< lUkaH 3 >

1 anantaraM tibiriyakaisarasya rAjatvasya panjcadazE vatsarE sati yadA pantIyapIlAtO yihUdAdEzAdhipati rhErOd tu gAlIlpradEzasya rAjA philipanAmA tasya bhrAtA tu yitUriyAyAstrAkhOnItiyApradEzasya ca rAjAsIt luSAnIyanAmA avilInIdEzasya rAjAsIt
Sasa, katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberia, wakati Pontio Pilato alikuwa gavana wa Uyahudi, Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo ndugu yake alikuwa mkuu wa mkoa wa Iturea na Trakoniti, na Lisania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
2 hAnan kiyaphAzcEmau pradhAnayAjAkAvAstAM tadAnIM sikhariyasya putrAya yOhanE madhyEprAntaram Izvarasya vAkyE prakAzitE sati
na wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa, Neno la Mungu lilimjia Yohana mwana wa Zakaria, jangwani.
3 sa yarddana ubhayataTapradEzAn samEtya pApamOcanArthaM manaHparAvarttanasya cihnarUpaM yanmajjanaM tadIyAH kathAH sarvvatra pracArayitumArEbhE|
Alisafiri katika mkoa wote kuzunguka Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi
4 yizayiyabhaviSyadvaktRgranthE yAdRzI lipirAstE yathA, paramEzasya panthAnaM pariSkuruta sarvvataH| tasya rAjapathanjcaiva samAnaM kurutAdhunA|
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha maneno ya Isaya nabii, “sauti ya mtu aliaye nyikani, “Itengenezeni tayari njia ya Bwana, yatengenezeni mapito yake yaliyoonyoka.
5 kAriSyantE samucchrAyAH sakalA nimnabhUmayaH| kAriSyantE natAH sarvvE parvvatAzcOpaparvvatAH| kAriSyantE ca yA vakrAstAH sarvvAH saralA bhuvaH| kAriSyantE samAnAstA yA uccanIcabhUmayaH|
Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa, barabara zilizopinda zitanyoshwa, na njia zilizoparaza zitalainishwa.
6 IzvarENa kRtaM trANaM drakSyanti sarvvamAnavAH| ityEtat prAntarE vAkyaM vadataH kasyacid ravaH||
Watu wote watauona wokovu wa Mungu.”
7 yE yE lOkA majjanArthaM bahirAyayustAn sOvadat rE rE sarpavaMzA AgAminaH kOpAt palAyituM yuSmAn kazcEtayAmAsa?
Hivyo, Yohana akawaambia makutano makubwa ya watu waliomjia wapate kubatizwa na yeye, “Ninyi uzao wa nyoka wenye sumu, nani aliwaonya kuikimbia gadhabu inayokuja?
8 tasmAd ibrAhIm asmAkaM pitA kathAmIdRzIM manObhi rna kathayitvA yUyaM manaHparivarttanayOgyaM phalaM phalata; yuSmAnahaM yathArthaM vadAmi pASANEbhya EtEbhya Izvara ibrAhImaH santAnOtpAdanE samarthaH|
Zaeni matunda yanayoedana na toba, na msianze kusema ndani yenu, “Tunaye Ibarahimu ambaye ni baba yetu; kwa sababu nawaambia ya kwamba, Mungu anaweza kumwinulia Ibrahimu watoto hata kutokana na mawe haya.
9 aparanjca tarumUlE'dhunApi parazuH saMlagnOsti yastaruruttamaM phalaM na phalati sa chidyatE'gnau nikSipyatE ca|
Tayari shoka limeshawekwa kwenye mzizi wa miti. Hivyo, kila mti usiozaa matunda mema, hukatwa na kutupwa motoni.
10 tadAnIM lOkAstaM papracchustarhi kiM karttavyamasmAbhiH?
Kisha watu katika makutano walimuuliza wakisema, “Sasa tunatakiwa tufanyeje?”
11 tataH sOvAdIt yasya dvE vasanE vidyEtE sa vastrahInAyaikaM vitaratu kiMnjca yasya khAdyadravyaM vidyatE sOpi tathaiva karOtu|
Alijibu na kuwaambia, “kama mtu ana kanzu mbili anatakiwa atoe kanzu moja kwa mwingine ambaye hana kabisa, na ambaye ana chakula na afanye vivyo hivyo.”
12 tataH paraM karasanjcAyinO majjanArtham Agatya papracchuH hE gurO kiM karttavyamasmAbhiH?
Kisha baadhi ya watoza ushuru walikuja pia kubatizwa, na wakamwambia, “Mwalimu, tunatakiwa kufanya nini?
13 tataH sOkathayat nirUpitAdadhikaM na gRhlita|
Akawaambia, “Msikusanye fedha zaidi kuliko mnachotakiwa kukusanya.”
14 anantaraM sEnAgaNa Etya papraccha kimasmAbhi rvA karttavyam? tataH sObhidadhE kasya kAmapi hAniM mA kArSTa tathA mRSApavAdaM mA kuruta nijavEtanEna ca santuSya tiSThata|
Baadhi ya maaskari pia wakamuuliza wakisema, “Na sisi je? Tunatakiwa tufanye nini?” Akawambia, “Msichukue fedha kwa mtu yeyote kwa nguvu, na msimtuhumu mtu yeyote kwa uongo. Ridhikeni na mishahara yenu.”
15 aparanjca lOkA apEkSayA sthitvA sarvvEpIti manObhi rvitarkayAnjcakruH, yOhanayam abhiSiktastrAtA na vEti?
Sasa, kwa kuwa watu walikuwa na shauku ya kumngojea Kristo atakaye kuja, kila mmoja alikuwa anawaza moyoni mwake kuhusu Yohana kama yeye ndiye Kristo.
16 tadA yOhan sarvvAn vyAjahAra, jalE'haM yuSmAn majjayAmi satyaM kintu yasya pAdukAbandhanaM mOcayitumapi na yOgyOsmi tAdRza EkO mattO gurutaraH pumAn Eti, sa yuSmAn vahnirUpE pavitra Atmani majjayiSyati|
Yohana akajibu kwa kuwaambia wote, “Mimi nawabatiza ninyi kwa maji, lakini kuna mmoja ajaye ambaye ana nguvu kuliko mimi, na sisitahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Atawabatiza ninyi kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17 aparanjca tasya hastE zUrpa AstE sa svazasyAni zuddharUpaM prasphOTya gOdhUmAn sarvvAn bhANPAgArE saMgrahISyati kintu bUSANi sarvvANyanirvvANavahninA dAhayiSyati|
Pepeto lake liko mkononi mwake ili kusafisha vizuri uwanda wake wa kupepetea ngano na kuikusanya ngano ghalani mwake. Lakini, atayateketeza makapi kwa moto ambao hauwezi kuzimika.
18 yOhan upadEzEnEtthaM nAnAkathA lOkAnAM samakSaM pracArayAmAsa|
Kwa maonyo mengine mengi pia, alihubiri habari njema kwa watu.
19 aparanjca hErOd rAjA philipnAmnaH sahOdarasya bhAryyAM hErOdiyAmadhi tathAnyAni yAni yAni kukarmmANi kRtavAn tadadhi ca
Yohana alimkemea pia Herode mkuu wa mkoa kwa kumuoa Herodia, mke wa ndugu yake na kwa maovu mengine mengi ambayo Herode alikuwa ameyatenda.
20 yOhanA tiraskRtO bhUtvA kArAgArE tasya bandhanAd aparamapi kukarmma cakAra|
Lakini baadaye Herode alifanya uovu mwingine mbaya sana. Alimfunga Yohana gerezani.
21 itaH pUrvvaM yasmin samayE sarvvE yOhanA majjitAstadAnIM yIzurapyAgatya majjitaH|
Kisha ilitokea kwamba, wakati watu wote walipokuwa wakibatizwa na Yohana, naye Yesu alibatizwa pia. Wakati alipokuwa akiomba, mbingu zikafunguka.
22 tadanantaraM tEna prArthitE mEghadvAraM muktaM tasmAcca pavitra AtmA mUrttimAn bhUtvA kapOtavat taduparyyavarurOha; tadA tvaM mama priyaH putrastvayi mama paramaH santOSa ityAkAzavANI babhUva|
Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili kama njiwa, wakati huo huo sauti ikaja kutoka mbinguni ikisema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa sana na wewe.”
23 tadAnIM yIzuH prAyENa triMzadvarSavayaska AsIt| laukikajnjAnE tu sa yUSaphaH putraH,
Sasa Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa na umri upatao miaka thelathini. Alikuwa ni mwana (kama ilivyotadhaniwa) wa Yusufu, mwana wa Eli,
24 yUSaph ElEH putraH, ElirmattataH putraH, mattat lEvEH putraH, lEvi rmalkEH putraH, malkiryAnnasya putraH; yAnnO yUSaphaH putraH|
mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yana, mwana wa Yusufu,
25 yUSaph mattathiyasya putraH, mattathiya AmOsaH putraH, AmOs nahUmaH putraH, nahUm iSlEH putraH iSlirnagEH putraH|
mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Esli, mwana wa Nagai,
26 nagirmATaH putraH, mAT mattathiyasya putraH, mattathiyaH zimiyEH putraH, zimiyiryUSaphaH putraH, yUSaph yihUdAH putraH|
mwana wa Maati, mwana wa Matathia, mwana wa Semeini, mwana wa Yusufu, mwana wa Yuda,
27 yihUdA yOhAnAH putraH, yOhAnA rISAH putraH, rISAH sirubbAbilaH putraH, sirubbAbil zaltIyElaH putraH, zaltIyEl nErEH putraH|
mwana wa Yoanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
28 nErirmalkEH putraH, malkiH adyaH putraH, addI kOSamaH putraH, kOSam ilmOdadaH putraH, ilmOdad EraH putraH|
mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
29 Er yOzEH putraH, yOziH ilIyESaraH putraH, ilIyESar yOrImaH putraH, yOrIm mattataH putraH, mattata lEvEH putraH|
mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Matathi, mwana wa Lawi,
30 lEviH zimiyOnaH putraH, zimiyOn yihUdAH putraH, yihUdA yUSuphaH putraH, yUSuph yOnanaH putraH, yAnan ilIyAkImaH putraH|
mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yusufu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliyakimu,
31 iliyAkImH milEyAH putraH, milEyA mainanaH putraH, mainan mattattasya putraH, mattattO nAthanaH putraH, nAthan dAyUdaH putraH|
mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
32 dAyUd yizayaH putraH, yizaya ObEdaH putra, ObEd bOyasaH putraH, bOyas salmOnaH putraH, salmOn nahazOnaH putraH|
mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
33 nahazOn ammInAdabaH putraH, ammInAdab arAmaH putraH, arAm hiSrONaH putraH, hiSrON pErasaH putraH, pEras yihUdAH putraH|
mwana wa Abinadabu, mwana wa Aramu, mwana wa Hesroni, mwana wa Peresi, mwana wa Yuda,
34 yihUdA yAkUbaH putraH, yAkUb ishAkaH putraH, ishAk ibrAhImaH putraH, ibrAhIm tErahaH putraH, tErah nAhOraH putraH|
mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Ibrahimu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
35 nAhOr sirugaH putraH, sirug riyvaH putraH, riyUH pElagaH putraH, pElag EvaraH putraH, Evar zElahaH putraH|
mwana wa Seruig, mwana wa Ragau, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
36 zElah kainanaH putraH, kainan arphakSadaH putraH, arphakSad zAmaH putraH, zAm nOhaH putraH, nOhO lEmakaH putraH|
mwana wa Kenani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Nuhu, mwana wa Lameki,
37 lEmak mithUzElahaH putraH, mithUzElah hanOkaH putraH, hanOk yEradaH putraH, yErad mahalalElaH putraH, mahalalEl kainanaH putraH|
mwana wa Methusela, mwana wa Henoko, mwana wa Yaredi, mwana Mahalalei, mwana wa Kenani,
38 kainan inOzaH putraH, inOz zEtaH putraH, zEt AdamaH putra, Adam Izvarasya putraH|
mwana wa Enoshi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, mwana wa Mungu.

< lUkaH 3 >