< Притчи 20 >

1 Вино - глумливо, сикера - буйна; и всякий, увлекающийся ими, неразумен.
Mvinyo ni mdhihaki na kileo ni mgomvi; yeyote apotoshwaye navyo hana hekima.
2 Гроза царя - как бы рев льва: кто раздражает его, тот грешит против самого себя.
Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba; yeye amkasirishaye hupoteza uhai wake.
3 Честь для человека - отстать от ссоры; а всякий глупец задорен.
Ni kwa heshima ya mtu kujitenga ugomvi, bali kila mpumbavu ni mwepesi kugombana.
4 Ленивец зимою не пашет: поищет летом - и нет ничего.
Mvivu halimi kwa majira; kwa hiyo wakati wa mavuno hutazama lakini hapati chochote.
5 Помыслы в сердце человека - глубокие воды, но человек разумный вычерпывает их.
Makusudi ya moyo wa mwanadamu ni maji yenye kina, lakini mtu mwenye ufahamu huyachota.
6 Многие хвалят человека за милосердие, но правдивого человека кто находит?
Watu wengi hujidai kuwa na upendo usiokoma, bali mtu mwaminifu ni nani awezaye kumpata?
7 Праведник ходит в своей непорочности: блаженны дети его после него!
Mtu mwenye haki huishi maisha yasiyo na lawama, wamebarikiwa watoto wake baada yake.
8 Царь, сидящий на престоле суда, разгоняет очами своими все злое.
Wakati mfalme aketipo katika kiti chake cha enzi kuhukumu, hupepeta ubaya wote kwa macho yake.
9 Кто может сказать: “Я очистил мое сердце, я чист от греха моего?”
Ni nani awezaye kusema, “Nimeuweka moyo wangu safi; mimi ni safi na sina dhambi?”
10 Неодинаковые весы, неодинаковая мера, то и другое мерзость пред Господом.
Mawe ya kupimia yaliyo tofauti na vipimo tofauti, Bwana huchukia vyote viwili.
11 Можно узнать даже отрока по занятиям его, чисто ли и правильно ли будет поведение его.
Hata mtoto hujulikana kwa matendo yake, kama tabia yake ni safi na adili.
12 Ухо слышащее и глаз видящий - и то и другое создал Господь.
Masikio yasikiayo na macho yaonayo, Bwana ndiye alivifanya vyote viwili.
13 Не люби спать, чтобы тебе не обеднеть; держи открытыми глаза твои, и будешь досыта есть хлеб.
Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini, uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.
14 “Дурно, дурно”, говорит покупатель, а когда отойдет, хвалится.
“Haifai, haifai!” asema mnunuzi, kisha huondoka akijisifia ununuzi wake.
15 Есть золото и много жемчуга, но драгоценная утварь - уста разумные.
Dhahabu kunayo, na marijani kwa wingi, lakini midomo inenayo maarifa ni kito cha thamani kilicho adimu.
16 Возьми платье его, так как он поручился за чужого; и за стороннего возьми от него залог.
Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
17 Сладок для человека хлеб, приобретенный неправдою; но после рот его наполнится дресвою.
Chakula kilichopatikana kwa hila ni kitamu kwa mwanadamu, bali huishia na kinywa kilichojaa changarawe.
18 Предприятия получают твердость чрез совещание, и по совещании веди войну.
Fanya mipango kwa kutafuta mashauri, ukipigana vita, tafuta maelekezo.
19 Кто ходит переносчиком, тот открывает тайну; и кто широко раскрывает рот, с тем не сообщайся.
Maneno ya kusengenya husababisha kutokuaminika, kwa hiyo mwepuke mtu anayezungumza kupita kiasi.
20 Кто злословит отца своего и свою мать, того светильник погаснет среди глубокой тьмы.
Ikiwa mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itazimwa katika giza nene.
21 Наследство, поспешно захваченное вначале, не благословится впоследствии.
Urithi upatikanao haraka mwanzoni, hautabarikiwa mwishoni.
22 Не говори: “Я отплачу за зло”; предоставь Господу, и Он сохранит тебя.
Usiseme, “Nitakulipiza kwa ajili ya kosa hili!” Mngojee Bwana, naye atakuokoa.
23 Мерзость пред Господом неодинаковые гири, и неверные весы - не добро.
Bwana anachukia sana mawe ya kupimia ya udanganyifu, nazo mizani zisizo halali hazimpendezi.
24 От Господа направляются шаги человека; человеку же как узнать путь свой?
Hatua za mtu huongozwa na Bwana. Anawezaje basi mtu yeyote kuelewa njia yake mwenyewe?
25 Сеть для человека - поспешно давать обет, и после обета обдумывать.
Ni mtego kwa mtu kuweka wakfu kitu kwa haraka na baada ya kitambo kidogo kufikiria tena nadhiri zake.
26 Мудрый царь вывеет нечестивых и обратит на них колесо.
Mfalme mwenye hekima hupepeta waovu, hulipitisha gurudumu la kupuria juu yao.
27 Светильник Господень - дух человека, испытывающий все глубины сердца.
Taa ya Bwana huchunguza roho ya mwanadamu, huchunguza utu wake wa ndani.
28 Милость и истина охраняют царя, и милостью он поддерживает престол свой.
Upendo na uaminifu humweka mfalme salama, kwa njia ya upendo, kiti chake cha enzi huwa salama.
29 Слава юношей - сила их, а украшение стариков - седина.
Utukufu wa vijana ni nguvu zao, mvi ni fahari ya uzee.
30 Раны от побоев врачевство против зла, и удары, проникающие во внутренности чрева.
Mapigo na majeraha huusafisha ubaya, nayo michapo hutakasa utu wa ndani.

< Притчи 20 >