< Псалтирь 72 >

1 О Соломоне. Боже! даруй царю Твой суд и сыну царя Твою правду,
Zaburi ya Solomoni. Ee Mungu, mjalie mfalme aamue kwa haki yako, mwana wa mfalme kwa haki yako.
2 да судит праведно людей Твоих и нищих Твоих на суде;
Atawaamua watu wako kwa haki, watu wako walioonewa kwa haki.
3 да принесут горы мир людям и холмы правду;
Milima italeta mafanikio kwa watu, vilima tunda la haki.
4 да судит нищих народа, да спасет сынов убогого и смирит притеснителя, -
Atawatetea walioonewa miongoni mwa watu na atawaokoa watoto wa wahitaji, ataponda mdhalimu.
5 и будут бояться Тебя, доколе пребудут солнце и луна, в роды родов.
Atadumu kama jua lidumuvyo, kama mwezi, vizazi vyote.
6 Он сойдет, как дождь на скошенный луг, как капли, орошающие землю;
Atakuwa kama mvua inyeshayo juu ya shamba lililofyekwa, kama manyunyu yanyeshayo ardhi.
7 во дни его процветет праведник, и будет обилие мира, доколе не престанет луна;
Katika siku zake wenye haki watastawi; mafanikio yatakuwepo mpaka mwezi utakapokoma.
8 он будет обладать от моря до моря и от реки до концов земли;
Atatawala kutoka bahari hadi bahari na kutoka Mto mpaka miisho ya dunia.
9 падут пред ним жители пустынь, и враги его будут лизать прах;
Makabila ya jangwani watamsujudia, na adui zake wataramba mavumbi.
10 цари Фарсиса и островов поднесут ему дань; цари Аравии и Савы принесут дары;
Wafalme wa Tarshishi na wa pwani za mbali watamletea kodi; wafalme wa Sheba na Seba watampa zawadi.
11 и поклонятся ему все цари; все народы будут служить ему;
Wafalme wote watamsujudia na mataifa yote yatamtumikia.
12 ибо он избавит нищего, вопиющего и угнетенного, у которого нет помощника.
Kwa maana atamwokoa mhitaji anayemlilia, aliyeonewa asiye na wa kumsaidia.
13 Будет милосерд к нищему и убогому, и души убогих спасет;
Atawahurumia wanyonge na wahitaji na kuwaokoa wahitaji kutoka mauti.
14 от коварства и насилия избавит души их, и драгоценна будет кровь их пред очами его;
Atawaokoa kutoka uonevu na ukatili, kwani damu yao ni ya thamani machoni pake.
15 и будет жить, и будут давать ему от золота Аравии, и будут молиться о нем непрестанно, всякий день благословлять его;
Aishi maisha marefu! Na apewe dhahabu ya Sheba. Watu wamwombee daima na kumbariki mchana kutwa.
16 будет обилие хлеба на земле, наверху гор; плоды его будут волноваться, как лес на Ливане, и в городах размножатся люди, как трава на земле;
Nafaka ijae tele katika nchi yote, juu ya vilele vya vilima na istawi. Tunda lake na listawi kama Lebanoni, listawi kama majani ya kondeni.
17 будет имя его вовек; доколе пребывает солнце, будет передаваться имя его; и благословятся в нем племена, все народы ублажат его.
Jina lake na lidumu milele, na lidumu kama jua. Mataifa yote yatabarikiwa kupitia kwake, nao watamwita aliyebarikiwa.
18 Благословен Господь Бог, Бог Израилев, един творящий чудеса,
Bwana Mungu, Mungu wa Israeli, apewe sifa, yeye ambaye peke yake hutenda mambo ya ajabu.
19 и благословенно имя славы Его вовек, и наполнится славою Его вся земля. Аминь и аминь.
Jina lake tukufu lisifiwe milele, ulimwengu wote ujae utukufu wake.
20 Кончились молитвы Давида, сына Иесеева.
Huu ndio mwisho wa maombi ya Daudi mwana wa Yese.

< Псалтирь 72 >