< Псалтирь 60 >

1 Начальнику хора. На музыкальном орудии Шушан-Эдуф. Писание Давида для изучения, когда он воевал с Сириею Месопотамскою и с Сириею Цованскою, и когда Иоав, возвращаясь, поразил двенадцать тысяч Идумеев в долине Соляной. Боже! Ты отринул нас, Ты сокрушил нас, Ты прогневался: обратись к нам.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Shushani Eduthi.” Utenzi wa Daudi wa kufundisha. Wakati alipopigana na Waaramu kutoka Aramu-Naharaimu na Aramu-Soba, naye Yoabu akarudi nyuma na kuwaua Waedomu 12,000 katika Bonde la Chumvi. Ee Mungu, umetukataa na kutokea ghafula juu yetu, umekasirika: sasa turejeshe upya!
2 Ты потряс землю, разбил ее: исцели повреждения ее, ибо она колеблется.
Umetetemesha nchi na kuipasua; uiponye mavunjiko yake, kwa maana inatetemeka.
3 Ты дал испытать народу твоему жестокое, напоил нас вином изумления.
Umewaonyesha watu wako nyakati za kukata tamaa; umetunywesha mvinyo unaotuyumbisha.
4 Даруй боящимся Тебя знамя, чтобы они подняли его ради истины,
Kwa wale wanaokucha wewe, umewainulia bendera, ili iweze kutwekwa dhidi ya upinde.
5 чтобы избавились возлюбленные Твои; спаси десницею Твоею и услышь меня.
Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
6 Бог сказал во святилище Своем: “восторжествую, разделю Сихем и долину Сокхоф размерю:
Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
7 Мой Галаад, Мой Манассия, Ефрем крепость главы Моей, Иуда скипетр Мой,
Gileadi ni yangu na Manase ni yangu; Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
8 Моав умывальная чаша Моя; на Едома простру сапог Мой. Восклицай Мне, земля Филистимская!”
Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
9 Кто введет меня в укрепленный город? Кто доведет меня до Едома?
Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
10 Не Ты ли, Боже, Который отринул нас, и не выходишь, Боже, с войсками нашими?
Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
11 Подай нам помощь в тесноте, ибо защита человеческая суетна.
Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
12 С Богом мы окажем силу, Он низложит врагов наших.
Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.

< Псалтирь 60 >