< Lucas 4 >

1 Jesus, cheio do Espírito Santo, voltou do rio Jordão e foi guiado, pelo mesmo Espírito, no deserto.
Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
2 Lá ele foi tentado pelo diabo durante quarenta dias. Ele não comeu nada durante todo esse tempo. Então, no fim desse período, ele estava faminto.
kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
3 O diabo lhe disse: “Se você é o Filho de Deus, mande que esta pedra vire pão.”
Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
4 Jesus respondeu: “Está escrito nas Sagradas Escrituras: ‘O homem não viverá só de pão.’”
Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
5 O diabo levou Jesus para um lugar alto e, em uma visão rápida, lhe mostrou todos os reinos do mundo.
Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
6 Então, o diabo disse a Jesus: “Eu lhe darei toda a autoridade sobre eles e toda a sua glória. Essa autoridade foi dada a mim e eu posso dá-la a quem eu quiser.
Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
7 Ajoelhe-se e me adore e poderá ter isso tudo.”
Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
8 Jesus respondeu: “Está escrito nas Sagradas Escrituras: ‘Adore o Senhor, seu Deus, e sirva apenas a ele.’”
Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
9 O diabo levou Jesus para Jerusalém e o deixou na parte mais alta do Templo e disse: “Se você é o Filho de Deus, então, pule.
Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
10 Pois está escrito nas Sagradas Escrituras: ‘Ele ordenará que os seus anjos cuidem de você,
Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
11 segurando-o para protegê-lo até mesmo de tropeçar em uma pedra.’”
na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
12 Jesus respondeu: “Está escrito nas Sagradas Escrituras: ‘Não teste o Senhor, seu Deus.’”
Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
13 Quando o diabo acabou de tentar Jesus de todas as formas, ele desistiu e preferiu esperar por outra oportunidade.
Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
14 Jesus voltou para a Galileia, tomado pelo poder do Espírito. As notícias sobre Jesus se espalharam por todos os lugares.
Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
15 Jesus ensinou nas sinagogas, e todos o elogiavam.
Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
16 Ele chegou em Nazaré, onde havia crescido. No sábado, foi para a sinagoga, como de costume.
Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
17 Lá, eles deram o livro do profeta Isaías para que ele lesse. Jesus abriu o livro e encontrou o lugar em que está escrito:
Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
18 “O Espírito do Senhor está sobre mim, pois ele me escolheu para anunciar as boas novas aos necessitados. Ele me enviou para anunciar que os prisioneiros serão soltos, que os cegos verão, que os oprimidos serão libertados
“Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
19 e para declarar o momento em que o Senhor nos salvará.”
kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
20 Ele fechou o livro e o devolveu ao ajudante da sinagoga. Depois, ele se sentou. Todas as pessoas que estavam na sinagoga olhavam fixamente para Jesus.
Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
21 Ele lhes disse: “Este trecho das Sagradas Escrituras, que vocês acabaram de ouvir, se cumpriu hoje!”
Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
22 Todos que estavam lá o elogiavam. Eles estavam maravilhados com a sua forma agradável de falar. As pessoas pensaram: “Ele não é o filho de José?”
Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
23 Jesus respondeu: “Eu tenho certeza de que vocês repetirão esse provérbio para mim: ‘Médico, cure a si mesmo!’ E irão perguntar: ‘Por que você não faz aqui, em sua própria cidade, o que ouvimos que você fez em Cafarnaum?’
Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
24 Eu lhes digo que isto é verdade: nenhum profeta é bem recebido em sua própria cidade.
Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
25 Eu garanto que havia muitas viúvas em Israel durante a época de Elias, quando houve uma grande seca durante três anos e meio, causando muita fome em todo o país.
Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
26 Ainda assim, Deus não enviou Elias para qualquer uma dessas viúvas. Ele se encaminhou apenas para uma viúva em Sarepta, na região de Sidom.
Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
27 Mesmo havendo muitos leprosos em Israel no tempo de Eliseu, o único que ele curou foi Naamã, o sírio.”
Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
28 Quando eles ouviram isso, todos que estavam na sinagoga ficaram furiosos.
Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
29 Eles se levantaram e o expulsaram da cidade. Depois, eles o levaram para o alto da colina em que a cidade estava construída, para jogá-lo do penhasco.
Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
30 Mas, ele passou entre eles e foi embora.
Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
31 Jesus foi para Cafarnaum, uma cidade na região da Galileia. No sábado, ele começou a ensinar o povo de lá.
Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
32 Eles estavam impressionados com o que ele lhes ensinava, pois falava com autoridade.
Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
33 Na sinagoga, havia um homem que estava possuído pelo demônio. Ele gritou:
Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
34 “Então, Jesus de Nazaré, o que você quer de nós? Você veio para nos destruir? Eu sei quem é você: é o Santo que Deus enviou!”
“Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
35 Jesus o interrompeu, dizendo: “Fique quieto!” Então, ele ordenou ao demônio: “Saia deste homem!” Na frente de todos, o demônio jogou o homem no chão e saiu dele sem lhe causar ferimentos.
Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
36 Todos ficaram admirados e perguntavam uns aos outros: “Que palavras são essas? Com poder e autoridade, ele ordena que os espíritos saiam, e eles obedecem!”
Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
37 As notícias sobre Jesus se espalharam pelas cidades ao redor.
Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
38 Ao sair da sinagoga, Jesus foi para a casa de Simão. A sogra de Simão estava doente, com uma febre muito alta, e eles pediram que Jesus a ajudasse.
Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
39 Jesus foi e ficou perto dela. Ele ordenou que a febre passasse e, assim, aconteceu. Ela se levantou imediatamente e preparou uma refeição para eles.
Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
40 Quando o sol se pôs, eles levaram a Jesus todos que estavam doentes, sofrendo de várias doenças. Ele colocou as suas mãos sobre eles, um após o outro, e todos foram curados.
Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
41 Vários demônios, expulsos das pessoas, gritavam: “Você é o Filho de Deus!” Mas, Jesus os repreendia e se recusava a deixar que eles falassem, pois eles sabiam que ele era o Messias.
Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
42 Na manhã do dia seguinte, Jesus saiu para encontrar um lugar tranquilo e silencioso. Mas, a multidão saiu a sua procura e, finalmente, o encontrou. Eles insistiam para que ele não fosse embora.
Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
43 Ele lhes disse: “Eu também preciso ir a outras cidades, para anunciar as boas novas do Reino de Deus. Foi para isso que eu fui enviado.”
Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
44 Então, Jesus percorreu as sinagogas da Judeia, anunciando as boas novas do Reino.
Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.

< Lucas 4 >