< lUkaH 3 >

1 anantaraM tibiriyakaisarasya rAjatvasya panjcadazE vatsarE sati yadA pantIyapIlAtO yihUdAdEzAdhipati rhErOd tu gAlIlpradEzasya rAjA philipanAmA tasya bhrAtA tu yitUriyAyAstrAkhOnItiyApradEzasya ca rAjAsIt luSAnIyanAmA avilInIdEzasya rAjAsIt
Mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alikuwa anatawala mkoa wa Yudea. Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo, ndugu yake, alikuwa mkuu wa mikoa ya Iturea na Trakoniti. Lusania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
2 hAnan kiyaphAzcEmau pradhAnayAjAkAvAstAM tadAnIM sikhariyasya putrAya yOhanE madhyEprAntaram Izvarasya vAkyE prakAzitE sati
na Anasi na Kayafa walikuwa makuhani wakuu mjini Yerusalem. Wakati huo ndipo neno la Mungu lilipomjia Yohane, mwana wa Zakariya, kule jangwani.
3 sa yarddana ubhayataTapradEzAn samEtya pApamOcanArthaM manaHparAvarttanasya cihnarUpaM yanmajjanaM tadIyAH kathAH sarvvatra pracArayitumArEbhE|
Basi, Yohane akaenda katika sehemu zote zilizopakana na mto Yordani, akihubiri watu watubu na kubatizwa ili Mungu awaondolee dhambi.
4 yizayiyabhaviSyadvaktRgranthE yAdRzI lipirAstE yathA, paramEzasya panthAnaM pariSkuruta sarvvataH| tasya rAjapathanjcaiva samAnaM kurutAdhunA|
Ndivyo ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake; nyosheni mapito yake.
5 kAriSyantE samucchrAyAH sakalA nimnabhUmayaH| kAriSyantE natAH sarvvE parvvatAzcOpaparvvatAH| kAriSyantE ca yA vakrAstAH sarvvAH saralA bhuvaH| kAriSyantE samAnAstA yA uccanIcabhUmayaH|
Kila bonde litafukiwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa; palipopindika patanyooshwa, njia mbaya zitatengenezwa.
6 IzvarENa kRtaM trANaM drakSyanti sarvvamAnavAH| ityEtat prAntarE vAkyaM vadataH kasyacid ravaH||
Na, watu wote watauona wokovu utokao kwa Mungu.”
7 yE yE lOkA majjanArthaM bahirAyayustAn sOvadat rE rE sarpavaMzA AgAminaH kOpAt palAyituM yuSmAn kazcEtayAmAsa?
Basi, Yohane akawa anawaambia watu wengi waliofika ili awabatize: “Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mngeweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?
8 tasmAd ibrAhIm asmAkaM pitA kathAmIdRzIM manObhi rna kathayitvA yUyaM manaHparivarttanayOgyaM phalaM phalata; yuSmAnahaM yathArthaM vadAmi pASANEbhya EtEbhya Izvara ibrAhImaH santAnOtpAdanE samarthaH|
Basi, onyesheni kwa matendo kwamba mmetubu. Msianze sasa kusema: Sisi ni watoto wa Abrahamu. Nawaambieni hakika, Mungu anaweza kuyageuza mawe haya yawe watoto wa Abrahamu!
9 aparanjca tarumUlE'dhunApi parazuH saMlagnOsti yastaruruttamaM phalaM na phalati sa chidyatE'gnau nikSipyatE ca|
Lakini, sasa hivi shoka limewekwa tayari kukata mizizi ya miti. Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.”
10 tadAnIM lOkAstaM papracchustarhi kiM karttavyamasmAbhiH?
Umati wa watu ukamwuliza, “Tufanye nini basi?”
11 tataH sOvAdIt yasya dvE vasanE vidyEtE sa vastrahInAyaikaM vitaratu kiMnjca yasya khAdyadravyaM vidyatE sOpi tathaiva karOtu|
Akawajibu, “Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo.”
12 tataH paraM karasanjcAyinO majjanArtham Agatya papracchuH hE gurO kiM karttavyamasmAbhiH?
Nao watoza ushuru wakaja pia ili wabatizwe, wakamwuliza, “Mwalimu, tufanye nini?”
13 tataH sOkathayat nirUpitAdadhikaM na gRhlita|
Naye akawaambia, “Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa.”
14 anantaraM sEnAgaNa Etya papraccha kimasmAbhi rvA karttavyam? tataH sObhidadhE kasya kAmapi hAniM mA kArSTa tathA mRSApavAdaM mA kuruta nijavEtanEna ca santuSya tiSThata|
Nao askari wakamwuliza, “Na sisi tufanye nini?” Naye akawajibu, “Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu.”
15 aparanjca lOkA apEkSayA sthitvA sarvvEpIti manObhi rvitarkayAnjcakruH, yOhanayam abhiSiktastrAtA na vEti?
Wote walikuwa wanatazamia kitu fulani; basi, wakaanza kujiuliza mioyoni mwao kuhusu Yohane: kuwa labda yeye ndiye Kristo.
16 tadA yOhan sarvvAn vyAjahAra, jalE'haM yuSmAn majjayAmi satyaM kintu yasya pAdukAbandhanaM mOcayitumapi na yOgyOsmi tAdRza EkO mattO gurutaraH pumAn Eti, sa yuSmAn vahnirUpE pavitra Atmani majjayiSyati|
Hapo Yohane akawaambia wote, “Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi ambaye sistahili hata kumfungulia kamba za viatu vyake. Yeye atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17 aparanjca tasya hastE zUrpa AstE sa svazasyAni zuddharUpaM prasphOTya gOdhUmAn sarvvAn bhANPAgArE saMgrahISyati kintu bUSANi sarvvANyanirvvANavahninA dAhayiSyati|
Yeye ni kama mtu anayeshika mikononi mwake chombo cha kupuria nafaka, aipure nafaka yake, akusanye ngano ghalani mwake, na makapi ayachome kwa moto usiozimika.”
18 yOhan upadEzEnEtthaM nAnAkathA lOkAnAM samakSaM pracArayAmAsa|
Hivyo, pamoja na mawaidha mengine mengi, Yohane aliwahimiza watu akiwahubiria Habari Njema.
19 aparanjca hErOd rAjA philipnAmnaH sahOdarasya bhAryyAM hErOdiyAmadhi tathAnyAni yAni yAni kukarmmANi kRtavAn tadadhi ca
Lakini Yohane alimgombeza Herode, mkuu wa mkoa, kwa sababu alikuwa amemchukua Herodia, mke wa ndugu yake, na kumfanya mke wake; na pia kwa ajili ya mabaya yote aliyokuwa amefanya.
20 yOhanA tiraskRtO bhUtvA kArAgArE tasya bandhanAd aparamapi kukarmma cakAra|
Kisha Herode akazidisha ubaya wake kwa kumtia Yohane gerezani.
21 itaH pUrvvaM yasmin samayE sarvvE yOhanA majjitAstadAnIM yIzurapyAgatya majjitaH|
Watu wote walipokuwa wamekwisha batizwa, Yesu naye alibatizwa. Na alipokuwa akisali, mbingu zilifunguka,
22 tadanantaraM tEna prArthitE mEghadvAraM muktaM tasmAcca pavitra AtmA mUrttimAn bhUtvA kapOtavat taduparyyavarurOha; tadA tvaM mama priyaH putrastvayi mama paramaH santOSa ityAkAzavANI babhUva|
na Roho Mtakatifu akamshukia akiwa na umbo kama la njiwa. Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ndiwe Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
23 tadAnIM yIzuH prAyENa triMzadvarSavayaska AsIt| laukikajnjAnE tu sa yUSaphaH putraH,
Yesu alipoanza kazi yake hadharani, alikuwa na umri upatao miaka thelathini, na watu walidhani yeye ni mwana wa Yosefu, mwana wa Heli.
24 yUSaph ElEH putraH, ElirmattataH putraH, mattat lEvEH putraH, lEvi rmalkEH putraH, malkiryAnnasya putraH; yAnnO yUSaphaH putraH|
Heli alikuwa mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yanai, mwana wa Yosefu,
25 yUSaph mattathiyasya putraH, mattathiya AmOsaH putraH, AmOs nahUmaH putraH, nahUm iSlEH putraH iSlirnagEH putraH|
mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Hesli, mwana wa Nagai,
26 nagirmATaH putraH, mAT mattathiyasya putraH, mattathiyaH zimiyEH putraH, zimiyiryUSaphaH putraH, yUSaph yihUdAH putraH|
mwana wa Maathi, mwana wa Matathia, mwana wa Shemeni, mwana wa Yoseki, mwana wa Yuda,
27 yihUdA yOhAnAH putraH, yOhAnA rISAH putraH, rISAH sirubbAbilaH putraH, sirubbAbil zaltIyElaH putraH, zaltIyEl nErEH putraH|
mwana wa Yohanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
28 nErirmalkEH putraH, malkiH adyaH putraH, addI kOSamaH putraH, kOSam ilmOdadaH putraH, ilmOdad EraH putraH|
mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
29 Er yOzEH putraH, yOziH ilIyESaraH putraH, ilIyESar yOrImaH putraH, yOrIm mattataH putraH, mattata lEvEH putraH|
mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Mathati, mwana wa Lawi,
30 lEviH zimiyOnaH putraH, zimiyOn yihUdAH putraH, yihUdA yUSuphaH putraH, yUSuph yOnanaH putraH, yAnan ilIyAkImaH putraH|
mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yosefu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliakimu,
31 iliyAkImH milEyAH putraH, milEyA mainanaH putraH, mainan mattattasya putraH, mattattO nAthanaH putraH, nAthan dAyUdaH putraH|
mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
32 dAyUd yizayaH putraH, yizaya ObEdaH putra, ObEd bOyasaH putraH, bOyas salmOnaH putraH, salmOn nahazOnaH putraH|
mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
33 nahazOn ammInAdabaH putraH, ammInAdab arAmaH putraH, arAm hiSrONaH putraH, hiSrON pErasaH putraH, pEras yihUdAH putraH|
mwana wa Aminadabu, mwana wa Admini, mwana wa Arni, mwana wa Hesroni, mwana wa Feresi, mwana wa Yuda,
34 yihUdA yAkUbaH putraH, yAkUb ishAkaH putraH, ishAk ibrAhImaH putraH, ibrAhIm tErahaH putraH, tErah nAhOraH putraH|
mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Abrahamu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
35 nAhOr sirugaH putraH, sirug riyvaH putraH, riyUH pElagaH putraH, pElag EvaraH putraH, Evar zElahaH putraH|
mwana wa Serugi, mwana wa Reu, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
36 zElah kainanaH putraH, kainan arphakSadaH putraH, arphakSad zAmaH putraH, zAm nOhaH putraH, nOhO lEmakaH putraH|
mwana wa Kainani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Noa, mwana wa Lameki,
37 lEmak mithUzElahaH putraH, mithUzElah hanOkaH putraH, hanOk yEradaH putraH, yErad mahalalElaH putraH, mahalalEl kainanaH putraH|
mwana wa Mathusala, mwana wa Henoki, mwana wa Yaredi, mwana wa Mahalaleli, mwana wa Kenani,
38 kainan inOzaH putraH, inOz zEtaH putraH, zEt AdamaH putra, Adam Izvarasya putraH|
mwana wa Enosi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, aliyekuwa wa Mungu.

< lUkaH 3 >