< Притчи 26 >

1 Как снег летом и дождь во время жатвы, так честь неприлична глупому.
Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
2 Как воробей вспорхнет, как ласточка улетит, так незаслуженное проклятие не сбудется.
Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
3 Бич для коня, узда для осла, а палка для глупых.
Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
4 Не отвечай глупому по глупости его, чтобы и тебе не сделаться подобным ему;
Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
5 но отвечай глупому по глупости его, чтобы он не стал мудрецом в глазах своих.
Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
6 Подрезывает себе ноги, терпит неприятность тот, кто дает словесное поручение глупцу.
Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
7 Неровно поднимаются ноги у хромого, - и притча в устах глупцов.
Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
8 Что влагающий драгоценный камень в пращу, то воздающий глупому честь.
Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
9 Что колючий терн в руке пьяного, то притча в устах глупцов.
Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
10 Сильный делает все произвольно: и глупого награждает, и всякого прохожего награждает.
Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
11 Как пес возвращается на блевотину свою, так глупый повторяет глупость свою.
Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
12 Видал ли ты человека, мудрого в глазах его? На глупого больше надежды, нежели на него.
Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
13 Ленивец говорит: “Лев на дороге! лев на площадях!”
Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
14 Дверь ворочается на крючьях своих, а ленивец на постели своей.
Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
15 Ленивец опускает руку свою в чашу, и ему тяжело донести ее до рта своего.
Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
16 Ленивец в глазах своих мудрее семерых, отвечающих обдуманно.
Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
17 Хватает пса за уши, кто, проходя мимо, вмешивается в чужую ссору.
Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
18 Как притворяющийся помешанным бросает огонь, стрелы и смерть,
Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
19 так - человек, который коварно вредит другу своему и потом говорит: “я только пошутил;
ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
20 Где нет больше дров, огонь погасает, и где нет наушника, раздор утихает.
Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
21 Уголь - для жара и дрова - для огня, а человек сварливый - для разжигания ссоры.
Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
22 Слова наушника - как лакомства, и они входят во внутренность чрева.
Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
23 Что нечистым серебром обложенный глиняный сосуд, то пламенные уста и сердце злобное.
Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
24 Устами своими притворяется враг, а в сердце своем замышляет коварство.
Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
25 Если он говорит и нежным голосом, не верь ему, потому что семь мерзостей в сердце его.
Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
26 Если ненависть прикрывается наедине, то откроется злоба его в народном собрании.
Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
27 Кто роет яму, тот упадет в нее, и кто покатит вверх камень, к тому он воротится.
Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
28 Лживый язык ненавидит уязвляемых им, и льстивые уста готовят падение.
Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.

< Притчи 26 >