< Притчи 28 >

1 Нечестивый бежит, когда никто не гонится за ним; а праведник смел, как лев.
Waovu hukimbia wakati hakuna mtu anayewafukuza, bali wale watendao haki ni thabiti kama simba kijana.
2 Когда страна отступит от закона, тогда много в ней начальников; а при разумном и знающем муже она долговечна.
Kwa sababu ya uhalifu wa nchi, kuna wakuu wengi, bali kwa mtu mwenye ufahamu na maarifa, itadumu kwa muda mrefu.
3 Человек бедный и притесняющий слабых то же, что проливной дождь, смывающий хлеб.
Mtu masikini mwenye kukandamiza watu wengine masikini ni kama mvua inayopiga ambayo haisazi chakula.
4 Отступники от закона хвалят нечестивых, а соблюдающие закон негодуют на них.
Wale wanaokataa sheria huwatukuza watu waovu, bali wale wenye kuitunza sheria hupigana dhidi yao.
5 Злые люди не разумеют справедливости, а ищущие Господа разумеют все.
Watu wabaya hawafahamu haki, bali wale wanaomtafuta Yehova wanafahamu kila kitu.
6 Лучше бедный, ходящий в своей непорочности, нежели тот, кто извращает пути свои, хотя он и богат.
Ni bora mtu masikini ambaye anatembea katika uadilifu, kuliko mtu tajiri ambaye ni mdanganyifu katika njia zake.
7 Хранящий закон - сын разумный, а знающийся с расточителями срамит отца своего.
Yeye anayetunza sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali mwenye ushirika na walafi humwaibisha baba yake.
8 Умножающий имение свое ростом и лихвою соберет его для благотворителя бедных.
Anayepata mafanikio kwa kutoza riba kubwa anakusanya utajiri wake kwa ajili ya mwingine ambaye atakuwa na huruma kwa watu masikini.
9 Кто отклоняет ухо свое от слушания закона, того и молитва - мерзость.
Kama mtu atageuzia mbali sikio lake kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
10 Совращающий праведных на путь зла сам упадет в свою яму, а непорочные наследуют добро.
Yeye anayempotosha mwenye uadilifu katika njia ya uovu ataangukia kwenye shimo lake mwenyewe, bali wakamilifu watapata urithi mwema.
11 Человек богатый - мудрец в глазах своих, но умный бедняк обличит его.
Mtu tajiri anaweza kuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu masikini mwenye ufahamu atamtafuta.
12 Когда торжествуют праведники, великая слава, но когда возвышаются нечестивые, люди укрываются.
Kunapokuwa na ushindi kwa wenye kutenda haki, kunafuraha kuu, bali wanapoinuka waovu, watu hujificha wenyewe.
13 Скрывающий свои преступления не будет иметь успеха; а кто сознается и оставляет их, тот будет помилован.
Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali mwenye kutubu na kuziacha ataonyeshwa rehema.
14 Блажен человек, который всегда пребывает в благоговении; а кто ожесточает сердце свое, тот попадет в беду.
Anafuraha ambaye huishi kwa unyenyekevu, bali anayeufanya moyo wake ataanguka katika taabu.
15 Как рыкающий лев и голодный медведь, так нечестивый властелин над бедным народом.
Kama simba anayeunguruma au dubu anayeshabulia ni kama mtawala mwovu juu ya watu masikini.
16 Неразумный правитель много делает притеснений, а ненавидящий корысть продолжит дни.
Mtawala anayekosa ufahamu ni mkandamizaji katili, bali mwenye kuchukia aibu atadumu katika siku zake.
17 Человек, виновный в пролитии человеческой крови, будет бегать до могилы, чтобы кто не схватил его.
Kama mtu anahatia kwa sababu amemwaga damu ya mtu, atakuwa mkimbizi hadi kifo na hakuna atakayemsaidia.
18 Кто ходит непорочно, тот будет невредим; а ходящий кривыми путями упадет на одном из них.
Mwenye kuenenda kwa ukaminifu atakuwa salama, bali mwenye njia ya udanganyifu ataanguka ghafla.
19 Кто возделывает землю свою, тот будет насыщаться хлебом, а кто подражает праздным, тот насытится нищетою.
Anayefanya kazi kwenye shamba lake atapata chakula kingi, bali afuataye shughuli za upuuzi atapata umasikini mkubwa.
20 Верный человек богат благословениями, а кто спешит разбогатеть, тот не останется ненаказанным.
Mtu mwaminifu atapata baraka nyingi bali apataye utajiri wa haraka hawezi kukosa adhabu.
21 Быть лицеприятным - нехорошо: такой человек и за кусок хлеба сделает неправду.
Siyo vema kuonyesha upendeleo, lakini kwa kipande cha mkate mtu atafanya ubaya.
22 Спешит к богатству завистливый человек, и не думает, что нищета постигнет его.
Mtu mchoyo huharakisha kwenye utajiri, lakini hajui ni umasikini gani utakuja juu yake.
23 Обличающий человека найдет после большую приязнь, нежели тот, кто льстит языком.
Anayemkaripia mtu baadaye atapata fadhila zaidi kutoka kwake kuliko mwenye kumsifia sana kwa ulimi wake.
24 Кто обкрадывает отца своего и мать свою и говорит: “это не грех”, тот - сообщник грабителям.
Yule anayemwibia baba yake na mama yake na kusema, “Hiyo siyo dhambi,” ni mshirika wa mwenye kuharibu.
25 Надменный разжигает ссору, а надеющийся на Господа будет благоденствовать.
Mtu mwenye tamaa huchochea mafarakano, bali anayemtumaini Yehova atafanikiwa.
26 Кто надеется на себя, тот глуп; а кто ходит в мудрости, тот будет цел.
Yule anayeutumaini moyo wake mwenyewe ni mpumbavu, bali anayekwenda kwa hekima atajilinda mbali na hatari.
27 Дающий нищему не обеднеет; а кто закрывает глаза свои от него, на том много проклятий.
Mwenye kuwapa masikini hatapungukiwa kitu, bali anayewafumbia macho atapokea laana nyingi.
28 Когда возвышаются нечестивые, люди укрываются, а когда они падают, умножаются праведники.
Watu waovu wanapoinuka, watu hujificha wenyewe, lakini watu waovu wataangamia, wale watendao haki wataongezeka.

< Притчи 28 >