< Иов 38 >

1 Когда Елиуй перестал говорить, Господь отвечал Иову из бури и сказал:
Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
2 кто сей, омрачающий Провидение словами без смысла?
“Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
3 Препояшь ныне чресла твои, как муж: Я буду спрашивать тебя, и ты объясняй Мне:
Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
4 где был ты, когда Я полагал основания земли? Скажи, если знаешь.
Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
5 Кто положил меру ей, если знаешь? или кто протягивал по ней вервь?
Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
6 На чем утверждены основания ее, или кто положил краеугольный камень ее,
Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
7 при общем ликовании утренних звезд, когда все сыны Божии восклицали от радости?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
8 Кто затворил море воротами, когда оно исторглось, вышло как бы из чрева,
Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
9 когда Я облака сделал одеждою его и мглу пеленами его,
wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
10 и утвердил ему Мое определение, и поставил запоры и ворота,
Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
11 и сказал: доселе дойдешь и не перейдешь, и здесь предел надменным волнам твоим?
na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
12 Давал ли ты когда в жизни своей приказания утру и указывал ли заре место ее,
Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
13 чтобы она охватила края земли и стряхнула с нее нечестивых,
ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
14 чтобы земля изменилась, как глина под печатью, и стала, как разноцветная одежда,
Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
15 и чтобы отнялся у нечестивых свет их и дерзкая рука их сокрушилась?
'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
16 Нисходил ли ты во глубину моря и входил ли в исследование бездны?
Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
17 Отворялись ли для тебя врата смерти, и видел ли ты врата тени смертной?
Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
18 Обозрел ли ты широту земли? Объясни, если знаешь все это.
Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
19 Где путь к жилищу света, и где место тьмы?
Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
20 Ты, конечно, доходил до границ ее и знаешь стези к дому ее.
Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
21 Ты знаешь это, потому что ты был уже тогда рожден, и число дней твоих очень велико.
Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
22 Входил ли ты в хранилища снега и видел ли сокровищницы града,
Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
23 которые берегу Я на время смутное, на день битвы и войны?
vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
24 По какому пути разливается свет и разносится восточный ветер по земле?
Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
25 Кто проводит протоки для излияния воды и путь для громоносной молнии,
Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
26 чтобы шел дождь на землю безлюдную, на пустыню, где нет человека,
na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
27 чтобы насыщать пустыню и степь и возбуждать травные зародыши к возрастанию?
kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
28 Есть ли у дождя отец? или кто рождает капли росы?
Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
29 Из чьего чрева выходит лед, и иней небесный, - кто рождает его?
Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
30 Воды, как камень, крепнут, и поверхность бездны замерзает.
Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
31 Можешь ли ты связать узел Хима и разрешить узы Кесиль?
Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
32 Можешь ли выводить созвездия в свое время и вести Ас с ее детьми?
Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
33 Знаешь ли ты уставы неба, можешь ли установить господство его на земле?
Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
34 Можешь ли возвысить голос твой к облакам, чтобы вода в обилии покрыла тебя?
Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
35 Можешь ли посылать молнии, и пойдут ли они и скажут ли тебе: вот мы?
Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
36 Кто вложил мудрость в сердце, или кто дал смысл разуму?
Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
37 Кто может расчислить облака своею мудростью и удержать сосуды неба,
Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
38 когда пыль обращается в грязь и глыбы слипаются?
wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
39 Ты ли ловишь добычу львице и насыщаешь молодых львов,
Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
40 когда они лежат в берлогах или покоятся под тенью в засаде?
wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
41 Кто приготовляет ворону корм его, когда птенцы его кричат к Богу, бродя без пищи?
Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?

< Иов 38 >