< 1-я Паралипоменон 15 >

1 И построил он себе домы в городе Давидовом, и приготовил место для ковчега Божия, и устроил для него скинию.
Baada ya Daudi kujijengea nyumba zake katika Mji wa Daudi, akatengeneza sehemu kwa ajili ya Sanduku la Mungu, kisha akasimamisha hema kwa ajili yake.
2 Тогда сказал Давид: никто не должен носить ковчега Божия, кроме левитов, потому что их избрал Господь на то, чтобы носить ковчег Божий и служить Ему во веки.
Kisha Daudi akasema, “Hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kulibeba Sanduku la Mungu isipokuwa Walawi peke yao, kwa sababu Bwana aliwachagua kulibeba Sanduku la Bwana na kuhudumu mbele zake milele.”
3 И собрал Давид всех Израильтян в Иерусалим, чтобы внести ковчег Господень на место его, которое он для него приготовил.
Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu ili kulipandisha Sanduku la Bwana na kulileta hadi kwenye sehemu aliyokuwa ametengeneza kwa ajili yake.
4 И созвал Давид сыновей Аароновых и левитов:
Kisha Daudi akawakusanya pamoja wazao wa Aroni na Walawi:
5 из сыновей Каафовых, Уриила начальника и братьев его - сто двадцать человек;
Kutoka wazao wa Kohathi, Urieli kiongozi na ndugu zake 120,
6 из сыновей Мерариных, Асаию начальника и братьев его - двести двадцать человек;
Kutoka wazao wa Merari, Asaya kiongozi na ndugu zake 220.
7 из сыновей Гирсоновых, Иоиля начальника и братьев его - сто тридцать человек;
Kutoka wazao wa Gershoni, Yoeli kiongozi na ndugu zake 130.
8 из сыновей Елисафановых, Шемаию начальника и братьев его - двести;
Kutoka wazao wa Elisafani, Shemaya kiongozi na ndugu zake 200.
9 из сыновей Хевроновых, Елиела начальника и братьев его - восемьдесят;
Kutoka wazao wa Hebroni, Elieli kiongozi na ndugu zake 80.
10 из сыновей Уззииловых, Аминадава начальника и братьев его - сто двенадцать.
Kutoka wazao wa Uzieli, Aminadabu kiongozi na ndugu zake 112.
11 И призвал Давид священников: Садока и Авиафара, и левитов: Уриила, Асаию, Иоиля, Шемаию, Елиела и Аминадава,
Kisha Daudi akawaita makuhani Sadoki na Abiathari, pamoja na Walawi Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli na Aminadabu.
12 и сказал им: вы, начальники родов левитских, освятитесь сами и братья ваши, и принесите ковчег Господа Бога Израилева на место, которое я приготовил для него;
Akawaambia, “Ninyi ndio viongozi wa jamaa za Walawi. Ninyi pamoja na Walawi wenzenu inawapasa mjitakase na kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli hadi mahali ambapo nimetengeneza kwa ajili yake.
13 ибо как прежде не вы это делали, то Господь Бог наш поразил нас за то, что мы не взыскали Его, как должно.
Ilikuwa ni kwa sababu hii, ninyi Walawi, hamkulipandisha Sanduku la Bwana mara ya kwanza, hata ikasababisha Bwana Mungu wetu kuwaka hasira dhidi yetu. Hatukumuuliza jinsi ya kufanya ili tupate kulileta jinsi alivyoagiza.”
14 И освятились священники и левиты для того, чтобы нести ковчег Господа, Бога Израилева.
Kwa hiyo makuhani pamoja na Walawi wakajitakasa ili kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli.
15 И понесли сыновья левитов ковчег Божий, как заповедал Моисей по слову Господа, на плечах, на шестах.
Nao Walawi wakalichukua Sanduku la Mungu mabegani mwao wakitumia mipiko, kama vile Mose alivyoamuru sawasawa na neno la Bwana.
16 И приказал Давид начальникам левитов поставить братьев своих певцов с музыкальными орудиями, с псалтирями и цитрами и кимвалами, чтобы они громко возвещали глас радования.
Daudi akawaambia viongozi wa Walawi kuwaweka ndugu zao waimbaji ili waimbe nyimbo za shangwe, wakiwa na vyombo vya uimbaji: zeze, vinubi na matoazi.
17 И поставили левиты Емана, сына Иоилева, и из братьев его, Асафа, сына Верехиина, а из сыновей Мерариных, братьев их, Ефана, сына Кушаии;
Basi Walawi wakawaweka Hemani mwana wa Yoeli; kutoka miongoni mwa ndugu zake, Asafu mwana wa Berekia; kutoka miongoni mwa ndugu zao Wamerari, Ethani mwana wa Kushaiya;
18 и с ними братьев их второстепенных: Захарию, Бена, Иаазиила, Шемирамофа, Иехиила, Унния, Елиава, Ванею, Маасея, Маттафию, Елифлеуя, Микнея и Овед-Едома и Иеиела, привратников.
hawa ndio waliochaguliwa kuwa wasaidizi wao: Zekaria, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaya, Maaseya, Matithia, Elifelehu, Mikneya, pamoja na mabawabu Obed-Edomu na Yehieli.
19 Еман, Асаф и Ефан играли громко на медных кимвалах,
Waimbaji Hemani, Asafu na Ethani walichaguliwa kupiga matoazi ya shaba;
20 а Захария, Азиил, Шемирамоф, Иехиил, Унний, Елиав, Маасей и Ванея - на псалтирях, тонким голосом.
Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Maaseya na Benaya walikuwa wapiga zeze kufuatana na sauti ya alamothi,
21 Маттафия же, Елифлеуй, Микней, Овед-Едом, Иеиел и Азазия - на цитрах, чтобы делать начало.
na Matithia, Elifelehu, Mikneya, Obed-Edomu, Yehieli na Azazia walikuwa wapiga vinubi, wakiongozwa kwa kufuata sauti ya sheminithi.
22 А Хенания, начальник левитов, был учитель пения, потому что был искусен в нем.
Kenania kiongozi wa Walawi alikuwa msimamizi wa uimbaji; huu ndio uliokuwa wajibu wake kwa sababu alikuwa stadi katika hilo.
23 Верехия и Елкана были придверниками у ковчега.
Berekia na Elikana walikuwa mabawabu kwa ajili ya Sanduku.
24 Шевания, Иосафат, Нафанаил, Амасай, Захария, Ванея и Елиезер, священники, трубили трубами пред ковчегом Божиим. Овед-Едом и Иехия были придверниками у ковчега.
Shebania, Yoshafati, Nethaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, makuhani, walikuwa wapiga tarumbeta mbele ya Sanduku la Mungu. Obed-Edomu na Yehiya waliwekwa pia kuwa mabawabu wa Sanduku.
25 Так Давид и старейшины Израилевы и тысяченачальники пошли перенести ковчег завета Господня из дома Овед-Едомова с веселием.
Basi Daudi pamoja na wazee wa Israeli na majemadari wa vikosi vya elfu wakaenda ili kulipandisha Sanduku la Agano la Bwana kutoka nyumba ya Obed-Edomu kwa shangwe.
26 И когда Бог помог левитам, несшим ковчег завета Господня, тогда закололи в жертву семь тельцов и семь овнов.
Kwa sababu Mungu alikuwa amewasaidia Walawi waliokuwa wanalichukua Sanduku la Agano la Bwana, mafahali saba na kondoo dume saba walitolewa dhabihu.
27 Давид был одет в виссонную одежду, а также и все левиты, несшие ковчег, и певцы, и Хенания начальник музыкантов и певцов. На Давиде же был еще льняной ефод.
Basi Daudi alikuwa amevaa joho la kitani safi, kama walivyokuwa wamevaa Walawi wote waliokuwa wanalichukua lile Sanduku, waimbaji nao walivaa vivyo hivyo, pamoja na Kenania aliyekuwa anaongoza nyimbo za waimbaji. Daudi alivaa pia kisibau cha kitani safi.
28 Так весь Израиль вносил ковчег завета Господня с восклицанием, при звуке рога и труб и кимвалов, играя на псалтирях и цитрах.
Hivyo Israeli wote wakalipandisha Sanduku la Agano la Bwana kwa shangwe, wakipiga pembe za kondoo dume, tarumbeta, matoazi, wakipiga zeze na vinubi.
29 Когда ковчег завета Господня входил в город Давидов, Мелхола, дочь Саулова, смотрела в окно и, увидев царя Давида, скачущего и веселящегося, уничижила его в сердце своем.
Sanduku la Agano la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea, akamdharau moyoni mwake.

< 1-я Паралипоменон 15 >