< Бытие 36 >

1 Вот родословие Исава, он же Едом.
Hivi ndivyo vizazi vya Esau (yaani Edomu).
2 Исав взял себе жен из дочерей Ханаанских: Аду, дочь Елона Хеттеянина, и Оливему, дочь Аны, сына Цивеона Евеянина,
Esau akaoa wake kutoka miongoni mwa wanawake wa Kanaani: Ada binti wa Eloni Mhiti, Oholibama binti wa Ana, mjukuu wa kike wa Sibeoni Mhivi,
3 и Васемафу, дочь Измаила, сестру Наваиофа.
pia akaoa Basemathi binti wa Ishmaeli, dada yake Nebayothi.
4 Ада родила Исаву Елифаза, Васемафа родила Рагуила,
Ada akamzalia Esau Elifazi, Basemathi akamzaa Reueli,
5 Оливема родила Иеуса, Иеглома и Корея. Это сыновья Исава, родившиеся ему в земле Ханаанской.
Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wana wa Esau waliozaliwa kwake huko Kanaani.
6 И взял Исав жен своих и сыновей своих, и дочерей своих, и всех людей дома своего, и все стада свои, и весь скот свой, и все имение свое, которое он приобрел в земле Ханаанской, и пошел Исав в другую землю от лица Иакова, брата своего,
Esau akawachukua wake zake, watoto wake wa kiume na wa kike na wote wa nyumbani mwake, mifugo yake pamoja na wanyama wake wengine wote na mali yake yote ambayo alikuwa ameipata akiwa Kanaani, akahamia katika nchi iliyo mbali na Yakobo ndugu yake.
7 ибо имение их было так велико, что они не могли жить вместе, и земля странствования их не вмещала их, по множеству стад их.
Mali zao zilikuwa nyingi sana kiasi kwamba haikuwa rahisi wao kuishi pamoja, nchi waliyokuwa wakiishi isingewatosha wote kwa ajili ya mifugo yao.
8 И поселился Исав на горе Сеир, Исав, он же Едом.
Kwa hiyo Esau (ambaye ni Edomu) aliishi katika nchi ya kilima huko Seiri.
9 И вот родословие Исава, отца Идумеев, на горе Сеир.
Hawa ndio wazao wa Esau, baba wa Waedomu, katika nchi ya kilima cha Seiri.
10 Вот имена сынов Исава: Елифаз, сын Ады, жены Исавовой, и Рагуил, сын Васемафы, жены Исавовой.
Haya ndiyo majina ya wana wa Esau: Elifazi, mwana wa Esau ambaye mkewe Ada alimzalia; na Reueli, mwana wa Esau ambaye mkewe Basemathi alimzalia.
11 У Елифаза были сыновья: Феман, Омар, Цефо, Гафам и Кеназ.
Wana wa Elifazi ni: Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi.
12 Фамна же была наложница Елифаза, сына Исавова, и родила Елифазу Амалика. Вот сыновья Ады, жены Исавовой.
Elifazi mwana wa Esau alikuwa pia na suria aliyeitwa Timna, ambaye alimzalia Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Ada mke wa Esau.
13 И вот сыновья Рагуила: Нахаф и Зерах, Шамма и Миза. Это сыновья Васемафы, жены Исавовой.
Wana wa Reueli ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Basemathi mkewe Esau.
14 И сии были сыновья Оливемы, дочери Аны, сына Цивеонова, жены Исавовой: она родила Исаву Иеуса, Иеглома и Корея.
Wana wa Oholibama binti Ana, mkewe Esau, aliyekuwa mjukuu wa Sibeoni, aliomzalia Esau ni: Yeushi, Yalamu na Kora.
15 Вот старейшины сынов Исавовых. Сыновья Елифаза, первенца Исавова: старейшина Феман, старейшина Омар, старейшина Цефо, старейшина Кеназ,
Hawa ndio waliokuwa wakuu miongoni mwa wazao wa Esau: Wakuu wa wana wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau ni: Temani, Omari, Sefo, Kenazi,
16 старейшина Корей, старейшина Гафам, старейшина Амалик. Сии старейшины Елифазовы в земле Едома; сии сыновья Ады.
Kora, Gatamu na Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wakuu waliotoka kwa Elifazi huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Ada.
17 Сии сыновья Рагуила, сына Исавова: старейшина Нахаф, старейшина Зерах, старейшина Шамма, старейшина Миза. Сии старейшины Рагуиловы в земле Едома; сии сыновья Васемафы, жены Исавовой.
Wakuu wa wana wa Reueli, mwana wa Esau ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa Reueli huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Basemathi mkewe Esau.
18 Сии сыновя Оливеммы, жены Исавовой: старейшина Иеус, старейшина Иеглом, старейшина Корей. Сии старейшины Оливемы, дочери Аны, жены Исавовой.
Wakuu wa wana wa Esau ambao mkewe Oholibama alimzalia ni: Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa mke wa Esau, Oholibama binti Ana.
19 Вот сыновья Исава, и вот старейшины их. Это Едом.
Hawa ndio waliokuwa wana wa Esau (ndiye Edomu), na hawa ndio waliokuwa wakuu wao.
20 Сии сыновья Сеира Хорреянина, жившие в земле той: Лотан, Шовал, Цивеон, Ана,
Hawa ndio walikuwa wana wa Seiri, Mhori, waliokuwa wakiishi katika nchi ile: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
21 Дишон, Эцер и Дишан. Сии старейшины Хорреев, сынов Сеира, в земле Едома.
Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio wana wa Seiri huko Edomu waliokuwa wakuu kwa Wahori.
22 Сыновья Лотана были: Хори и Геман; а сестра у Лотана: Фамна.
Wana wa Lotani walikuwa: Hori na Homamu. Timna alikuwa dada yake Lotani.
23 Сии сыновья Шовала: Алван, Манахаф, Эвал, Шефо и Онам.
Wana wa Shobali walikuwa: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo na Onamu.
24 Сии сыновья Цивеона: Аиа и Ана. Это тот Ана, который нашел теплые воды в пустыне, когда пас ослов Цивеона, отца своего.
Wana wa Sibeoni walikuwa: Aiya na Ana. Huyu Ana ndiye aligundua chemchemi ya maji moto jangwani alipokuwa akichunga punda za Sibeoni baba yake.
25 Сии дети Аны: Дишон и Оливема, дочь Аны.
Watoto wa Ana walikuwa: Dishoni na Oholibama binti wa Ana.
26 Сии сыновья Дишона: Хемдан, Эшбан, Ифран и Херан.
Wana wa Dishoni walikuwa: Hemdani, Eshbani, Ithrani na Kerani.
27 Сии сыновья Эцера: Билган, Зааван, Укам и Акан.
Wana wa Eseri walikuwa: Bilhani, Zaavani na Akani.
28 Сии сыновья Дишана: Уц и Аран.
Wana wa Dishani walikuwa: Usi na Arani.
29 Сии старейшины Хорреев: старейшина Лотан, старейшина Шовал, старейшина Цивеон, старейшина Ана,
Hawa ndio waliokuwa wakuu wa Wahori: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
30 старейшина Дишон, старейшина Эцер, старейшина Дишан. Вот старейшины Хорреев, по старшинствам их в земле Сеир.
Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Wahori, kufuatana na makundi yao, katika nchi ya Seiri.
31 Вот цари, царствовавшие в земле Едома, прежде царствования царей у сынов Израилевых:
Wafuatao ni wafalme waliotawala Edomu kabla ya mfalme yeyote wa Israeli kutawala:
32 царствовал в Едоме Бела, сын Веоров, а имя городу его Дингава.
Bela mwana wa Beori alikuwa mfalme wa Edomu. Mji wake uliitwa Dinhaba.
33 И умер Бела, и воцарился по нем Иовав, сын Зераха, из Восоры.
Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra akawa mfalme baada yake.
34 Умер Иовав, и воцарился по нем Хушам, из земли Феманитян.
Yobabu alipofariki, Hushamu kutoka nchi ya Watemani akawa mfalme baada yake.
35 И умер Хушам, и воцарился по нем Гадад, сын Бедадов, который поразил Мадианитян на поле Моава; имя городу его Авиф.
Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi, aliyeshinda Midiani katika nchi ya Moabu, akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Avithi.
36 И умер Гадад, и воцарился по нем Самла из Масреки.
Hadadi alipofariki, Samla kutoka Masreka akawa mfalme baada yake.
37 И умер Самла, и воцарился по нем Саул из Реховофа, что при реке.
Samla alipofariki, Shauli kutoka Rehobothi ngʼambo ya Mto Frati akawa mfalme baada yake.
38 И умер Саул, и воцарился по нем Баал-Ханан, сын Ахбора.
Shauli alipofariki, Baal-Hanani mwana wa Akbori akawa mfalme baada yake.
39 И умер Баал-Ханан, сын Ахбора, и воцарился по нем Гадар сын Варадов; имя городу его Пау; имя жене его Мегетавеель, дочь Матреды, сына Мезагава.
Baal-Hanani mwana wa Akbori alipofariki, Hadadi akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Pau, na mkewe aliitwa Mehetabeli binti Matredi, binti Me-Zahabu.
40 Сии имена старейшин Исавовых, по племенам их, по местам их, по именам их, по народам их: старейшина Фимна, старейшина Алва, старейшина Иетеф,
Hawa ndio wakuu waliotokana na Esau, kwa majina, kufuatana na koo zao na nchi zao: Timna, Alva, Yethethi,
41 старейшина Оливема, старейшина Эла, старейшина Пинон,
Oholibama, Ela, Pinoni,
42 старейшина Кеназ, старейшина Феман, старейшина Мивцар,
Kenazi, Temani, Mibsari,
43 старейшина Магдиил, старейшина Ирам. Вот старейшины Идумейские, по их селениям, в земле обладания их. Вот Исав, отец Идумеев.
Magdieli na Iramu. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Edomu, kufuatana na makazi yao katika nchi waliyoimiliki. Huyu ndiye alikuwa Esau, baba wa Waedomu.

< Бытие 36 >