< Псалтирь 2 >

1 Псалом Давида. Зачем мятутся народы, и племена замышляют тщетное?
Kwa nini mataifa wanafanya dhoruba, kwa nini watu wanafanya njama ambazo zitafeli?
2 Восстают цари земли, и князья совещаются вместе против Господа и против Помазанника Его.
Wafalme wa nchi kwa pamoja hushikilia misimamo yao na watawala kwa pamoja hufanya njama kinyume na Yahwe na kinyume na Masihi, wakisema,
3 “Расторгнем узы их, и свергнем с себя оковы их”.
“Ngoja tuzikate pingu walizo tufingia sisi na kuzitupa pingu zao.”
4 Живущий на небесах посмеется, Господь поругается им.
Yeye aketie katika mbingu atacheka kwa dharau mbele yao; Bwana atawadhihaki wao.
5 Тогда скажет им во гневе Своем и яростью Своею приведет их в смятение:
Kisha ataongea nao katika hasira yake na kuwaogofya kwa gadhabu yake, akisema,
6 “Я помазал Царя Моего над Сионом, святою горою Моею;
“Mimi mwenyewe nilimpaka mafuta mfalme wa Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7 возвещу определение: Господь сказал Мне: Ты Сын Мой; Я ныне родил Тебя;
Nami nitatangaza amri ya Yahwe. Yeye aliniambia, “wewe ni mwanangu! Leo hii nimekuwa baba yako.
8 проси у Меня, и дам народы в наследие Тебе и пределы земли во владение Тебе;
Uniombe, nami nitakupa wewe taifa kwa ajili ya urithi na mikoa ya nchi iliyo bora kwa ajili ya umiliki wako.
9 Ты поразишь их жезлом железным; сокрушишь их, как сосуд горшечника”.
Wewe utawavunja wao kwa fimbo ya chuma; kama vile mtungi wa mfinyanzi, wewe utawavunja wao vipande vipande.”
10 Итак вразумитесь, цари; научитесь, судьи земли!
Hivyo sasa, ninyi wafalme; mchukue tahadhari; mjirekebishe.
11 Служите Господу со страхом и радуйтесь с трепетом.
Mwabuduni Yahwe kwa hofu na mfurahi mkitetemeka.
12 Почтите Сына, чтобы Он не прогневался, и чтобы вам не погибнуть в пути вашем, ибо гнев Его возгорится вскоре. Блаженны все, уповающие на Него.
Mumbusu mwana vinginevyo atawakasirikia, na mtakufa pale pale hasira yake ikiwaka. Ni jinsi gani wamebarikiwa wale wote watafutao usalama ndani yake.

< Псалтирь 2 >