< Luke 10 >

1 Masuole chu, Pumapa'n, midang sômsarileinik a thanga, abop abopin an sena rang khopuitina le muntina, ama motona a tîra.
Baada ya hayo, Bwana aliwachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawiliwawili, wamtangulie katika kila kijiji na mahali ambapo yeye mwenyewe alitaka kwenda.
2 An kôma, “Bu ât rang atama, ania a mintûp ranga sin rang mi an tôm, Masikin, a bu mintûp ranga sintho rang mi tîr rangin bu pumapa kôm ngên roi.”
Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache. Kwa hivyo, mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake.
3 “Se roi! Melang lâia belrite om anga han nangni ki tîr ani.
Sasa nendeni; fahamuni kwamba ninawatuma ninyi kama kondoo wanaokwenda kati ya mbwa mwitu.
4 Sumkok mo, cholite mo, kekok mo, chôi no roi; lampuia khom tute chibai no roi.
Msichukue mfuko wa fedha, mkoba, wala viatu; msimsalimu mtu yeyote njiani.
5 In nin lûtna kipa, ‘Hi ina hin rathanngamna om rese’ ti bak roi.
Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza wasalimuni hivi: Amani iwe katika nyumba hii!
6 Rathanngamna midit mi an oma anîn chu nin rathanngamna chibai hah an chunga om a tih; an om nôn chu nin chibai hah lâk kîr nôk roi.
Kama akiwako mwenye kupenda amani, amani yenu itakaa naye, la sivyo, itawarudieni.
7 Nin tungna ina han omtit ungla, nangni an pêk murdi sâk ungla, nêk roi, sinthopu chu lo pêk rang ani sikin. In tin lôrdul no roi.
Kaeni katika nyumba hiyo mkila na kunywa wanavyowapeni, maana mfanyakazi anastahili mshahara wake. Msiende mara nyumba hii mara nyumba ile.
8 Khopui nin lûta nangni an modôma anîn chu, nangni an pêk kai chu sâk roi.
Kama mkifika mji fulani na watu wakiwakaribisha, kuleni wanavyowapeni.
9 Ma khuoa damloi ngei mindam ungla, an kôma, ‘Pathien Rêngram nin kôma ajuong nâi zoi’ tipe ngei roi.
Ponyeni wagonjwa walioko huko, waambieni watu: Ufalme wa Mungu umekaribia kwenu.
10 Khopui nin lûtna nâm nangni an modôm nôn chu, lampuia jôkpai ungla,
Lakini mkiingia katika mji wowote, wasipowakaribisheni, tokeni; nanyi mpitapo katika barabara zao semeni:
11 nin khopuia pildi, kin kea kop tena khom nin chunga kin khôngthâk nôk vang ania, ‘Pathien Rêngram chu nin kôm ajuong nâi zoi!’ tipe ngei roi, a tia.
Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu tunawakung'utieni. Lakini, jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
12 Nangni ki ril, Pathien Roijêk Nikhuo tika chu, ma khopuingei tuong rang nêkin chu, Sodom chu ajâi om uol atih!”
Hakika nawaambieni, siku ile mji huo utapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Sodoma.
13 “Korazin, na chungroi arik bah na! Bethsaida, khom na chung roi arik bah na! Nangnia sininkhêl itho ngei hah Tyre le Sydon khuoa tho nisenla chu, thoila puon insilin, pildi inpolin an sietnangei insîr an tih.
“Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Maana, kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika kule Tiro na Sidoni, watu wake wangalikwishavaa mavazi ya gunia kitambo, na kukaa katika majivu kuonyesha kwamba wametubu.
14 Roijêk Nîn chu nin tuong rang nêkin Tyre le Sydon chu ajâi om uol an tih.
Hata hivyo, Siku ya Hukumu ninyi mtapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Tiro na Sidoni.
15 Nangma Capernaum khom, nethenin invân idênin nên pâk rang mini? Dûkmuna kêng vôrpai na ni rang.” (Hadēs g86)
Na wewe Kafarnaumu, unataka kujikweza mpaka mbinguni? La; utaporomoshwa mpaka Kuzimu.” (Hadēs g86)
16 Jisua'n a ruoisingei kôma, “Tutu nin chong rangâi chu ko chong rangâi ani, tutu nangni heng chu ni heng ani, tutu ni heng chu ni tîrpu heng ani,” a tia.
Halafu akasema, “Anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; na anayekataa kuwapokea ninyi, anakataa kunipokea mimi. Yeyote anayekataa kunipokea, anakataa kumpokea yule aliyenituma.”
17 Hanchu, sômsarileinik ngei hah râisân takin an hong kîra, “Pumapa, ni rimingin ramkhoringei tena kin chong an jôm” an tia.
Baadaye, wale sabini na wawili walirudi wamejaa furaha, wakisema, “Bwana, hata pepo wametutii tulipolitaja jina lako.”
18 Jisua'n a thuon ngeia, “Soitan, invân renga kôlinlek anga juong tâk ku mu,” a tia.
Yeye akawaambia, “Nilimwona Shetani jinsi alivyokuwa anaporomoka kama umeme kutoka mbinguni.
19 An kôma, “Rangâi roi, murûlngei le âinuvet chunga lôn theina le râlngei roineina chunga rachamneina nangni ke pêk, itên nangni minna thei noni ngei,” a tia.
Naam, nimewapeni uwezo wa kukanyaga nyoka na ng'e, na uwezo juu ya nguvu zote za yule adui; hakuna chochote kitakachowadhuru.
20 “Ania ramkhoringeiin nin chong an jôm sikin nan râiminsân no roia, Invâna nin riming mizieka a om sikin nan râiminsân roi” a tipe ngeia.
Hata hivyo, msifurahi kwa sababu pepo wamewatii, bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.”
21 Ma zora han Jisua Ratha Inthiengin a sipa, “O Pa, invân le pilchung Pumapa, mivâr, mi theithiem ngei kôma ni ip, mi inmôlngei kôma nu phuong sikin nang ki minpâk. Ani, O Pa, maha nu lungdo le na nuomlam tak ani,” a tia.
Saa ileile, Yesu akafurahi kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akasema, “Nakushukuru ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa kuwa umewaficha wenye hekima na elimu mambo haya, ukawafumbulia wadogo. Naam, Baba, ndivyo ilivyokupendeza.”
22 Ka Pa'n neinun murdi ni pêk zoi. Tutên, Pa ti loiin chu Nâipasal riet mak. Tutên Nâipasal ti loiin chu Pa khom riet mak, Nâipasalin ânphuongna ngei tiloiin chu.
Kisha akasema, “Baba yangu ameweka yote mikononi mwangu. Hakuna amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala amjuaye Baba ni nani ila Mwana, na yeyote yule ambaye Mwana anataka kumfunulia hayo.”
23 Hanchu, Jisua ruoisingei tieng ân heia, inrûkten, “Hi ngei nin mu hih idôra mi satvur mo nin ni!
Halafu akawaelekea wafuasi wake akawaambia, “Heri wanaoona yale mnayoyaona ninyi!
24 Dêipungei, rêngngei tamtakin nin mu ngei hih mu rang an nuoma chuh mu mak ngei, nin iriet ngei a riet an nuoma chuh riet mak ngei,” a tipe ngeia.
Hakika, manabii na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona ninyi wasiyaone, na kusikia yale mnayoyasikia wasiyasikie.”
25 Balam minchupu inkhat Jisua minvak rangin a honga, a kôma, “Minchupu, Kumtuong ringna ka manna rangin imo ki sin rang?” a tia. (aiōnios g166)
Baadaye mwalimu mmoja wa Sheria alisimama akamwuliza akitaka kumtega, “Mwalimu, nifanye nini ili nipate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
26 Jisua'n a thuona, “Lekhabu'n imo ati? Imo no pore ngâi?” a tia.
Yesu akamwuliza, “Imeandikwa nini katika Sheria? Unaelewaje?”
27 Hanchu ama'n, “Pumapa na Pathien chu, nu mulung murdi'n, ni ringna murdi'n, na râtna murdi'n ni mindonna murdi'n lungkham roh. Nangma lung nên kham anghan nu bungmingei lungkham roh ati,” tiin a thuona.
Akamjibu, “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote. Na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”
28 Jisua'n a kôma, “Ni ti mindik, ha angtak han thô inla, ring ni tih,” a tia.
Yesu akawaambia, “Vema! Fanya hivyo, nawe utaishi.”
29 Hannisenla, Balam minchupu hah theiintum nuomin, Jisua kôma, “Tumo ku bungngei?” a tia.
Lakini yeye akitaka kujihakikishia kuwa mwema akamwuliza Yesu, “Na jirani yangu ni nani?”
30 Hanchu, Jisua'n a thuona, “Hanchu voikhat, mi inkhat Jerusalem renga Jericho'a a sea, inru ngei a tonga, an jêmpola, an tôk bita, a thi vângin an mâk raka.
Yesu akamjibu, “Mtu mmoja alikuwa anashuka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko. Alipokuwa njiani, alivamiwa na majambazi, wakamnyang'anya mali yake na kumpiga, wakamwacha amelala pale nusu mfu.
31 Hanchu ha lampuia han ochai inkhat a juong sea, ha mi hah a mûn chu lam dang tieng a piela.
Kumbe, kuhani mmoja akawa anapita barabara ileile, akamwona, akapita kando.
32 Ma ang nanâk han, Levi mi a juonga, a ena, hanchu lamsîr tieng a piela.
Hali kadhalika na Mlawi mmoja, alipofika mahali akamwona, akapita kando.
33 Hanchu, Samari mi inkhat han ha lampuia lônin a honga, a mûn chu lungkham a mua.
Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa anasafiri, alifika pale yule mtu alipokuwa, naye alipomwona, alimwonea huruma.
34 A kôm ava pana, a sâbengei sariek le uain a buoka, a thom pea, a sakuording chunga a minchuonga, khuol tung ina a tuonga, a donsûi zoia.
Akamwendea, akamtibu majeraha yake kwa kumtia mafuta na divai; na kuyafunga halafu akampandisha juu ya punda wake akampeleka katika nyumba moja ya wageni akamuuguza.
35 A nangtûka chu, sum dârnik a kelsuoa, khuol tung in enkolpu a pêka, ‘Lei donsûi inla,’ a chunga na thâm kai chu ko hong kîr nôk tika nang thuon ki tih” a tia.
Kesho yake akatoa fedha dinari mbili akampa yule mwenye nyumba, akamwambia, Muuguze mtu huyu; na chochote utakachotumia zaidi, nitakulipa nitakaporudi.”
36 Jisua'n, a kôma, “Inthum ngei lâia han atu tak ha mo inru ngei tongpu bungmi ani ranga ni iem?” a tia.
Kisha Yesu akauliza, “Kati ya hao watatu, ni yupi aliyeonyesha kuwa jirani yake yule aliyevamiwa na majambazi?”
37 Balam minchupu han a kôma, “inriengmupu tak hah” tiin a thuona. Jisua'n, “Sênla, nang khom ha ang tak han tho roh,” a tipea.
Yule mwalimu wa Sheria akamjibu, “Ni yule aliyemwonea huruma.” Yesu akamwambia, “Nenda ukafanye vivyo hivyo.”
38 Hanchu, Jisua le a ruoisingei an khuol se nân, khuo inkhata an lûta, nupang a riming Martha a ina a modôm ngeia.
Walipokuwa safarini, waliingia katika kijiji kimoja na mwanamke mmoja, aitwaye Martha, alimkaribisha nyumbani kwake.
39 A juorpuinu riming chu Mary ani, ama han Pumapa ke bula insungin, a chongril a rangâia.
Martha alikuwa na dada yake aitwaye Maria; huyu aliketi karibu na Yesu akisikiliza mafundisho yake.
40 Ania, Martha chu sinthôn ânpol oka, a honga, “Pumapa, kênzirpui nûn ke theivaia sintho ranga ni mâkrak hih ni mindon pe mak che mo hi?” ni hong san rangin tipe roh! a tia.
Lakini Martha alikuwa anashughulika na mambo mengi. Basi, akamwendea Yesu, akamwambia, “Bwana, hivi hujali kwamba dada yangu ameniacha nishughulike peke yangu? Mwambie basi, anisaidie.”
41 Pumapa'n amanu kôma, “Martha, Martha, neinun tamtak ni mindon sika nênjêl kêng.
Lakini Bwana akamjibu, “Martha, Martha, unahangaika na kusumbuka kwa mambo mengi.
42 Inkhat vai kêng ai nâng, Mary hin neinun dik a thanga, a kôm renga isut nôk rang ni khâi mak,” a tipea.
Kitu kimoja tu ni muhimu. Maria amechagua kitu bora zaidi ambacho hakuna mtu atakayemnyag'anya.”

< Luke 10 >