMzIravAdiSma, kintu yUyaM nAnarttiSTa, vayaM yuSmAkaM nikaTa arodiSma, kintu yuyaM na vyalapiSTa, bAlakairetAdRzaisteSAm upamA bhavati|
Wanafanana na watoto wanaocheza kwenye eneo la soko, wanaokaa na kuitana mmoja baada wa mwingine wakisema, 'Tumepuliza filimbi kwa ajili yenu, na hamkucheza. tumeomboleza na hamkulia.'
33 yato yohan majjaka Agatya pUpaM nAkhAdat drAkSArasaJca nApivat tasmAd yUyaM vadatha, bhUtagrastoyam|
Yohana mbatizaji alikuja hakula mkate wala hakunywa divai, na mkasema “Ana pepo.
34 tataH paraM mAnavasuta AgatyAkhAdadapivaJca tasmAd yUyaM vadatha, khAdakaH surApazcANDAlapApinAM bandhureko jano dRzyatAm|
Mwana wa Mtu amekuja amekula na kunywa na mkasema, “Angali ni mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na wenye dhambi!
35 kintu jJAnino jJAnaM nirdoSaM viduH|
Lakini hekima imetambulika kuwa ina haki kwa watoto wake wote.”
36 pazcAdekaH phirUzI yIzuM bhojanAya nyamantrayat tataH sa tasya gRhaM gatvA bhoktumupaviSTaH|
Mmoja wa mafarisayo alimwomba Yesu aende kula pamoja naye. Baada ya Yesu kuingia kwenye nyumba ya farisayo, aliegemea kwenye meza ili ale.
37 etarhi tatphirUzino gRhe yIzu rbhektum upAvekSIt tacchrutvA tannagaravAsinI kApi duSTA nArI pANDaraprastarasya sampuTake sugandhitailam AnIya
Tazama kulikuwa na mwanamke mmoja katika jiji hilo aliyekuwa na dhambi. Akagundua kuwa alikuwa amekaa kwa Farisayo, akaleta chupa ya manukato.
38 tasya pazcAt pAdayoH sannidhau tasyau rudatI ca netrAmbubhistasya caraNau prakSAlya nijakacairamArkSIt, tatastasya caraNau cumbitvA tena sugandhitailena mamarda|
Alisimama nyuma yake karibu na miguu yake huku akilia. Tena alianza kulowanisha miguu yake kwa machozi, na kuifuta kwa nywele za kichwa chake, akiibusu miguu yake na kuipaka manukato.
39 tasmAt sa nimantrayitA phirUzI manasA cintayAmAsa, yadyayaM bhaviSyadvAdI bhavet tarhi enaM spRzati yA strI sA kA kIdRzI ceti jJAtuM zaknuyAt yataH sA duSTA|
Na yule farisayo aliyekuwa amemwalika Yesu alipoona hivyo, akawaza mwenyewe akisema, “Kama huyu mtu angekuwa nabii, angejua huyu ni nani na ni aina gani ya mwanamke anayemgusa, ya kuwa ni mwenye dhambi.
40 tadA yAzustaM jagAda, he zimon tvAM prati mama kiJcid vaktavyamasti; tasmAt sa babhASe, he guro tad vadatu|
Yesu akajibu na kumwambia, “Simoni nina kitu cha kukuambia. “Akasema” “Kiseme tu mwalimu!”
41 ekottamarNasya dvAvadhamarNAvAstAM, tayorekaH paJcazatAni mudrApAdAn aparazca paJcAzat mudrApAdAn dhArayAmAsa|
Yesu akasema “Kulikuwa na wadaiwa wawili kwa mkopeshaji mmoja. Mmoja alikuwa anadaiwa dinari mia tano na wa pili alidaiwa dinari hamsini.
42 tadanantaraM tayoH zodhyAbhAvAt sa uttamarNastayo rRNe cakSame; tasmAt tayordvayoH kastasmin preSyate bahu? tad brUhi|
Na walipokuwa hawana pesa ya kumlipa aliwasamehe wote. Sasa ni nani atampenda zaidi?
43 zimon pratyuvAca, mayA budhyate yasyAdhikam RNaM cakSame sa iti; tato yIzustaM vyAjahAra, tvaM yathArthaM vyacArayaH|
Simoni akamjibu na kusema, “Nadhani aliyesamehewa zaidi.”Yesu akamwambia, “Umehukumu kwa usahihi.”
44 atha tAM nArIM prati vyAghuThya zimonamavocat, strImimAM pazyasi? tava gRhe mayyAgate tvaM pAdaprakSAlanArthaM jalaM nAdAH kintu yoSideSA nayanajalai rmama pAdau prakSAlya kezairamArkSIt|
Yesu akamgeukia mwanamke na kusema kwa Simoni, “Unamwona huyu mwanamke. Nimeingia kwenye Nyumba yako. Hukunipa maji kwa ajili ya miguu yangu, lakini huyu, kwa machozi yake, alilowanisha miguu yangu na kuifuta kwa nywele zake.
45 tvaM mAM nAcumbIH kintu yoSideSA svIyAgamanAdArabhya madIyapAdau cumbituM na vyaraMsta|
Hukunibusu, lakini yeye, tangu alipoingia humu hakuacha kunibusu miguu yangu.
46 tvaJca madIyottamAGge kiJcidapi tailaM nAmardIH kintu yoSideSA mama caraNau sugandhitailenAmarddIt|
Hukuipaka miguu yangu kwa mafuta, lakini ameipaka miguu yangu kwa manukato.
47 atastvAM vyAharAmi, etasyA bahu pApamakSamyata tato bahu prIyate kintu yasyAlpapApaM kSamyate solpaM prIyate|
Kwa jambo hili, nakwambia kwamba alikuwa na dhambi nyingi na amesamehewa zaidi, na pia alipenda zaidi. Lakini aliyesamehewa kidogo, hupenda kidogo tu.”
48 tataH paraM sa tAM babhASe, tvadIyaM pApamakSamyata|
Baadaye akamwambia mwanamke, “Dhambi zako zimesamehewa”
49 tadA tena sArddhaM ye bhoktum upavivizuste parasparaM vaktumArebhire, ayaM pApaM kSamate ka eSaH?
Wale waliokaa mezani pamoja naye wakaanza kusemezana wao kwa wao, “Huyu ni nani mpaka anasamehe dhambi?”
50 kintu sa tAM nArIM jagAda, tava vizvAsastvAM paryyatrAsta tvaM kSemeNa vraja|
Na Yesu akamwambia mwanamke, “Imani yako imekuokoa. Enenda kwa amani”

< lUkaH 7 >