< Иов 37 >

1 И от сего трепещет сердце мое и подвиглось с места своего.
“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
2 Слушайте, слушайте голос Его и гром, исходящий из уст Его.
Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
3 Под всем небом раскат его, и блистание его - до краев земли.
Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
4 За ним гремит глас; гремит Он гласом величества Своего и не останавливает его, когда голос Его услышан.
Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
5 Дивно гремит Бог гласом Своим, делает дела великие, для нас непостижимые.
Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
6 Ибо снегу Он говорит: будь на земле; равно мелкий дождь и большой дождь в Его власти.
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7 Он полагает печать на руку каждого человека, чтобы все люди знали дело Его.
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8 Тогда зверь уходит в убежище и остается в своих логовищах.
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9 От юга приходит буря, от севера - стужа.
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10 От дуновения Божия происходит лед, и поверхность воды сжимается.
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11 Также влагою Он наполняет тучи, и облака сыплют свет Его,
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12 и они направляются по намерениям Его, чтоб исполнить то, что Он повелит им на лице обитаемой земли.
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13 Он повелевает им идти или для наказания, или в благоволение, или для помилования.
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
14 Внимай сему, Иов; стой и разумевай чудные дела Божии.
“Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
15 Знаешь ли, как Бог располагает ими и повелевает свету блистать из облака Своего?
Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
16 Разумеешь ли равновесие облаков, чудное дело Совершеннейшего в знании?
Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
17 Как нагревается твоя одежда, когда Он успокаивает землю от юга?
Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
18 Ты ли с Ним распростер небеса, твердые, как литое зеркало?
je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
19 Научи нас, что сказать Ему? Мы в этой тьме ничего не можем сообразить.
“Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
20 Будет ли возвещено Ему, что я говорю? Сказал ли кто, что сказанное доносится Ему?
Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
21 Теперь не видно яркого света в облаках, но пронесется ветер и расчистит их.
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22 Светлая погода приходит от севера, и окрест Бога страшное великолепие.
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23 Вседержитель! мы не постигаем Его. Он велик силою, судом и полнотою правосудия. Он никого не угнетает.
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24 Посему да благоговеют пред Ним люди, и да трепещут пред Ним все мудрые сердцем!
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

< Иов 37 >