< Иов 29 >

1 И продолжал Иов возвышенную речь свою и сказал:
Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
2 о, если бы я был, как в прежние месяцы, как в те дни, когда Бог хранил меня,
“Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
3 когда светильник Его светил над головою моею, и я при свете Его ходил среди тьмы;
wakati taa yake iliniangazia kichwani changu, na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!
4 как был я во дни молодости моей, когда милость Божия была над шатром моим,
Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
5 когда еще Вседержитель был со мною, и дети мои вокруг меня,
wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
6 когда пути мои обливались молоком, и скала источала для меня ручьи елея!
wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
7 когда я выходил к воротам города и на площади ставил седалище свое, -
“Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
8 юноши, увидев меня, прятались, а старцы вставали и стояли;
vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
9 князья удерживались от речи и персты полагали на уста свои;
wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
10 голос знатных умолкал, и язык их прилипал к гортани их.
wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
11 Ухо, слышавшее меня, ублажало меня; око видевшее восхваляло меня,
Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
12 потому что я спасал страдальца вопиющего и сироту беспомощного.
kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
13 Благословение погибавшего приходило на меня, и сердцу вдовы доставлял я радость.
Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
14 Я облекался в правду, и суд мой одевал меня, как мантия и увясло.
Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
15 Я был глазами слепому и ногами хромому;
Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
16 отцом был я для нищих и тяжбу, которой я не знал, разбирал внимательно.
Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
17 Сокрушал я беззаконному челюсти и из зубов его исторгал похищенное.
Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
18 И говорил я: в гнезде моем скончаюсь, и дни мои будут многи, как песок;
“Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe, nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.
19 корень мой открыт для воды, и роса ночует на ветвях моих;
Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji, nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.
20 слава моя не стареет, лук мой крепок в руке моей.
Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu, upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’
21 Внимали мне и ожидали, и безмолвствовали при совете моем.
“Watu walinisikiliza kwa tumaini, wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.
22 После слов моих уже не рассуждали; речь моя капала на них.
Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.
23 Ждали меня, как дождя, и, как дождю позднему, открывали уста свои.
Waliningojea kama manyunyu ya mvua na kuyapokea maneno yangu kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.
24 Бывало, улыбнусь им - они не верят; и света лица моего они не помрачали.
Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha; nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.
25 Я назначал пути им и сидел во главе и жил как царь в кругу воинов, как утешитель плачущих.
Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao; niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake; nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.

< Иов 29 >