< Притчи 12 >

1 Кто любит наставление, тот любит знание; а кто ненавидит обличение, тот невежда.
Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
2 Добрый приобретает благоволение от Господа; а человека коварного Он осудит.
Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
3 Не утвердит себя человек беззаконием; корень же праведников неподвижен.
Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
4 Добродетельная жена - венец для мужа своего; а позорная - как гниль в костях его.
Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
5 Помышления праведных - правда, а замыслы нечестивых - коварство.
Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
6 Речи нечестивых - засада для пролития крови, уста же праведных спасают их.
Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
7 Коснись нечестивых несчастие - и нет их, а дом праведных стоит.
Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
8 Хвалят человека по мере разума его, а развращенный сердцем будет в презрении.
Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
9 Лучше простой, но работающий на себя, нежели выдающий себя за знатного, но нуждающийся в хлебе.
Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
10 Праведный печется и о жизни скота своего, сердце же нечестивых жестоко.
Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
11 Кто возделывает землю свою, тот будет насыщаться хлебом; а кто идет по следам празднолюбцев, тот скудоумен.
Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
12 Нечестивый желает уловить в сеть зла; но корень праведных тверд.
Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
13 Нечестивый уловляется грехами уст своих; но праведник выйдет из беды. Смотрящий кротко помилован будет, а встречающийся в воротах стеснит других.
Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
14 От плода уст своих человек насыщается добром, и воздаяние человеку - по делам рук его.
Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
15 Путь глупого прямой в его глазах; но кто слушает совета, тот мудр.
Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
16 У глупого тотчас же выкажется гнев его, а благоразумный скрывает оскорбление.
Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
17 Кто говорит то, что знает, тот говорит правду; а у свидетеля ложного - обман.
Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
18 Иной пустослов уязвляет как мечом, а язык мудрых - врачует.
Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
19 Уста правдивые вечно пребывают, а лживый язык - только на мгновение.
Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
20 Коварство - в сердце злоумышленников, радость - у миротворцев.
Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
21 Не приключится праведнику никакого зла, нечестивые же будут преисполнены зол.
Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
22 Мерзость пред Господом - уста лживые, а говорящие истину благоугодны Ему.
Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
23 Человек рассудительный скрывает знание, а сердце глупых высказывает глупость.
Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
24 Рука прилежных будет господствовать, а ленивая будет под данью.
Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
25 Тоска на сердце человека подавляет его, а доброе слово развеселяет его.
Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
26 Праведник указывает ближнему своему путь, а путь нечестивых вводит их в заблуждение.
Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
27 Ленивый не жарит своей дичи; а имущество человека прилежного многоценно.
Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
28 На пути правды - жизнь, и на стезе ее нет смерти.
Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.

< Притчи 12 >