< 1-я Паралипоменон 6 >

1 Сыновья Левия: Гирсон, Кааф и Мерари.
Wana wa Levi walikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
2 Сыновья Каафа: Амрам, Ицгар, Хеврон и Узиил.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
3 Дети Амрама: Аарон, Моисей и Мариам. Сыновья Аарона: Надав, Авиуд, Елеазар и Ифамар.
Wana wa Amramu walikuwa Aruni, Musa, Miriamu. Wana wa Aruni walikuwa Nadabu, Abihu, Eleazari, na Ithamari.
4 Елеазар родил Финееса, Финеес родил Авишуя;
Eleazari akawa baba wa Finehasi, na Finehasi akawa baba wa Abishua.
5 Авишуй родил Буккия, Буккий родил Озию;
Abishua akawa baba wa Buki, na Buki akawa baba wa Uzi.
6 Озия родил Зерахию, Зерахия родил Мераиофа;
Uzi akawa baba wa Zerahia, na Zerahia akawa baba wa Meraioti.
7 Мераиоф родил Амарию, Амария родил Ахитува;
Meraioti akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
8 Ахитув родил Садока, Садок родил Ахимааса;
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Ahimazi.
9 Ахимаас родил Азарию, Азария родил Иоанана;
Ahimazi akawa baba wa Azaria, na Azaria akawa baba wa Yohanani.
10 Иоанан родил Азарию, - это тот, который был священником в храме, построенном Соломоном в Иерусалиме.
Yohanani akawa baba wa Azaria, aliye hudumu katika hekalu alilo lijenga Sulemani ndaniya Yerusalemu.
11 И родил Азария Амарию, Амария родил Ахитува;
Azaria akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
12 Ахитув родил Садока, Садок родил Селлума;
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Shalumu.
13 Селлум родил Хелкию, Хелкия родил Азарию;
Shalumu akawa baba wa Hilikia, na Hilikia akawa baba wa Azaria.
14 Азария родил Сераию, Сераия родил Иоседека.
Azaria akawa baba Seraia, na Seraia akawa baba wa Yehozadaki.
15 Иоседек пошел в плен, когда Господь переселил Иудеев и Иерусалимлян рукою Навуходоносора.
Yehozadaki akaenda matekani Yahweh alipo wapeleka utumwani Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Nebukadneza.
16 Итак сыновья Левия: Гирсон, Кааф и Мерари.
Wana wa Levi walikuwa Gerishomu, Kohathi, na Merari.
17 Вот имена сыновей Гирсоновых: Ливни и Шимей.
Wana wa Gerishomu walikuwa Libini na Shimei.
18 Сыновья Каафа: Амрам, Ицгар, Хеврон и Узиил.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
19 Сыновья Мерари: Махли и Муши. Вот потомки Левия по родам их.
Wana wa Merari walikuwa Mahili na Mushi. Hawa walikuwa koo za Walawi kwa familia za baba zao.
20 У Гирсона: Ливни, сын его; Иахав, сын его; Зимма, сын его;
Uzao wa Gerishomu ulianza na mwanae Libini. Mwana wa Libini alikuwa Jahathi. Mwanae alikuwa Zima.
21 Иоах, сын его; Иддо, сын его; Зерах, сын его; Иеафрай, сын его.
Mwanae alikuwa Yoa. Mwanae alikuwa alikuwa Ido. Mwanae alikuwa Zera. Mwanae alikuwa Yeatherai.
22 Сыновья Каафа: Аминадав, сын его; Корей, сын его; Асир, сын его;
Uzao wa Kohathi ulianza na mwanae Aminadabu. Mwanae alikuwa Kora. Mwanae alikuwa Asiri.
23 Елкана, сын его; Евиасаф, сын его; Асир, сын его;
Mwanae alikuwa Elikana. Mwanae alikuwa Ebiasa. Mwanae alikuwa Asiri.
24 Тахаф, сын его; Уриил, сын его; Узия, сын его; Саул, сын его.
Mwanae alikuwa Tahathi. Mwanae alikuwa Urieli. Mwanae alikuwa uzia. Mwanae alikuwa Shauli.
25 Сыновья Елканы: Амасай и Ахимоф.
Wana wa Elikana walikuwa Amasai, Ahimothi, na Elikana.
26 Елкана, сын его; Цофай, сын его; Нахаф, сын его;
Mwana wa huyu Elikana wa pili alikuwa Zofai. Mwanae alikuwa Nahathi.
27 Елиаф, сын его; Иерохам, сын его, Елкана, сын его; Самуил, сын его.
Mwanae alikuwa Eliabu. Mwanae alikuwa Yehoramu. Mwanae alikuwa Elikana.
28 Сыновья Самуила: первенец Иоиль, второй Авия.
Wana wa Samwali walikuwa mzaliwa wa kwanza, Yoeli, na Abija, wa pili.
29 Сыновья Мерари: Махли; Ливни, сын его; Шимей, сын его; Уза, сын его;
Mwana wa Merari alikuwa Mahili. Mwanae alikuwa Libini.
30 Шима, сын его; Хаггия, сын его; Асаия, сын его.
Mwanae alikuwa Shimei. Mwanae alikuwa Uza. Mwanae alikuwa Shimea. Mwanae alikuwa Hagia. Mwana alikuwa Asaia.
31 Вот те, которых Давид поставил начальниками над певцами в доме Господнем, со времени поставления в нем ковчега.
Haya ndio majina ya wanaume ambao Daudi waliwaeka kusimamia muziki katika nyumba ya Yahweh, baada ya sanduku kuja hapo.
32 Они служили певцами пред скиниею собрания, доколе Соломон не построил дома Господня в Иерусалиме. И они становились на службу свою по уставу своему.
Walitumika kwa kuimba mbele ya hema, hema la kukutania, mpaka Sulemani alipo jenga nyumba ya Yahweh ndani ya Yerusalemu. Walikamilisha wajibu wao kwa kadiri ya maelekezo waliopewa.
33 Вот те, которые становились с сыновьями своими: из сыновей Каафовых Еман певец, сын Иоиля, сын Самуила,
Hawa walitumika pamoja na wana wao. Katika makabila ya Wakohathi alitoka Hemani mwana muziki. Babu zake walikuwa hawa, kurudi nyuma ya wakati: Hemani alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Samweli.
34 сын Елканы, сын Иерохама, сын Елиила, сын Тоаха,
Samweli alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Yerohamu. Yerohamu alikuwa mwana wa Elieli. Elieli alikuwa mwana wa Toa.
35 сын Цуфа, сын Елканы, сын Махафа, сын Амасая,
Toa alikuwa mwana wa Zufi. Zufi alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Mahathi. Mahathi alikuwa mwana wa Amasai. Amasai alikuwa mwana wa Elikana.
36 сын Елканы, сын Иоиля, сын Азарии, сын Цефании,
Elikana alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Azaria. Azaria alikuwa mwana wa Zefania.
37 сын Тахафа, сын Асира, сын Авиасафа, сын Корея,
Zefania alikuwa mwana wa Tahathi. Tahathi alikuwa mwana wa Asiri. Asiri alikuwa mwana wa Ebiasa. Ebiasa alikuwa mwana wa Kora.
38 сын Ицгара, сын Каафа, сын Левия, сын Израиля;
Kora alikuwa mwana wa Izhari. Izhari alikuwa mwana wa Kohathi. Kohathi alikuwa mwana wa Levi. Levi alikuwa mwana wa Israeli.
39 и брат его Асаф, стоявший на правой стороне его, - Асаф, сын Берехии, сын Шимы,
Msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliye simama mkono wake wa kuume. Asafu alikuwa mwana Berekia. Berekia alikuwa mwana wa Shimea.
40 сын Михаила, сын Ваасеи, сын Малхии,
Shimea alikuwa mwana Mikaeli. Mikaeli alikuwa mwana wa Baaseia. Baaseia alikuwa mwana wa Malikiya.
41 сын Ефни, сын Зераха, сын Адаии,
Malikiya alikuwa mwana wa Ethini. Ethini alikuwa mwana wa Zera. Zera alikuwa mwana wa Adaia.
42 сын Ефана, сын Зиммы, сын Шимия,
Adaia alikuwa mwana wa Ethani. Ethani alikuwa mwana wa Zima. Zima alikuwa mwana wa Shimei.
43 сын Иахафа, сын Гирсона, сын Левия.
Shimei alikuwa mwana wa Yahathi. Yahathi alikuwa mwana wa Gerishomu. Gerishomu alikuwa mwana wa Levi.
44 А из сыновей Мерари, братьев их, на левой стороне: Ефан, сын Кишия, сын Авдия, сын Маллуха,
Upande wa mkono wa koshoto wa Hemani walikuwa wasaidizi wake wana wa Merari. Alikuwa Ethani mwana wa Kishi. Kishi alikuwa mwana wa Abdi. Abdi alikuwa mwana wa Maluki.
45 сын Хашавии, сын Амасии, сын Хелкии,
Maluki alikuwa mwana wa Hashabia. Hashabia alikuwa mwana wa Amazia. Amazia alikuwa mwana wa Hilikia.
46 сын Амция, сын Вания, сын Шемера,
Hilikia alikuwa mwana wa Amzi. Amzi alikuwa mwana wa Bani. Bani alikuwa mwana wa Shemeri.
47 сын Махлия, сын Мушия, сын Мерари, сын Левия.
Shemeri alikuwa mwana wa Mahili. Mahili alikuwa mwana wa Mushi. Mushi alikuwa mwana wa Merari. Merari alikuwa mwana wa Levi.
48 Братья их левиты определены на всякие службы при доме Божием;
Walawi, alipangiwa kufanya kazi zote za hema, nyumba ya Mungu.
49 Аарон же и сыновья его сожигали на жертвеннике всесожжения и на жертвеннике кадильном, и совершали всякое священнодействие во Святом Святых и для очищения Израиля во всем, как заповедал раб Божий Моисей.
Aruni na wana wake walitoa sadaka katika madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketeza; na sadaka katika madhabahu ya uvumba kwa kazi zote katika pa patakatifu. Hizi sadaka zilifanya maombezi kwa ajili ya Waisraeli, kwa kadiri ya yote ambayo Musa mtumishi wa Mungu aliwaamuru.
50 Вот сыновья Аарона: Елеазар, сын его; Финеес, сын его; Авиуд, сын его;
Uzao wa Aruni una kumbukwa kama ifuatavyo: Mwana wa Aruni alikuwa Eleazari. Mwana Eleazari alikuwa Finehasi. Mwana wa Finehasi alikuwa Abishua.
51 Буккий, сын его; Уззий, сын его; Зерахия, сын его;
Mwana wa Abishua alikuwa Buki. Mwana wa Buki alikuwa Uzi. Mwana wa Buki alikuwa Zerahia.
52 Мераиоф, сын его; Амария, сын его; Ахитув, сын его;
Mwana wa Zerahia alikuwa Meraiothi. Mwana wa Meraiothi alikuwa Amaria. Mwana wa Amaria alikuwa Ahitubi.
53 Садок, сын его; Ахимаас, сын его.
Mwana wa Ahitubi alikuwa Zadoki. Mwana wa Zadoki alikuwa Ahimazi.
54 И вот жилища их по селениям их в пределах их: сыновьям Аарона из племени Каафова, так как жребий выпал им,
Hizi ni sehemu ambazo wazao wa Aruni walipangiwa kuishi, wazao wa Aruni ambao walitoka katika koo za Wakohathi (maeneo ya kwanza yalikuwa yao).
55 дали Хеврон, в земле Иудиной, и предместья его вокруг его;
Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda na nchi ya malisho,
56 поля же сего города и села его отдали Халеву, сыну Иефонниину.
lakini maeneo ya mji na vijiji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
57 Сыновьям Аарона дали также города убежищ: Хеврон и Ливну с их предместьями, Иаттир и Ештемоа и предместья его,
Kwa wazao wa Aruni waliwapa: Hebroni ( mji wa makimblio), na Libina pamoja na nchi ya malisho, Yatiri, Eshitemoa pamoja na nchi ya malisho,
58 и Хилен и предместья его, Давир и предместья его,
Hileni pamoja na nchi ya malisho, na Debiri pamoja na nchi ya malisho.
59 и Ашан и предместья его, Вефсамис и предместья его,
Waliwapa uzao wa Aruni: Ashani pamoja na nchi ya malisho na Bethi Shemeshi pamoja na nchi ya malisho;
60 а от колена Вениаминова - Геву и предместья ее, и Аллемеф и предместья его, и Анафоф и предместья его: всех городов их в племенах их тринадцать городов.
na kutoka katika kabila la Benjamini walipewa Geba pamoja na nchi ya malisho, Alemethi pamoja na nchi ya malisho, na Anothothi na nchi ya malisho. Jumla ya miji yao ilikuwa kumi na tatu.
61 Остальным сыновьям Каафа, из семейств этого колена, дано по жребию десять городов из удела половины колена Манассиина.
Uzao mwengine wa Kohathi waliwapa kwa sehemu miji kumi kutoka kwa kabila la Manase.
62 Сыновьям Гирсона по племенам их, от колена Иссахарова, и от колена Асирова, и от колена Неффалимова, и от колена Манассиина в Васане, дано тринадцать городов.
Kwa uzao wa Gerishomu kwa koo zao tofauti walipewa miji kumi na tatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri, Naftali, na nusu ya kabila la Manase huko Bashani.
63 Сыновьям Мерари по племенам их, от колена Рувимова, и от колена Гадова, и от колена Завулонова, дано по жребию двенадцать городов.
Kwa uzao wa Merari walipewa miji kumi, kulingana na koo zao, kutoka kwa makabila ya Rubeni, Gadi, na Zebuluni.
64 Так дали сыны Израилевы левитам города и предместья их.
Hivyo watu wa Israeli walitoa hii miji pamoja na nchi za malisho kwa Walawi.
65 Дали они по жребию от колена сыновей Иудиных, и от колена сыновей Симеоновых, и от колена сыновей Вениаминовых те города, которые они назвали по именам.
Walitoa kwa sehemu miji iliyo tajwa awali kutoka katika kabila la Yuda, Simeoni, na Benjamini.
66 Некоторым же племенам сыновей Каафовых даны были города от колена Ефремова.
Kwa baadhi ya koo za Wakohathi walitoa miji kutoka kwa kabila la Efraimu.
67 И дали им города убежищ: Сихем и предместья его на горе Ефремовой, и Гезер и предместья его,
Waliwapa: Shekemu ( mji wa makimbilio) pamoja na nchi ya malisho katika milima ya Efraimu, Gezeri na nchi ya malisho,
68 и Иокмеам и предместья его, и Беф-Орон и предместья его,
Jokimeamu pamoja na nchi ya malisho, Bethi Horoni pamoja na nchi ya malisho,
69 и Аиалон и предместья его, и Гаф-Риммон и предместья его;
Aiyaloni pamoja na nchi ya malisho, na Gathi Rimoni pamoja na nchi ya malisho.
70 от половины колена Манассиина - Анер и предместья его, Билеам и предместья его. Это поколению остальных сыновей Каафовых.
Nusu ya kabila la Manase waliwapa Wakohathi: Aneri pamoja na nchi ya malisho na Bileamu pamoja na nchi ya malisho. Hizi zikawa mali za koo za Wakohathi.
71 Сыновьям Гирсона от племени полуколена Манассиина дали Голан в Васане и предместья его, и Аштароф и предместья его.
Kwa uzao wa Gerishomu kutoka koo za nusu ya kabila la Manase, waliwapa: Golani huko Baashani na nchi ya malisho na Ashitarothi pamoja na nchi ya malisho.
72 От колена Иссахарова - Кедес и предместья его, Давраф и предместья его,
Kabila la Isakari liliwapa uzao wa Gerishomu: Kedeshi pamoja na nchi ya malisho, Dabera pamoja na nchi ya malisho,
73 и Рамоф и предместья его, и Анем и предместья его;
Ramothi pamoja na nchi ya malisho, na Anemu pamoja na nchi ya malisho.
74 от колена Асирова - Машал и предместья его, и Авдон и предместья его,
Isakari alipokea kutoka kwa kabila la Asheri: Mashali pamoja na nchi ya malisho, Abdoni pamoja na nchi ya malisho,
75 и Хукок и предместья его, и Рехов и предместья его;
Hukoki pamoja na nchi ya malisho, na Rehobu pamoja na nchi ya malisho.
76 от колена Неффалимова - Кедес в Галилее и предместья его, и Хаммон и предместья его, и Кириафаим и предместья его.
Walipokea kutoka kabila la Naftali: Kedeshi iliyo Galileya pamoja na nchi ya malisho, Hamoni pamoja na nchi ya malisho, na Kiriathaimu pamoja na nchi ya malisho.
77 А прочим сыновьям Мерариным - от колена Завулонова Риммон и предместья его, Фавор и предместья его.
Kwa Walawi wengine, uzao wa Merari, walipewa kutoka kabila la Zebuluni: Rimono pamoja na nchi ya malisho na Tabori pamoja na nchi ya malisho.
78 По ту сторону Иордана, против Иерихона, на восток от Иордана, от колена Рувимова дали Восор в пустыне и предместья его, и Иаацу и предместья ее,
Kwa wao pia walipewa, upande wa pili wa Yordani huko Yeriko, kwa upande wa mashariki mwa mto: Bezeri katika jangwa pamoja na nchi ya malisho, Yahzahi pamoja na nchi ya malisho,
79 и Кедемоф и предместья его, и Мефааф и предместья его;
Kedemothi pamoka na nchi ya malisho, ma Mefathi pamoja na nchi ya malisho. Hizi zilitolewa kutoka kabila la Rubeni.
80 от колена Гадова - Рамоф в Галааде и предместья его, и Маханаим и предместья его,
Walawi walipokea kutoka kabila la Gadi: Ramothi ya Gileadi pamoja na nchi ya malisho, Mahanaimu pamoja na nchi ya malisho,
81 и Есевон и предместья его, и Иазер и предместья его.
Heshiboni pamoja na nchi ya malisho, na Yazeri pamoja na nchi ya malisho.

< 1-я Паралипоменон 6 >