< Псалтирь 36 >

1 Начальнику хора. Раба Господня Давида. Нечестие беззаконного говорит в сердце моем: нет страха Божия пред глазами его,
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
2 ибо он льстит себе в глазах своих, будто отыскивает беззаконие свое, чтобы возненавидеть его;
Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
3 слова уст его - неправда и лукавство; не хочет он вразумиться, чтобы делать добро;
Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
4 на ложе своем замышляет беззаконие, становится на путь недобрый, не гнушается злом.
Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
5 Господи! милость Твоя до небес, истина Твоя до облаков!
Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
6 Правда Твоя, как горы Божии, и судьбы Твои - бездна великая! Человеков и скотов хранишь Ты, Господи!
Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
7 Как драгоценна милость Твоя, Боже! Сыны человеческие в тени крыл Твоих покойны:
Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
8 насыщаются от тука дома Твоего, и из потока сладостей Твоих Ты напояешь их,
Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
9 ибо у Тебя источник жизни; во свете Твоем мы видим свет.
Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
10 Продли милость Твою к знающим Тебя и правду Твою к правым сердцем,
Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
11 да не наступит на меня нога гордыни, и рука грешника да не изгонит меня:
Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
12 там пали делающие беззаконие, низринуты и не могут встать.
Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!

< Псалтирь 36 >