< 1-я Паралипоменон 11 >

1 И собрались все Израильтяне к Давиду в Хеврон и сказали: вот, мы кость твоя и плоть твоя;
Israeli yote walimjia Daudi kwa pamoja huko Hebroni wakamwambia, “Sisi ni nyama yako na damu yako.
2 и вчера, и третьего дня, когда еще Саул был царем, ты выводил и вводил Израиля, и Господь Бог твой сказал тебе: “ты будешь пасти народ Мой, Израиля, и ты будешь вождем народа Моего Израиля”.
Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani, naye Bwana Mungu wako alikuambia, ‘Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’”
3 И пришли все старейшины Израилевы к царю в Хеврон, и заключил с ними Давид завет в Хевроне пред лицем Господним; и они помазали Давида в царя над Израилем, по слову Господню, чрез Самуила.
Wazee wote wa Israeli walipokuwa wamewasili kwa Mfalme Daudi huko Hebroni, alifanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Bwana, nao wakamtia Daudi mafuta awe mfalme wa Israeli, sawasawa na Bwana alivyoahidi kupitia kwa Samweli.
4 И пошел Давид и весь Израиль к Иерусалиму, то есть к Иевусу. А там были Иевусеи, жители той земли.
Daudi na Waisraeli wote wakaenda Yerusalemu (ndio Yebusi). Nao Wayebusi walioishi humo
5 И сказали жители Иевуса Давиду: не войдешь сюда. Но Давид взял крепость Сион; это город Давидов.
wakamwambia Daudi, “Wewe hutaingia humu.” Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.
6 И сказал Давид: кто прежде всех поразит Иевусеев, тот будет главою и военачальником. И взошел прежде всех Иоав, сын Саруи, и сделался главою.
Daudi alikuwa amesema, “Yeyote aongozaye mashambulizi dhidi ya Wayebusi, atakuwa jemadari mkuu.” Yoabu mwana wa Seruya akawa wa kwanza kukwea, naye akawa mkuu.
7 Давид жил в той крепости, потому и называли ее городом Давидовым.
Daudi akafanya makao yake kwenye ngome, hivyo ukaitwa Mji wa Daudi.
8 И он обстроил город кругом, начиная от Милло, всю окружность, а Иоав возобновил остальные части города.
Akajenga mji pande zote, kuanzia kwenye mito hadi kwenye ukuta kuzunguka, wakati huo huo Yoabu akajenga sehemu zingine zilizobaki za Yerusalemu.
9 И преуспевал Давид, и возвышался более и более, и Господь Саваоф был с ним.
Daudi akazidi kuwa na nguvu zaidi na zaidi, kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote alikuwa pamoja naye.
10 Вот главные из сильных у Давида, которые крепко подвизались с ним в царстве его, вместе со всем Израилем, чтобы воцарить его, по слову Господню, над Израилем,
Hawa ndio waliokuwa wakuu wa mashujaa wa Daudi: wao pamoja na Israeli wote wakauimarisha ufalme wake ili kuenea katika nchi yote, kama Bwana alivyoahidi.
11 и вот число храбрых, которые были у Давида: Иесваал, сын Ахамани, главный из тридцати. Он поднял копье свое на триста человек и поразил их в один раз.
Hii ndio orodha ya mashujaa wa Daudi: Yashobeamu, Mhakmoni, alikuwa mkuu wa maafisa; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua katika pambano moja.
12 По нем Елеазар, сын Додо Ахохиянина, из трех храбрых:
Aliyefuata alikuwa Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu.
13 он был с Давидом в Фасдамиме, куда Филистимляне собрались на войну. Там часть поля была засеяна ячменем, и народ побежал от Филистимлян;
Huyo alikuwa pamoja na Daudi huko Pas-Damimu, wakati Wafilisti walikusanyika huko kwa ajili ya vita. Huko ambapo kulikuwa na shamba lililokuwa limejaa shayiri, vikosi vya Israeli vikawakimbia Wafilisti.
14 но они стали среди поля, сберегли его и поразили Филистимлян. И даровал Господь спасение великое!
Lakini Eleazari na Daudi wakasimama imara katikati ya lile shamba, nao wakalishindania na wakawaua Wafilisti. Naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
15 Трое сих главных из тридцати вождей взошли на скалу к Давиду, в пещеру Одоллам, когда стан Филистимлян был расположен в долине Рефаимов.
Wakuu watatu miongoni mwa wale thelathini, walimwendea Daudi katika mwamba huko kwenye pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
16 Давид тогда был в укрепленном месте, а охранное войско Филистимлян было тогда в Вифлееме.
Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
17 И сильно захотелось пить Давиду, и он сказал: кто напоит меня водою из колодезя Вифлеемского, что у ворот?
Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilichoko karibu na lango la Bethlehemu!”
18 Тогда эти трое пробились сквозь стан Филистимский и почерпнули воды из колодезя Вифлеемского, что у ворот, и взяли, и принесли Давиду. Но Давид не захотел пить ее и вылил ее во славу Господа,
Kwa hivyo wale watatu, wakapita katikati ya safu za Wafilisti, wakachota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
19 и сказал: сохрани меня Господь, чтоб я сделал это! Стану ли я пить кровь мужей сих, полагавших души свои! Ибо с опасностью собственной жизни они принесли воду. И не захотел пить ее. Вот что сделали трое этих храбрых.
Akasema, “Mungu apishie mbali kwamba nifanye hivi! Je kweli, niinywe damu ya watu hawa waliohatarisha maisha yao?” Kwa sababu walihatarisha maisha yao kuyaleta yale maji, Daudi hakukubali kuyanywa. Huo ndio uliokuwa ujasiri wa wale mashujaa watatu.
20 И Авесса, брат Иоава, был главным из трех: он убил копьем своим триста человек, и был в славе у тех троих.
Abishai, ndugu yake Yoabu ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
21 Из трех он был знатнейшим и был начальником; но с теми тремя не равнялся.
Alitunukiwa heshima maradufu ya wale Watatu, akawa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
22 Ванея, сын Иодая, мужа храброго, великий по делам, из Кавцеила: он поразил двух сыновей Ариила Моавитского; он же сошел и убил льва во рву, в снежное время;
Benaya, mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
23 он же убил Египтянина, человека ростом в пять локтей: в руке Египтянина было копье, как навой у ткачей, а он подошел к нему с палкою и, вырвав копье из руки Египтянина, убил его его же копьем:
Alimuua Mmisri aliyekuwa na urefu kama dhiraa tano. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki kama mti wa mfumaji mkononi mwake, Benaya alimwendea na rungu. Akamnyangʼanya Mmisri mkuki wake na kumuua nao.
24 вот что сделал Ванея, сын Иодая. И он был в славе у тех троих храбрых;
Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
25 он был знатнее тридцати, но с тремя не равнялся, и Давид поставил его ближайшим исполнителем своих приказаний.
Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu: Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
26 А главные из воинов: Асаил, брат Иоава; Елханан, сын Додо, из Вифлеема;
Wale watu mashujaa walikuwa: Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,
27 Шамма Гародитянин; Херец Пелонитянин;
Shamothi Mharori, Helesi Mpeloni,
28 Ира, сын Икеша, Фекоитянин; Евиезер Анафофянин;
Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa, Abiezeri kutoka Anathothi,
29 Сивхай Хушатянин; Илай Ахохиянин;
Sibekai Mhushathi, Ilai Mwahohi,
30 Магарай Нетофафянин; Хелед, сын Вааны, Нетофафянин;
Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi,
31 Иттай, сын Рибая, из Гивы Вениаминовой; Ванея Пирафонянин;
Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini, Benaya Mpirathoni,
32 Хурай из Нагале-Гааша; Авиел из Аравы;
Hurai kutoka mabonde ya Gaashi, Abieli Mwaribathi,
33 Азмавеф Бахарумиянин; Елияхба Шаалбонянин.
Azmawethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni,
34 Сыновья Гашема Гизонитянина: Ионафан, сын Шаге, Гараритянин;
wana wa Hashemu Mgiloni, Yonathani mwana wa Shagee Mharari,
35 Ахиам, сын Сахара, Гараритянин; Елифал, сын Уры;
Ahiamu mwana wa Sakari Mharari, Elifale mwana wa Uru,
36 Хефер из Махеры; Ахиа Пелонитянин;
Heferi Mmekerathi, Ahiya Mpeloni,
37 Хецрой Кармилитянин; Наарай, сын Езбая;
Hezro Mkarmeli, Naarai mwana wa Ezbai,
38 Иоиль, брат Нафана; Мивхар, сын Гагрия;
Yoeli nduguye Nathani, Mibhari mwana wa Hagri,
39 Целек Аммонитянин; Нахарай Берофянин, оруженосец Иоава, сына Саруи;
Seleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,
40 Ира Ифриянин; Гареб Ифриянин;
Ira Mwithiri, Garebu Mwithiri,
41 Урия Хеттеянин; Завад, сын Ахлая;
Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Alai,
42 Адина, сын Шизы, Рувимлянин, Глава Рувимлян, и у него было тридцать;
Adina mwana wa Shiza Mreubeni, ambaye alikuwa mkuu wa Wareubeni, akiwa pamoja na watu thelathini,
43 Ханан, сын Маахи; Иосафат Мифниянин;
Hanani mwana wa Maaka, Yoshafati Mmithni,
44 Уззия Аштерофянин; Шама и Иеиел, сыновья Хофама Ароерянина;
Uzia Mwashterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Mwaroeri,
45 Иедиаел, сын Шимрия, и Иоха, брат его, Фициянин;
Yediaeli mwana wa Shimri, nduguye Yoha Mtizi,
46 Елиел из Махавима, и Иеривай и Иошавия, сыновья Елнаама, и Ифма Моавитянин;
Elieli Mmahawi, Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu, Ithma Mmoabu,
47 Елиел, Овед и Иасиел из Мецоваи.
Elieli, na Obedi na Yaasieli Mmesobai.

< 1-я Паралипоменон 11 >