< Псалтирь 148 >

1 Аллилуия. Хвалите Господа с небес, хвалите Его в вышних.
Msifuni Yahwe. Msifuni Yahwe, ninyi mlio katika mbingu; msifuni yeye, ninyi mlio juu.
2 Хвалите Его, все Ангелы Его, хвалите Его, все воинства Его.
Msifuni yeye, enyi malaika wake wote; msifuni yeye, majeshi ya malaika wake wote.
3 Хвалите Его, солнце и луна, хвалите Его, все звезды света.
Msifuni yeye, enyi jua na mwezi; msifuni yeye, nyota zote zing'aazo.
4 Хвалите Его, небеса небес и воды, которые превыше небес.
Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu zaidi na maji yaliyo juu ya anga.
5 Да хвалят имя Господа, ибо Он сказал, и они сделались, повелел, и сотворились;
Na vilisifu jina la Yahwe, maana aliamuru, navyo vikaumbwa.
6 поставил их на веки и веки; дал устав, который не прейдет.
Pia ameviimrisha milele na milele; naye alitoa amri ambayo haitabadilika.
7 Хвалите Господа от земли, великие рыбы и все бездны,
Msifuni yeye kutoka nchi, ninyi viumbe wa baharini na viumbe vyote katika kina cha bahari,
8 огонь и град, снег и туман, бурный ветер, исполняющий слово Его,
moto na mvua ya mawe, theluji na mawingu, upepo wa dhoruba ukitimiza neno lake.
9 горы и все холмы, дерева плодоносные и все кедры,
Msifuni yeye, enyi milima na vilima, miti ya matunda na mierezi yote,
10 звери и всякий скот, пресмыкающиеся и птицы крылатые,
wanyama pori na wanyama wafugwao, viumbe vitambaavyo na ndege.
11 цари земные и все народы, князья и все судьи земные,
Msifuni Yahwe, wafalme wa nchi na mataifa yote, wakuu na watawala wote wa nchi,
12 юноши и девицы, старцы и отроки
wote vijana wa kiume na vijana wa kike, wazee na watoto.
13 да хвалят имя Господа, ибо имя Его единого превознесенно, слава Его на земле и на небесах.
Na walisifu jina la Yahwe, kwa kuwa jina lake pekee limetukuka na utukufu wake umeongezwa juu ya nchi na mbingu.
14 Он возвысил рог народа Своего, славу всех святых Своих, сынов Израилевых, народа, близкого к Нему. Аллилуия.
Naye ameyainua mapembe ya watu wake kwa ajili ya sifa kutoka kwa waaminifu wake wote, Waisraeli, watu wa karibu naye. Msifuni Yahwe.

< Псалтирь 148 >