< Luka 3 >

1 Umwaha, ugwa kumi na tano owalongozye hwakwe Kaisari Tiberia, Pantio Pilato nali liwali owayahudi, na Herode omwene owa Galilaya, no Filipo oholo wakwe omwene uwa Iturea nensi eya Trakoniti, na Lisania no mwene owa Abilene,
Sasa, katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberia, wakati Pontio Pilato alikuwa gavana wa Uyahudi, Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo ndugu yake alikuwa mkuu wa mkoa wa Iturea na Trakoniti, na Lisania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
2 Wakati owa kohani ogosi owa anasi no Kayafa, izu elya NGOLOBHE lya fishiye oYohana omwana owa Zakaria, mwipoli.
na wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa, Neno la Mungu lilimjia Yohana mwana wa Zakaria, jangwani.
3 Afishele mnsi yonti yelikaribu ne Yordani, alombeleye owoziwa owa lete usajilwa olwa hwefwe embibhi.
Alisafiri katika mkoa wote kuzunguka Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi
4 Neshe shahwasimbilwe chuo eshe mazu aga kuwe Isaya, “Izu ya mntu wali mwipoli, “Lilenganyi idala elya GOSI, gagalosyaji omwashile hwakwe.
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha maneno ya Isaya nabii, “sauti ya mtu aliaye nyikani, “Itengenezeni tayari njia ya Bwana, yatengenezeni mapito yake yaliyoonyoka.
5 Entebha yonti yayimema nigamba nagamba hayisiwa, papatejile payibha pagoloshe papakwanyushe paile nganiha.
Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa, barabara zilizopinda zitanyoshwa, na njia zilizoparaza zitalainishwa.
6 Bhonti abhebele bhayihulo owaule owa NGOLOBHE.”
Watu wote watauona wokovu wa Mungu.”
7 Basi, abhabholele amabongano bhala bhabhaliye ili abhoziwe amwe mpapwo wenzoha wenu yabhasundile amwe ayinjile enkuni yehayenza?
Hivyo, Yohana akawaambia makutano makubwa ya watu waliomjia wapate kubatizwa na yeye, “Ninyi uzao wa nyoka wenye sumu, nani aliwaonya kuikimbia gadhabu inayokuja?
8 Basi fumyaje amadondo gagahwanziwa ulusajilo, wala mgajeahwanza ayanje mmoyo genyu, “Tilinawo udada uIbrahimu eshi embabhola yaje amawe ega, ONGOLOBHE abhajiye ahwubhosrzye uIbrahimu abhana.
Zaeni matunda yanayoedana na toba, na msianze kusema ndani yenu, “Tunaye Ibarahimu ambaye ni baba yetu; kwa sababu nawaambia ya kwamba, Mungu anaweza kumwinulia Ibrahimu watoto hata kutokana na mawe haya.
9 Neshi etwanga tayari ebhehwelwe pamashinshi age makwi. Basi, kila likwi lya sagalipapa amadondo aminza, lidumlwa nalitaje mmwoto.
Tayari shoka limeshawekwa kwenye mzizi wa miti. Hivyo, kila mti usiozaa matunda mema, hukatwa na kutupwa motoni.
10 Amabungano gabhozya, “Tikhozye wole eshi?”
Kisha watu katika makutano walimuuliza wakisema, “Sasa tunatakiwa tufanyeje?”
11 Wabhajibu wabhabhozya, “Yali na magolola gabhele na apele yasaga aunigolola yali nevyalye wape abhombe eshoshesho.”
Alijibu na kuwaambia, “kama mtu ana kanzu mbili anatakiwa atoe kanzu moja kwa mwingine ambaye hana kabisa, na ambaye ana chakula na afanye vivyo hivyo.”
12 Bhabhasonjezya bhape bhenza ahwoziwe, bhabhozya,”Manyiziji, tubhombe yenu ate?
Kisha baadhi ya watoza ushuru walikuja pia kubatizwa, na wakamwambia, “Mwalimu, tunatakiwa kufanya nini?
13 Wabhabhola, “Mgaje sonjezye ahantu zaidi ya hata hahapangwilwe.
Akawaambia, “Msikusanye fedha zaidi kuliko mnachotakiwa kukusanya.”
14 Asikali bhape bhabhozya bhayanga, “ate nate tibhombe wele? Wabhabhole msafwele omntu wala msashitake ilenka antele myanje no mshahara gwenyu.”
Baadhi ya maaskari pia wakamuuliza wakisema, “Na sisi je? Tunatakiwa tufanye nini?” Akawambia, “Msichukue fedha kwa mtu yeyote kwa nguvu, na msimtuhumu mtu yeyote kwa uongo. Ridhikeni na mishahara yenu.”
15 Basi, abhantu nabhali bhabhagola gaganzafumile, wonti bhasega sebhaga mmoyo gabho enongwa ezya Yohana nkashe umwene Kristi.
Sasa, kwa kuwa watu walikuwa na shauku ya kumngojea Kristo atakaye kuja, kila mmoja alikuwa anawaza moyoni mwake kuhusu Yohana kama yeye ndiye Kristo.
16 UYohana wagalula wabhabhozya bhonti lyoli ane embozya namenze lelo ahwenza ohwemaha ashile ane sembwezizye ayengezye olwabho olye vilato vyakwe. omwahale ayibhoziwa hupepo ozelu no mwoto.
Yohana akajibu kwa kuwaambia wote, “Mimi nawabatiza ninyi kwa maji, lakini kuna mmoja ajaye ambaye ana nguvu kuliko mimi, na sisitahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Atawabatiza ninyi kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17 Afwanaje ubheto lwakwa lulimakho no wape ayozya tee mhati yakwe na bhonganye engano yakwe. Mshanga, antele amapetelo aigapemba mmwoto gwa sagaguzima.
Pepeto lake liko mkononi mwake ili kusafisha vizuri uwanda wake wa kupepetea ngano na kuikusanya ngano ghalani mwake. Lakini, atayateketeza makapi kwa moto ambao hauwezi kuzimika.
18 Basi hurusundo hugamwabho aminji, abhalombeleye abhantu.
Kwa maonyo mengine mengi pia, alihubiri habari njema kwa watu.
19 Lelo omwene oHerode akhalipiwe nomwe kwajili ya Herode, ushe wa holo wakwe, namabhibhi gonti gabhombile o Herode.
Yohana alimkemea pia Herode mkuu wa mkoa kwa kumuoa Herodia, mke wa ndugu yake na kwa maovu mengine mengi ambayo Herode alikuwa ameyatenda.
20 Ahonjezye eli neli afunjile oyohani mwijela.
Lakini baadaye Herode alifanya uovu mwingine mbaya sana. Alimfunga Yohana gerezani.
21 Bhabhantu wonti bhabhamaushe ahinziwe no Yesu wape ahoziwe wape alabhile emwanya zya higushe.
Kisha ilitokea kwamba, wakati watu wote walipokuwa wakibatizwa na Yohana, naye Yesu alibatizwa pia. Wakati alipokuwa akiomba, mbingu zikafunguka.
22 Upepo uzelu ahishile pamwanya yakwe hufwano ongwebelebele, neshe enjebha izu lya fumile amwanya, “Awe wemwana wane wegene. Ensogwezewe nawe.”
Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili kama njiwa, wakati huo huo sauti ikaja kutoka mbinguni ikisema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa sana na wewe.”
23 No Yesu yoyo nahandile amanyizye, ali apate umri wakwe neshe amaha salathini. ategemelwa ajemwana wa Yusufu, wa Eli,
Sasa Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa na umri upatao miaka thelathini. Alikuwa ni mwana (kama ilivyotadhaniwa) wa Yusufu, mwana wa Eli,
24 Wo Mathati, walawi, wa MeIki, wayana wa Yusufu,
mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yana, mwana wa Yusufu,
25 Wa Matathia, wa Amosi, wa Nahumu, wa Esli, wa Nagai,
mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Esli, mwana wa Nagai,
26 Wa Maati, wa Matathia, wa Semeini, wa Yusufu, wa Yuda,
mwana wa Maati, mwana wa Matathia, mwana wa Semeini, mwana wa Yusufu, mwana wa Yuda,
27 Wa Yohana, wa Rese, wa Zerubabeli, wa SheaItieli, wa Neri,
mwana wa Yoanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
28 MeIki, wa Adi, wa Kosamu, wa Elmadamu, wa Eri,
mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
29 Wa Yoshua, wa Eliezeri, wa Yorimu, wa Matathi, wa Lawi,
mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Matathi, mwana wa Lawi,
30 Wa Simioni, wa Yuda, wa Yusufu, wa Yonamu, wa Eliyakimu,
mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yusufu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliyakimu,
31 Wa Melea, wa Mena, wa Matatha, wa nathani, wa Daudi,
mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
32 Wa Yese, wa Obedi, wa Boazi wa Salmoni, wa Nashoni,
mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
33 Wa Abinadabu, wa Aramu, wa Hesroni, wa Peresi, wa Yuda,
mwana wa Abinadabu, mwana wa Aramu, mwana wa Hesroni, mwana wa Peresi, mwana wa Yuda,
34 Wa Yakobo, wa Isaka, wa Ibrahimu, wa Tera, wa Nahori,
mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Ibrahimu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
35 Wa Seruig, wa Ragau, wa Pelegi, wa Eberi, wa Sala,
mwana wa Seruig, mwana wa Ragau, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
36 Wa Kenani, wa Arfaksadi, wa Shemu, wa Nuhu, wa Lameki,
mwana wa Kenani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Nuhu, mwana wa Lameki,
37 Wa Methusela, wa Henoko, wa Yaredi, wa Mahalalei, wa Kenani,
mwana wa Methusela, mwana wa Henoko, mwana wa Yaredi, mwana Mahalalei, mwana wa Kenani,
38 Wa Enoshi, wa Sethi, wa Adamu, wa NGOLOBHE.
mwana wa Enoshi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, mwana wa Mungu.

< Luka 3 >