< mArkaH 1 >

1 Izvaraputrasya yIzukhrISTasya susaMvAdArambhaH|
Huu ni mwanzo wa injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
2 bhaviSyadvAdinAM granthESu lipiritthamAstE, pazya svakIyadUtantu tavAgrE prESayAmyaham| gatvA tvadIyapanthAnaM sa hi pariSkariSyati|
Kama ilivyoandikwa na nabii Isaya, “Tazama, ninamtuma mjumbe wangu mbele yako, mmoja atakayetayarisha njia yako.
3 "paramEzasya panthAnaM pariSkuruta sarvvataH| tasya rAjapathanjcaiva samAnaM kurutAdhunA|" ityEtat prAntarE vAkyaM vadataH kasyacidravaH||
Sauti ya mtu aitaye nyikani, “Ikamilisheni njia ya Bwana; zinyosheni njia zake”.
4 saEva yOhan prAntarE majjitavAn tathA pApamArjananimittaM manOvyAvarttakamajjanasya kathAnjca pracAritavAn|
Yohana alikuja, akibatiza nyikani na kuhubiri ubatizo wa toba kwa msamaha wa dhambi.
5 tatO yihUdAdEzayirUzAlamnagaranivAsinaH sarvvE lOkA bahi rbhUtvA tasya samIpamAgatya svAni svAni pApAnyaggIkRtya yarddananadyAM tEna majjitA babhUvuH|
Nchi yote ya Yudea na watu wote wa Yerusalemu walikwenda kwake. Walikuwa wakibatizwa naye katika mto Yordani, wakiungama dhambi zao.
6 asya yOhanaH paridhEyAni kramElakalOmajAni, tasya kaTibandhanaM carmmajAtam, tasya bhakSyANi ca zUkakITA vanyamadhUni cAsan|
Yohana alikuwa anavaa vazi la manyoya ya ngamia na mkanda wa ngozi kiunoni mwake, na alikuwa anakula nzige na asali ya porini.
7 sa pracArayan kathayAnjcakrE, ahaM namrIbhUya yasya pAdukAbandhanaM mOcayitumapi na yOgyOsmi, tAdRzO mattO gurutara EkaH puruSO matpazcAdAgacchati|
Alihubiri na kusema, “Yupo mmoja anakuja baada yangu mwenye nguvu zaidi kuliko mimi, na sina hadhi hata ya kuinama chini na kufungua kamba za viatu vyake.
8 ahaM yuSmAn jalE majjitavAn kintu sa pavitra AtmAni saMmajjayiSyati|
Mimi niliwabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza ninyi kwa Roho Mtakatifu.”
9 aparanjca tasminnEva kAlE gAlIlpradEzasya nAsaradgrAmAd yIzurAgatya yOhanA yarddananadyAM majjitO'bhUt|
Ilitokea katika siku hizo kwamba Yesu alikuja kutoka Nazareti ya Galilaya, na alibatizwa na Yohana katika mto Yordani.
10 sa jalAdutthitamAtrO mEghadvAraM muktaM kapOtavat svasyOpari avarOhantamAtmAnanjca dRSTavAn|
Wakati Yesu alipoinuka kutoka majini, aliona mbingu zimegawanyika wazi na Roho akishuka chini juu yake kama njiwa.
11 tvaM mama priyaH putrastvayyEva mamamahAsantOSa iyamAkAzIyA vANI babhUva|
Na sauti ilitoka mbinguni, “Wewe ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa sana na wewe.”
12 tasmin kAlE AtmA taM prAntaramadhyaM ninAya|
Kisha mara moja Roho akamlazimisha kwenda nyikani.
13 atha sa catvAriMzaddinAni tasmin sthAnE vanyapazubhiH saha tiSThan zaitAnA parIkSitaH; pazcAt svargIyadUtAstaM siSEvirE|
Alikuwako nyikani siku arobaini, akijaribiwa na Shetani. Alikuwa pamoja na wanyama wa mwituni, na malaika walimhudumia.
14 anantaraM yOhani bandhanAlayE baddhE sati yIzu rgAlIlpradEzamAgatya IzvararAjyasya susaMvAdaM pracArayan kathayAmAsa,
Sasa baada ya Yohana kukamatwa, Yesu alikuja Galilaya akitangaza injili ya Mungu,
15 kAlaH sampUrNa IzvararAjyanjca samIpamAgataM; atOhEtO ryUyaM manAMsi vyAvarttayadhvaM susaMvAdE ca vizvAsita|
akisema, “Muda umetimia, na ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuamini katika injili”.
16 tadanantaraM sa gAlIlIyasamudrasya tIrE gacchan zimOn tasya bhrAtA andriyanAmA ca imau dvau janau matsyadhAriNau sAgaramadhyE jAlaM prakSipantau dRSTvA tAvavadat,
Na akipita kando ya bahari ya Galilaya, alimwona Simoni na Andrea ndugu wa Simoni wakitupa nyavu zao katika bahari, kwa kuwa walikuwa wavuvi.
17 yuvAM mama pazcAdAgacchataM, yuvAmahaM manuSyadhAriNau kariSyAmi|
Yesu aliwaambia, “Njoni, nifuateni, na nitawafanya wavuvi wa watu.”
18 tatastau tatkSaNamEva jAlAni parityajya tasya pazcAt jagmatuH|
Na mara moja waliacha nyavu na wakamfuata.
19 tataH paraM tatsthAnAt kinjcid dUraM gatvA sa sivadIputrayAkUb tadbhrAtRyOhan ca imau naukAyAM jAlAnAM jIrNamuddhArayantau dRSTvA tAvAhUyat|
Wakati Yesu alipotembea umbali kidogo, alimwona Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana ndugu yake; walikuwa kwenye mtumbwi wakitengeneza nyavu.
20 tatastau naukAyAM vEtanabhugbhiH sahitaM svapitaraM vihAya tatpazcAdIyatuH|
Mara aliwaita na wao walimwacha baba yao Zebedayo ndani ya mtumbwi na watumishi waliokodiwa, wakamfuata.
21 tataH paraM kapharnAhUmnAmakaM nagaramupasthAya sa vizrAmadivasE bhajanagrahaM pravizya samupadidEza|
Na walipofika Kaperinaumu, siku ya Sabato, Yesu aliingia kwenye sinagogi na kufundisha.
22 tasyOpadEzAllOkA AzcaryyaM mEnirE yataH sOdhyApakAiva nOpadizan prabhAvavAniva prOpadidEza|
Walilishangaa fundisho lake, kwa vile alikuwa akiwafundisha kama mtu ambaye ana mamlaka na siyo kama waandishi.
23 aparanjca tasmin bhajanagRhE apavitrabhUtEna grasta EkO mAnuSa AsIt| sa cItzabdaM kRtvA kathayAnjcakE
Wakati huo huo kulikuwa na mtu katika sinagogi lao aliyekuwa na roho mchafu, na alipiga kelele,
24 bhO nAsaratIya yIzO tvamasmAn tyaja, tvayA sahAsmAkaM kaH sambandhaH? tvaM kimasmAn nAzayituM samAgataH? tvamIzvarasya pavitralOka ityahaM jAnAmi|
akisema, “Tuna nini cha kufanya na wewe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Nakujua u nani. Wewe ni Mtakatifu pekee wa Mungu!”
25 tadA yIzustaM tarjayitvA jagAda tUSNIM bhava itO bahirbhava ca|
Yesu alimkemea pepo na kusema, “Nyamaza na utoke ndani yake!”
26 tataH sO'pavitrabhUtastaM sampIPya atyucaizcItkRtya nirjagAma|
Na roho mchafu alimwangusha chini na akatoka kwake wakati akilia kwa sauti ya juu.
27 tEnaiva sarvvE camatkRtya parasparaM kathayAnjcakrirE, ahO kimidaM? kIdRzO'yaM navya upadEzaH? anEna prabhAvEnApavitrabhUtESvAjnjApitESu tE tadAjnjAnuvarttinO bhavanti|
Na watu wote walishangaa, hivyo wakaulizana kila mmoja, “Hii ni nini? Fundisho jipya lenye mamlaka? Hata huamuru pepo wachafu nao wanamtii!”
28 tadA tasya yazO gAlIlazcaturdiksthasarvvadEzAn vyApnOt|
Na habari kuhusu yeye mara moja zikasambaa kila mahali ndani ya mkoa wote wa Galilaya.
29 aparanjca tE bhajanagRhAd bahi rbhUtvA yAkUbyOhanbhyAM saha zimOna Andriyasya ca nivEzanaM pravivizuH|
Na mara moja baada ya kutoka nje ya sinagogi, waliingia nyumbani mwa Simoni na Andrea wakiwa na Yakobo na Yohana.
30 tadA pitarasya zvazrUrjvarapIPitA zayyAyAmAsta iti tE taM jhaTiti vijnjApayAnjcakruH|
Sasa mama mkwe wa Simoni alikuwa amelala mgonjwa wa homa, na mara moja walimwambia Yesu habari zake.
31 tataH sa Agatya tasyA hastaM dhRtvA tAmudasthApayat; tadaiva tAM jvarO'tyAkSIt tataH paraM sA tAn siSEvE|
Hivyo alikuja, alimshika kwa mkono, na kumwinua juu; homa ikaondoka kwake, na akaanza kuwahudumia.
32 athAstaM gatE ravau sandhyAkAlE sati lOkAstatsamIpaM sarvvAn rOgiNO bhUtadhRtAMzca samAninyuH|
Jioni hiyo wakati jua limekwisha zama, walimletea kwake wote waliokuwa wagonjwa, au waliopagawa na pepo.
33 sarvvE nAgarikA lOkA dvAri saMmilitAzca|
Mji wote walikusanyika pamoja katika mlango.
34 tataH sa nAnAvidharOgiNO bahUn manujAnarOgiNazcakAra tathA bahUn bhUtAn tyAjayAnjcakAra tAn bhUtAn kimapi vAkyaM vaktuM niSiSEdha ca yatOhEtOstE tamajAnan|
Aliwaponya wengi waliokuwa wagonjwa wa magonjwa mbalimbali na kutoa pepo wengi, bali hakuruhusu pepo kuongea kwa sababu walimjua.
35 aparanjca sO'tipratyUSE vastutastu rAtrizESE samutthAya bahirbhUya nirjanaM sthAnaM gatvA tatra prArthayAnjcakrE|
Aliamka asubuhi na mapema, wakati ilikuwa bado giza; aliondoka na kwenda mahali pa faragha na aliomba huko.
36 anantaraM zimOn tatsagginazca tasya pazcAd gatavantaH|
Simoni na wote waliokuwa pamoja naye walimtafuta.
37 taduddEzaM prApya tamavadan sarvvE lOkAstvAM mRgayantE|
Walimpata na wakamwambia, “Kila mmoja anakutafuta”
38 tadA sO'kathayat Agacchata vayaM samIpasthAni nagarANi yAmaH, yatO'haM tatra kathAM pracArayituM bahirAgamam|
Aliwaambia, “Twendeni mahali pengine, nje katika miji inayozunguka, ili niweze kuhubiri huko pia. Ndiyo sababu nilikuja hapa.”
39 atha sa tESAM gAlIlpradEzasya sarvvESu bhajanagRhESu kathAH pracArayAnjcakrE bhUtAnatyAjayanjca|
Alikwenda akipita Galilaya yote, akihubiri katika masinagogi yao na kukemea pepo.
40 anantaramEkaH kuSThI samAgatya tatsammukhE jAnupAtaM vinayanjca kRtvA kathitavAn yadi bhavAn icchati tarhi mAM pariSkarttuM zaknOti|
Mwenye ukoma mmoja alikuja kwake. Alikuwa akimsihi; alipiga magoti na alimwambia, “Kama unataka, waweza kunifanya niwe safi.”
41 tataH kRpAlu ryIzuH karau prasAryya taM spaSTvA kathayAmAsa
Akisukumwa na huruma, Yesu alinyosha mkono wake na kumgusa, akimwambia, “Ninataka. Uwe msafi.”
42 mamEcchA vidyatE tvaM pariSkRtO bhava| EtatkathAyAH kathanamAtrAt sa kuSThI rOgAnmuktaH pariSkRtO'bhavat|
Mara moja ukoma ukamtoka, na alifanywa kuwa safi.
43 tadA sa taM visRjan gAPhamAdizya jagAda
Yesu akamwonya vikali na akamwambia aende mara moja,
44 sAvadhAnO bhava kathAmimAM kamapi mA vada; svAtmAnaM yAjakaM darzaya, lOkEbhyaH svapariSkRtEH pramANadAnAya mUsAnirNItaM yaddAnaM tadutsRjasva ca|
Alimwambia, “Hakikisha hausemi neno kwa yeyote, lakini nenda, ujionyeshe kwa kuhani, na utoe dhabihu kwa ajili ya utakaso ambayo Musa aliagiza, kama ushuhuda kwao.”
45 kintu sa gatvA tat karmma itthaM vistAryya pracArayituM prArEbhE tEnaiva yIzuH punaH saprakAzaM nagaraM pravESTuM nAzaknOt tatOhEtOrbahiH kAnanasthAnE tasyau; tathApi caturddigbhyO lOkAstasya samIpamAyayuH|
Lakini alikwenda na kuanza kumwambia kila mmoja na kueneza neno zaidi hata Yesu hakuweza tena kuingia mjini kwa uhuru. Hivyo alikaa mahali pa faragha na watu walikuja kwake kutoka kila mahali.

< mArkaH 1 >