< Псалтирь 22 >

1 Начальнику хора. При появлении зари. Псалом Давида. Боже мой! Боже мой! для чего Ты оставил меня? Далеки от спасения моего слова вопля моего.
Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali na wokovu wangu na mbali na maneno yangu yenye uchungu?
2 Боже мой! я вопию днем, - и Ты не внемлешь мне, ночью, - и нет мне успокоения.
Mungu wangu, ninalia mchana kutwa, lakini haunijibu, na wakati wa usiku sinyamazi!
3 Но Ты, Святый, живешь среди славословий Израиля.
Bado wewe ni mtakatifu; wewe umekaa kama mfalme pamoja na sifa za Israeli.
4 На Тебя уповали отцы наши; уповали, и Ты избавлял их;
Mababu zetu walikuamini wewe, na wewe uliwaokoa wao.
5 к Тебе взывали они, и были спасаемы; на Тебя уповали, и не оставались в стыде.
Walikulilia wewe nao waka okolewa. Wao walikuamini wewe na hawakuvunjwa moyo.
6 Я же червь, а не человек, поношение у людей и презрение в народе.
Bali mimi ni funza na sio mtu, nisiye faa kwa ubinadamu na hudharauliwa na watu.
7 Все, видящие меня, ругаются надо мною, говорят устами, кивая головою:
Wale wote wanionao hunisuta; hunidhihaki; hunitikisia vichwa vyao.
8 “он уповал на Господа; пусть избавит его, пусть спасет, если он угоден Ему”.
Wao husema, “Yeye anamwamini Yahwe; mwache Yahwe amuokoe. Mwache amuokoe yeye, kwa kuwa yeye anampendeza sana Yeye.”
9 Но Ты извел меня из чрева, вложил в меня упование у грудей матери моей.
Kwa kuwa wewe ulinileta kutoka tumboni; wewe ulinifanya nikuamini wewe wakati nikiwa nanyonya matiti ya mama yangu.
10 На Тебя оставлен я от утробы; от чрева матери моей Ты - Бог мой.
Nimekwisha tupwa kwako wewe tokea tumboni; wewe ni Mungu wangu tangu nikiwa tumboni mwa mama yangu!
11 Не удаляйся от меня, ибо скорбь близка, а помощника нет.
Usiwe mbali na mimi, kwa kuwa shida ikaribu; hayupo hata mmoja wa kusaidia.
12 Множество тельцов обступили меня; тучные Васанские окружили меня,
Maksai wengi wananizunguka mimi; maksai wenye nguvu ya Bashan wananizunguka mimi.
13 раскрыли на меня пасть свою, как лев, алчущий добычи и рыкающий.
Wao wanafungua midomo yao kwangu kama simba aungurumaye akirarua windo lake.
14 Я пролился, как вода; все кости мои рассыпались; сердце мое сделалось, как воск, растаяло посреди внутренности моей.
Ninamwagwa nje kama maji, na mifupa yangu yote imeteguka. Moyo wangu ni kama nta; nao unayeyuka ndani ya sehemu zangu za ndani.
15 Сила моя иссохла, как черепок; язык мой прильнул к гортани моей, и Ты свел меня к персти смертной.
Nguvu zangu zimekaushwa kama kipande cha ufinyanzi; ulimi wangu unanata juu ya mdomo wangu. Wewe umenilaza mimi katika vumbi la mauti.
16 Ибо псы окружили меня, скопище злых обступило меня, пронзили руки мои и ноги мои.
Kwa maana mbwa wamenizunguka; kundi la watu waovu limenizunguka; wamenitoboa mikono yangu na miguu yangu.
17 Можно было бы перечесть все кости мои; а они смотрят и делают из меня зрелище;
Nami ninaweza kuihesabu mifupa yangu. Wao wananitazama na kunishangaa.
18 делят ризы мои между собою и об одежде моей бросают жребий.
Wao wanagawa mavazi yangu kati yao wenyewe, wanapiga kura kwa ajili ya mavazi yangu.
19 Но Ты, Господи, не удаляйся от меня; сила моя! поспеши на помощь мне;
Usiwe mbali, Yahwe; tafadhali harakisha kunisaidia mimi, nguvu yangu!
20 избавь от меча душу мою и от псов одинокую мою;
Uiokoe roho yangu na upanga, maisha yangu mwenyewe na makucha ya mbwa mwitu.
21 спаси меня от пасти льва и от рогов единорогов, услышав, избавь меня.
Uniokoe na mdomo wa simba; uniokoe na mapembe ya ng'ombe wa porini.
22 Буду возвещать имя Твое братьям моим, посреди собрания восхвалять Тебя.
Nami nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kusanyiko la watu nitakusifu wewe.
23 Боящиеся Господа! восхвалите Его. Все семя Иакова! прославь Его. Да благоговеет пред Ним все семя Израиля,
Ninyi mnao mwogopa Yahwe, msifuni yeye! Ninyi nyote kizazi cha Yakobo, muheshimuni yeye! Simameni katika hofu yake, ninyi nyote kizazi cha Israeli!
24 ибо Он не презрел и не пренебрег скорби страждущего, не скрыл от него лица Своего, но услышал его, когда сей воззвал к Нему.
Kwa kuwa haja dharau au kuchukia mateso ya aliye taabishwa; Yahwe hajamficha uso wake yeye; pindi wale walio taabishwa walipo mlilia yeye, yeye alisikia.
25 О Тебе хвала моя в собрании великом; воздам обеты мои пред боящимися Его.
Yahwe, katika kusanyiko la watu wako nitakusifu kwa yale uliyo tenda; nami nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wanao muhofu yeye.
26 Да едят бедные и насыщаются; да восхвалят Господа ищущие Его; да живут сердца ваши во веки!
Walio onewa watakula na kutosheka; wale ambao humtafuta Yahwe watamsifu yeye. Mioyo yenu iishi milele.
27 Вспомнят, и обратятся к Господу все концы земли, и поклонятся пред Тобою все племена язычников,
Watu wote wa duniani watakumbuka na kumrudia Yahwe; familia zote za mataifa watapiga magoti chini mbele yako.
28 ибо Господне есть царство, и Он - Владыка над народами.
Kwa kuwa utawala ni wa Yahwe; yeye ni mtawala wa mataifa.
29 Будут есть и поклоняться все тучные земли; преклонятся пред Ним все нисходящие в персть и не могущие сохранить жизни своей.
Watu wote wa duniani waliofanikiwa wata sherekea na wata abudu; wale wote washukao katika mavumbi watapiga magoti mbele zake, wale ambao hawawezi kulinda maisha yao wenyewe.
30 Потомство мое будет служить Ему, и будет называться Господним вовек:
Kizazi kijacho kitamtumikia yeye; wao watakiambia kizazi kinachofuatia kuhusu Bwana.
31 придут и будут возвещать правду Его людям, которые родятся, что сотворил Господь.
Wao watakuja na kuzungumza kuhusu haki yake; wao watawaambia watu ambao bado hawaja zaliwa yale ambayo Yahwe ameyafanya!

< Псалтирь 22 >