< 1-я Паралипоменон 27 >

1 Вот сыны Израилевы по числу их, главы семейств, тысяченачальники и стоначальники и управители, которые по отделениям служили царю во всех делах, приходя и отходя каждый месяц, во все месяцы года. В каждом отделении было их по двадцать четыре тысячи.
Hii ndiyo orodha ya Waisraeli: viongozi wa jamaa, majemadari wa maelfu, majemadari wa mamia na maafisa wao, waliomtumikia mfalme kwa lolote lililohusu vikosi vya jeshi vilivyokuwa zamu mwezi baada ya mwezi katika mwaka mzima. Kila kikosi kimoja kilikuwa na watu 24,000.
2 Над первым отделением, для первого месяца, начальствовал Иашовам, сын Завдиила; в его отделении было двадцать четыре тысячи;
Msimamizi wa kikosi cha kwanza kwa mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Kulikuwa na watu 24,000 katika kikosi chake.
3 он был из сынов Фареса, главный над всеми военачальниками в первый месяц.
Yeye alikuwa mzao wa Peresi, na mkuu wa maafisa wote wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
4 Над отделением второго месяца был Додай Ахохиянин; в отделении его был и князь Миклоф, и в его отделении было двадцать четыре тысячи.
Msimamizi wa kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai Mwahohi. Miklothi ndiye alikuwa kiongozi wa kikosi chake. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
5 Третий главный военачальник, для третьего месяца, Ванея, сын Иодая, священника, и в его отделении было двадцать четыре тысячи:
Jemadari wa kikosi cha tatu kwa mwezi wa tatu alikuwa Benaya mwana wa kuhani Yehoyada. Ndiye alikuwa mkuu wa kikosi chake kilichokuwa na watu 24,000.
6 этот Ванея - один из тридцати храбрых и начальник над ними, и в его отделе находился Аммизавад, сын его.
Huyu ndiye yule Benaya aliyekuwa shujaa miongoni mwa wale Thelathini na ndiye alikuwa juu yao hao Thelathini. Mwanawe Amizabadi ndiye alikuwa mkuu katika kikosi chake.
7 Четвертый, для четвертого месяца, был Асаил, брат Иоава, и по нем Завадия, сын его, и в его отделении двадцать четыре тысячи.
Jemadari wa nne kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli nduguye Yoabu, mwanawe Zebadia ndiye aliingia mahali pake kwenye uongozi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
8 Пятый, для пятого месяца, князь Шамгуф Израхитянин, и в его отделении двадцать четыре тысячи.
Jemadari wa kikosi cha tano kwa mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi Mwizrahi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
9 Шестой, для шестого месяца, Ира, сын Иккеша, Фекоянин, и в его отделении двадцать четыре тысячи.
Jemadari wa kikosi cha sita kwa mwezi wa sita alikuwa Ira, mwana wa Ikeshi Mtekoa. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
10 Седьмой, для седьмого месяца, Хелец Пелонитянин, из сынов Ефремовых, и в его отделении двадцать четыре тысячи.
Jemadari wa kikosi cha saba kwa mwezi wa saba alikuwa Helesi Mpeloni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
11 Восьмой, для восьмого месяца, Совохай Хушатянин, из племени Зары, и в его отделении двадцать четыре тысячи.
Jemadari wa nane kwa mwezi wa nane, alikuwa Sibekai Mhushathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
12 Девятый, для девятого месяца, Авиезер Анафофянин, из сыновей Вениаминовых, и в его отделении двадцать четыре тысячи.
Jemadari wa tisa kwa mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri Mwanathothi wa Wabenyamini. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
13 Десятый, для десятого месяца, Магарай Нетофафянин, из племени Зары, и в его отделении двадцать четыре тысячи.
Jemadari wa kumi kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai Mnetofathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
14 Одиннадцатый, для одиннадцатого месяца, Ванея Пирафонянин, из сынов Ефремовых, и в его отделении двадцать четыре тысячи.
Jemadari wa kumi na moja kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya Mpirathoni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
15 Двенадцатый, для двенадцатого месяца, Хелдай Нетофафянин, из потомков Гофониила, и в его отделении двадцать четыре тысячи.
Jemadari wa kumi na mbili kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai Mnetofathi kutoka jamaa ya Othnieli. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
16 А над коленами Израилевыми, - у Рувимлян главным начальником был Елиезер, сын Зихри; у Симеона - Сафатия, сын Маахи;
Maafisa waliokuwa wanaoongoza makabila ya Israeli walikuwa: Kwa Wareubeni: Eliezeri mwana wa Zikri; kwa Wasimeoni: Shefatia mwana wa Maaka;
17 у Левия - Хашавия, сын Кемуила; у Аарона - Садок;
kwa Walawi: Hashabia mwana wa Kemueli; kwa Aroni: Sadoki;
18 у Иуды - Елиав, из братьев Давида; у Иссахара - Омри, сын Михаила;
kwa Yuda: Elihu, nduguye Daudi; kwa Waisakari: Omri mwana wa Mikaeli;
19 у Завулона - Ишмаия, сын Овадии; у Неффалима - Иеримоф, сын Азриила;
kwa Wazabuloni: Ishmaya mwana wa Obadia; kwa Wanaftali: Yeremothi mwana wa Azrieli;
20 у сыновей Ефремовых - Осия, сын Азазии; у полуколена Манассиина - Иоиль, сын Федаии;
kwa Waefraimu: Hoshea mwana wa Azazia; kwa nusu ya kabila la Manase: Yoeli mwana wa Pedaya;
21 у полуколена Манассии в Галааде - Иддо, сын Захарии; у Вениамина - Иаасиил, сын Авенира;
kwa nusu nyingine ya kabila la Manase huko Gileadi: Ido mwana wa Zekaria; kwa Wabenyamini: Yaasieli mwana wa Abneri;
22 у Дана - Азариил, сын Иерохама. Вот вожди колен Израилевых.
kwa Wadani: Azareli mwana wa Yerohamu. Hao ndio waliokuwa maafisa wa makabila ya Israeli.
23 Давид не делал счисления тех, которые были от двадцати лет и ниже, потому что Господь сказал, что Он умножит Израиля, как звезды небесные.
Daudi hakuwahesabu watu waliokuwa chini ya miaka ishirini, kwa sababu Bwana alikuwa ameahidi kuwafanya Israeli kuwa wengi kama nyota za angani.
24 Иоав, сын Саруи, начал делать счисление, но не кончил. И был за это гнев Божий на Израиля, и не вошло то счисление в летопись царя Давида.
Yoabu mwana wa Seruya alianza kuwahesabu watu lakini hakumaliza. Kwa sababu ya kuwahesabu watu, hasira ya Mungu iliwaka juu ya Israeli, nayo hiyo hesabu yao haikuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu za Mfalme Daudi.
25 Над сокровищами царскими был Азмавеф, сын Адиилов, а над запасами в поле, в городах, и в селах и в башнях - Ионафан, сын Уззии;
Azmawethi mwana wa Adieli ndiye alikuwa msimamizi wa hazina za mfalme. Msimamizi wa hazina katika mashamba, miji, vijiji na kwenye ngome alikuwa Yonathani mwana wa Uzia.
26 над занимающимися полевыми работами, земледелием - Езрий, сын Хелува;
Ezri mwana wa Kelubu alikuwa msimamizi wa wafanyakazi waliolima katika mashamba.
27 над виноградниками - Шимей из Рамы, а над запасами вина в виноградниках Завдий из Шефама;
Shimei Mramathi alikuwa msimamizi wa mashamba ya mizabibu. Zabdi Mshifmi alikuwa msimamizi wa zabibu, utengenezaji na uhifadhi wa divai katika mapipa makubwa.
28 над маслинами и смоковницами в долине - Баал-Ханан Гедеритянин, а над запасами деревянного масла - Иоас;
Baal-Hanani Mgederi ndiye alikuwa mwangalizi wa mashamba ya mfalme ya mizeituni na mikuyu katika tambarare za vilima vya magharibi. Yoashi alikuwa msimamizi wa ghala za mafuta ya zeituni.
29 над крупным скотом, пасущимся в Шароне - Шитрай Шаронянин, а над скотом в долинах - Шафат, сын Адлая;
Shitrai Msharoni alikuwa msimamizi wa makundi ya ngʼombe waliojilisha huko Sharoni. Shafati mwana wa Adlai alikuwa msimamizi wa yale makundi ya ngʼombe yaliyokuwa makondeni.
30 над верблюдами - Овил Исмаильтянин; над ослицами - Иехдия Меронифянин;
Obili Mwishmaeli alikuwa msimamizi wa ngamia. Yedeya Mmeronothi alikuwa msimamizi wa punda.
31 над мелким скотом - Иазиз Агаритянин. Все эти были начальниками над имением, которое было у царя Давида.
Yazizi Mhagri alikuwa msimamizi wa makundi ya kondoo na mbuzi. Hawa wote ndio waliokuwa maafisa wasimamizi wa mali alizokuwa nazo Mfalme Daudi.
32 Ионафан, дядя Давидов, был советником, человек умный и писец; Иехиил, сын Хахмониев, был при сыновьях царя;
Yonathani mjomba wa Daudi alikuwa mshauri, mtu mwenye ufahamu mkubwa na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakmoni alikuwa akiwahudumia wana wa mfalme.
33 Ахитофел был советником царя; Хусий Архитянин - другом царя;
Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme. Hushai Mwariki alikuwa rafiki wa mfalme.
34 после же Ахитофела Иодай, сын Ванеи, и Авиафар, а Иоав был военачальником у царя.
Baada ya Ahithofeli, Yehoyada mwana wa Benaya aliingia mahali pake kama mshauri wa mfalme pamoja na Abiathari. Yoabu alikuwa ndiye jemadari wa majeshi ya mfalme.

< 1-я Паралипоменон 27 >