< Иисус Навин 12 >

1 Вот цари той земли, которых поразили сыны Израилевы и которых землю взяли в наследие по ту сторону Иордана к востоку солнца, от потока Арнона до горы Ермона, и всю равнину к востоку:
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:
2 Сигон, царь Аморрейский, живший в Есевоне, владевший от Ароера, что при береге потока Арнона, и от средины потока, половиною Галаада, до потока Иавока, предела Аммонитян,
Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni. Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi.
3 и равниною до самого моря Хиннерефского к востоку и до моря равнины, моря Соленого, к востоку по дороге к Беф-Иешимофу, а к югу местами, лежащими при подошве Фасги;
Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.
4 сопредельный ему Ог, царь Васанский, последний из Рефаимов, живший в Астарофе и в Едреи,
Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.
5 владевший горою Ермоном и Салхою и всем Васаном, до предела Гессурского и Маахского, и половиною Галаада, до предела Сигона, царя Есевонского.
Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.
6 Моисей, раб Господень, и сыны Израилевы убили их; и дал ее Моисей, раб Господень, в наследие колену Рувимову и Гадову и половине колена Манассиина.
Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.
7 И вот цари Аморрейской земли, которых поразил Иисус и сыны Израилевы по эту сторону Иордана к западу, от Ваал-Гада на долине Ливанской до Халака, горы, простирающейся к Сеиру, которую отдал Иисус коленам Израилевым в наследие, по разделению их,
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao:
8 на горе, на низменных местах, на равнине, на местах, лежащих при горах, и в пустыне и на юге, Хеттеев, Аморреев, Хананеев, Ферезеев, Евеев и Иевусеев:
nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):
9 один царь Иерихона, один царь Гая, что близ Вефиля,
mfalme wa Yeriko mmoja mfalme wa Ai (karibu na Betheli) mmoja
10 один царь Иерусалима, один царь Хеврона,
mfalme wa Yerusalemu mmoja mfalme wa Hebroni mmoja
11 один царь Иармуфа, один царь Лахиса,
mfalme wa Yarmuthi mmoja mfalme wa Lakishi mmoja
12 один царь Еглона, один царь Газера,
mfalme wa Egloni mmoja mfalme wa Gezeri mmoja
13 один царь Давира, один царь Гадера,
mfalme wa Debiri mmoja mfalme wa Gederi mmoja
14 один царь Хормы, один царь Арада,
mfalme wa Horma mmoja mfalme wa Aradi mmoja
15 один царь Ливны, один царь Одоллама,
mfalme wa Libna mmoja mfalme wa Adulamu mmoja
16 один царь Македа, один царь Вефиля,
mfalme wa Makeda mmoja mfalme wa Betheli mmoja
17 один царь Таппуаха, один царь Хефера.
mfalme wa Tapua mmoja mfalme wa Heferi mmoja
18 Один царь Афека, один царь Шарона,
mfalme wa Afeki mmoja mfalme wa Lasharoni mmoja
19 один царь Мадона, один царь Асора,
mfalme wa Madoni mmoja mfalme wa Hazori mmoja
20 один царь Шимрон-Мерона, один царь Ахсафа,
mfalme wa Shimron-Meroni mmoja mfalme wa Akishafu mmoja
21 один царь Фаанаха, один царь Мегиддона,
mfalme wa Taanaki mmoja mfalme wa Megido mmoja
22 один царь Кедеса, один царь Иокнеама при Кармиле,
mfalme wa Kedeshi mmoja mfalme wa Yokneamu katika Karmeli mmoja
23 один царь Дора при Нафаф-Доре, один царь Гоима в Галгале,
mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori) mmoja mfalme wa Goimu katika Gilgali mmoja
24 один царь Фирцы. Всех царей тридцать один.
mfalme wa Tirsa mmoja wafalme jumla yao ilikuwa thelathini na mmoja.

< Иисус Навин 12 >