< Бытие 21 >

1 И призрел Господь на Сарру, как сказал; и сделал Господь Сарре, как говорил.
Yahwe akamsikiliza Sara kwa umakini kama alivyo kuwa amemwambia, Yahwe akamfanyia Sara kama alivyo kuwa amemwahidi.
2 Сарра зачала и родила Аврааму сына в старости его во время, о котором говорил ему Бог;
Sara akachukua mimba na akamzalia Abraham mtoto wa kiume katika uzee wake, katika muda ule ule ambao Mungu alikuwa amemwambia.
3 и нарек Авраам имя сыну своему, родившемуся у него, которого родила ему Сарра, Исаак;
Abraham akamwita jina mwanawe, ambaye alizaliwa kwake, na Sara, Isaka.
4 и обрезал Авраам Исаака, сына своего, в восьмой день, как заповедал ему Бог.
Abraham akamtahiri mwanawe Isaka alipofikisha siku nane, kama vile Mungu alivyokuwa amemwagiza.
5 Авраам был ста лет, когда родился у него Исаак, сын его.
Abraham alikuwa na umri wa miaka mia moja wakati mwanawe Isaka anazaliwa kwake.
6 И сказала Сарра: смех сделал мне Бог; кто ни услышит обо мне, рассмеется.
Sara akasema, “Mungu amenifanya nicheke; kila mtu atakaye sikia atacheka pamoja na nami.”
7 И сказала: кто сказал бы Аврааму: Сарра будет кормить детей грудью? ибо в старости его я родила сына.
Pia akasema, “Nani angesema kwa Abraham kwamba Sara atalea mtoto, na sasa kweli nimemzalia mtoto wakiume katika uzee wake!”
8 Дитя выросло и отнято от груди; и Авраам сделал большой пир в тот день, когда Исаак сын его отнят был от груди.
Mtoto akakua na akaachishwa kunyonya, na Abraham akafanya sherehe kubwa katika siku ambayo Isaka aliachishwa.
9 И увидела Сарра, что сын Агари Египтянки, которого она родила Аврааму, насмехается над ее сыном, Исааком,
Sara akamwona mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alikuwa amezaliwa kwa Abraham, akidhihaki.
10 и сказала Аврааму: выгони эту рабыню и сына ее, ибо не наследует сын рабыни сей с сыном моим Исааком.
Kwa hiyo akamwambia Abraham, “Mfukuze huyu mwanamke huyu mtumwa pamoja na mtoto wake: kwa kuwa mtoto huyu wa mwanamke mtumwa hawezi kuwa mrithi pamoja na mwanangu Isaka.”
11 И показалось это Аврааму весьма неприятным ради сына его Измаила.
Jambo hili likamuhuzunisha sana Abraham kwa sababu ya mwanawe.
12 Но Бог сказал Аврааму: не огорчайся ради отрока и рабыни твоей; во всем, что скажет тебе Сарра, слушайся голоса ее, ибо в Исааке наречется тебе семя;
Lakini Mungu akamwambia Abraham, “Usihuzunike kwa sababu ya kijana huyu, na kwa sababu ya mwanamke huyu mtumwa wako. Sikiliza maneno asemayo Sara juu ya jambo hili, kwa sababu itakuwa kupitia Isaka kwamba uzao wako utaitwa.
13 и от сына рабыни Я произведу великий народ, потому что он семя твое.
Nitamfanya pia mtoto wa mjakazi kuwa taifa, kwa sababu ni uzao wako.”
14 Авраам встал рано утром, и взял хлеба и мех воды, и дал Агари, положив ей на плечи, и отрока, и отпустил ее. Она пошла, и заблудилась в пустыне Вирсавии;
Abraham akaamka asubuhi na mapema, akachukua mkate na kiriba cha maji, akampatia Hajiri, akiweka juu ya bega lake. Akamtoa kijana akampatia Hajiri na akawaondoa. Hajiri akaondoka akapotea katika jangwa la Beerisheba.
15 и не стало воды в мехе, и она оставила отрока под одним кустом
Maji yalipokwisha kwenye kiriba akamtelekeza kijana katika moja ya vichaka.
16 и пошла, села вдали, в расстоянии на один выстрел из лука. Ибо она сказала: не хочу видеть смерти отрока. И она села поодаль против него, и подняла вопль, и плакала;
Kisha akaondoka, na akakaa umbali kidogo na yule kijana, umbali kama wa kutupa mshale, kwa vile alisema, “Na nisitazame kifo cha mtoto.” Alipokuwa amekaa kumkabili, akapaza sauti yake akalia.
17 и услышал Бог голос отрока оттуда, где он был; и Ангел Божий с неба воззвал к Агари и сказал ей: что с тобою, Агарь? не бойся; Бог услышал голос отрока оттуда, где он находится;
Mungu akasikia kilio cha kijana, na malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, “Nini kinakusumbua? Usiogope, kwa kuwa Mungu amesikia kilio cha kijana mahali alipo.
18 встань, подними отрока и возьми его за руку, ибо Я произведу от него великий народ.
Inuka msimamishe mtoto, na umtie moyo; kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa.”
19 И Бог открыл глаза ее, и она увидела колодезь с водою живою, и пошла, наполнила мех водою и напоила отрока.
Kisha Mungu akayafunua macho ya Hajiri, natazama akaona kisima cha maji. Akaenda akajaza kiriba maji, na akampatia kijana akanywa.
20 И Бог был с отроком; и он вырос, и стал жить в пустыне, и сделался стрелком из лука.
Mungu akawa pamoja na kijana, na akakua. Akaishi jangwani akawa mwindaji.
21 Он жил в пустыне Фаран; и мать его взяла ему жену из земли Египетской.
Akaishi katka jangwa la Parani, na mama yake akampatia mke kutoka Misri.
22 И было в то время, Авимелех с Фихолом, военачальником своим, сказал Аврааму: с тобою Бог во всем, что ты ни делаешь;
Ikawa kwamba katika wakati ule Abimeleki na Fikoli kamanda wa jeshi lake akamwambia Abraham, akisema, “Mungu yuko pamoja na wewe katika yote uyatendayo.
23 и теперь поклянись мне здесь Богом, что ты не обидишь ни меня, ни сына моего, ни внука моего; и как я хорошо поступал с тобою, так и ты будешь поступать со мною и землею, в которой ты гостишь.
Sasa niapie kwa Mungu kwamba hutanifanyia baya, wala mwanangu, wala uzao wangu. Onesha kwangu na kwa nchi ambayo umekuwa ukikaa agano lile lile la uaminifu ambalo nimekuonesha wewe.”
24 И сказал Авраам: я клянусь.
Abraham akasema, “Nina apa.”
25 И Авраам упрекал Авимелеха за колодезь с водою, который отняли рабы Авимелеховы.
Abraham pia akamlalamikia Abimeleki kuhusu kisima cha maji ambacho watumishi wa Abimeleki wamekinyang'anya.
26 Авимелех же сказал ему: не знаю, кто это сделал, и ты не сказал мне; я даже и не слыхал о том доныне.
Abimeleki akasema, “Sijui ni nani amefanya jambo hili. Hukuniambia mapema; na sijalisikia ila leo hii.”
27 И взял Авраам мелкого и крупного скота и дал Авимелеху, и они оба заключили союз.
Kwa hiyo Abraham akachukua kondoo na ng'ombe maksai akampatia Abimeleki, na wawili hawa wakafanya agano.
28 И поставил Авраам семь агниц из стада мелкого скота особо.
Kisha Abraham akatenga wanakondoo wa kike saba pekeyao.
29 Авимелех же сказал Аврааму: на что здесь сии семь агниц из стада овец, которых ты поставил особо?
Abimeleki akamwambia Abraham, “Nini maana ya hawa wanakondoo wa kike saba ambao umewatenga pekeyao?”
30 Авраам сказал: семь агниц сих возьми от руки моей, чтобы они были мне свидетельством, что я выкопал этот колодезь.
Akajibu, “Hawa wanakondoo wa kike saba utawapokea kutoka mkonono mwangu, ili kwamba uwe ushahidi kwangu, kuwa nichimba kisima hiki.”
31 Потому и назвал он сие место: Вирсавия, ибо тут оба они клялись
Kwa hiyo akaita mahali pale Beerisheba, kwa sababu mahali pale wote wawili wali apa kiapo.
32 и заключили союз в Вирсавии. И встал Авимелех и Фихол, военачальник его, и возвратились в землю Филистимскую.
Walifanya agano hapo Bersheba, kisha Abimeleki na Fikoli, amiri wa jeshi, wakarudi katika nchi ya Wafilisti.
33 И насадил Авраам при Вирсавии рощу и призвал там имя Господа, Бога вечного.
Abraham akapanda mti wa mkwaju katika Beerisheba. Na pale akamwabudu Yahwe, Mungu wa milele.
34 И жил Авраам в земле Филистимской, как странник, дни многие.
Abraham akasalia kuwa mgeni katika nchi ya Wafilisti kwa siku nyingi.

< Бытие 21 >