< Притчи 10 >

1 Притчи Соломона. Сын мудрый радует отца, а сын глупый - огорчение для его матери.
Mithali za Sulemani. Mwana mwenye hekima humfurahisha baba yake lakini mwana mpumbavu huleta majonzi kwa mama yake.
2 Не доставляют пользы сокровища неправедные, правда же избавляет от смерти.
Hazina zilizolimbikizwa kwa uovu hakosa thamani, bali kwa kutenda haki hujilinda mbali na kifo.
3 Не допустит Господь терпеть голод душе праведного, стяжание же нечестивых исторгнет.
Yehova hawaachi wale watendao haki wapate njaa, bali hamu ya waovu huizuia.
4 Ленивая рука делает бедным, а рука прилежных обогащает.
Mkono mlegevu humfanya mtu awe masikini, bali mkono wa mtu mwenye bidii hupata utajiri.
5 Собирающий во время лета - сын разумный, спящий же во время жатвы - сын беспутный.
Mwana mwenye busara hukusanya mazao wakati wa kiangazi, bali ni aibu kwake alalaye wakati wa mavuno.
6 Благословения - на голове праведника, уста же беззаконных заградит насилие.
Zawadi kutoka kwa Mungu zipo juu ya kichwa cha wale watendao haki; bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
7 Память праведника пребудет благословенна, а имя нечестивых омерзеет.
Mtu atendaye haki anatufurahisha tunapomkumbuka, bali jina la mwovu litaoza.
8 Мудрый сердцем принимает заповеди, а глупый устами преткнется.
Wale wenye akili hukubali maagiza, bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataangamia.
9 Кто ходит в непорочности, тот ходит безопасно; а кто превращает пути свои, тот будет наказан.
Yeye anayetembea katika uadilifu hutembea katika usalama, bali yule anayepotosha njia zake, ataonekana.
10 Кто мигает глазами, тот причиняет досаду, а глупый устами преткнется.
Yeye ambaye hukonyeza kwa jicho lake huleta majonzi, bali mpumbavu mwenye maneno mengi atatupwa chini.
11 Уста праведника - источник жизни, уста же беззаконных заградит насилие.
Kinywa cha mwenye kutenda haki ni kama chemchemi ya maji ya uzima, bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
12 Ненависть возбуждает раздоры, но любовь покрывает все грехи.
Chuki huchochea mafarakano, bali upendo hufunika juu ya makwazo yote.
13 В устах разумного находится мудрость, но на теле глупого - розга.
Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
14 Мудрые сберегают знание, но уста глупого близкая погибель.
Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
15 Имущество богатого - крепкий город его, беда для бедных - скудость их.
Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
16 Труды праведного - к жизни, успех нечестивого - ко греху.
Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.
17 Кто хранит наставление, тот на пути к жизни; а отвергающий обличение - блуждает.
Kuna njia kwenda kwenye uzima kwa yule anayefuata maongozo, bali anayekataa maonyo hupotea.
18 Кто скрывает ненависть, у того уста лживые; и кто разглашает клевету, тот глуп.
Yeye afichaye chuki anamidomo ya uongo, na yeye anayesambaza kashfa ni mpumbavu.
19 При многословии не миновать греха, а сдерживающий уста свои - разумен.
Katika maneno mengi, hapakosi uhalifu, bali aliyemwangalifu katika usemi wake ni mwenye busara.
20 Отборное серебро язык праведного, сердце же нечестивых - ничтожество.
Ulimi wa yule atendaye haki ni fedha safi; kuna thamani ndogo katika moyo wa mbaya.
21 Уста праведного пасут многих, а глупые умирают от недостатка разума.
Midomo ya yule atendaye haki huwastawisha wengi, bali wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa akili.
22 Благословение Господне - оно обогащает и печали с собою не приносит.
Zawadi njema za Yehova huleta utajiri na haweki maumivu ndani yake.
23 Для глупого преступное деяние как бы забава, а человеку разумному свойственна мудрость.
Uovu ni mchezo achezao mpumbavu, bali hekima ni furaha kwa mtu mwenye ufahamu.
24 Чего страшится нечестивый, то и постигнет его, а желание праведников исполнится.
Hofu ya mwenye uovu humkumba ghafla, bali shauku ya mwenye haki itatimizwa.
25 Как проносится вихрь, так нет более нечестивого; а праведник - на вечном основании.
Waovu ni kama dhoruba inayopita, na hawapo tena, bali mwenye haki ni msingi unaodumu milele.
26 Что уксус для зубов и дым для глаз, то ленивый для посылающих его.
Kama siki kwenye meno na moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27 Страх Господень прибавляет дней, лета же нечестивых сократятся.
Hofu ya Yehova huongeza maisha, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
28 Ожидание праведников радость, а надежда нечестивых погибнет.
Matumaini ya wale watendao haki ndiyo furaha yao, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
29 Путь Господень - твердыня для непорочного и страх для делающих беззаконие.
Njia ya Yehova huwalinda wale wenye uadilifu, bali kwa waovu ni uhalibifu.
30 Праведник во веки не поколеблется, нечестивые же не поживут на земле.
Wale watendao haki hawataondolewa, bali waovu hawatabaki katika nchi.
31 Уста праведника источают мудрость, а язык зловредный отсечëтся.
Katika kinywa cha wale watendao haki hutoka tunda la hekima, bali ulimi wa kupotosha utakatwa.
32 Уста праведного знают благоприятное, а уста нечестивых - развращенное.
Midomo ya wale watendao mema huyajua yanayokubalika, bali kinywa cha waovu, huyajua yanayopotosha.

< Притчи 10 >