< Números 1 >

1 E o SENHOR falou a Moisés no deserto de Sinai, no tabernáculo do testemunho, no primeiro dia do mês segundo, no segundo ano de sua saída da terra do Egito, dizendo:
Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
2 Tomai o censo de toda a congregação dos filhos de Israel por suas famílias, pelas casas de seus pais, com a conta dos nomes, todos os homens por suas cabeças:
“Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
3 De vinte anos acima, todos os que podem sair à guerra em Israel, os contareis tu e Arão por suas tropas.
Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
4 E estará convosco um homem de cada tribo, cada um chefe da casa de seus pais.
Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
5 E estes são os nomes dos homens que estarão convosco: Da tribo de Rúben, Elizur filho de Sedeur.
Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
6 De Simeão, Selumiel filho de Zurisadai.
kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
7 De Judá, Naassom filho de Aminadabe.
kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
8 De Issacar, Natanael filho de Zuar.
kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
9 De Zebulom, Eliabe filho de Helom.
kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
10 Dos filhos de José: de Efraim, Elisama filho de Amiúde; de Manassés, Gamaliel filho de Pedazur.
kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
11 De Benjamim, Abidã filho de Gideoni.
kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
12 De Dã, Aiezer filho de Amisadai.
kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
13 De Aser, Pagiel filho de Ocrã.
kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
14 De Gade, Eliasafe filho de Deuel.
kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
15 De Naftali, Aira filho de Enã.
kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
16 Estes foram os nomeados da congregação, príncipes das tribos de seus pais, capitães dos milhares de Israel.
Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
17 Tomou pois Moisés e Arão a estes homens que foram declarados por seus nomes:
Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
18 E juntaram toda a congregação no primeiro dia do mês segundo, e foram reunidos suas linhagens, pelas casas de seus pais, segundo a conta dos nomes, de vinte anos acima, por suas cabeças,
wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
19 Como o SENHOR o havia mandado a Moisés; e contou-os no deserto de Sinai.
kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
20 E os filhos de Rúben, primogênito de Israel, por suas gerações, por suas famílias, pelas casas de seus pais, conforme a conta dos nomes por suas cabeças, todos os homens de vinte anos acima, todos os que podiam sair à guerra;
Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
21 Os contados deles, da tribo de Rúben, foram quarenta e seis mil e quinhentos.
Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
22 Dos filhos de Simeão, por suas gerações, por suas famílias, pelas casas de seus pais, os contados deles conforme a conta dos nomes por suas cabeças, todos os homens de vinte anos acima, todos os que podiam sair à guerra;
Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
23 Os contados deles, da tribo de Simeão, cinquenta e nove mil e trezentos.
Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
24 Dos filhos de Gade, por suas gerações, por suas famílias, pelas casas de seus pais, conforme a conta dos nomes, de vinte anos acima, todos os que podiam sair à guerra;
Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
25 Os contados deles, da tribo de Gade, quarenta e cinco mil seiscentos e cinquenta.
Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
26 Dos filhos de Judá, por suas gerações, por suas famílias, pelas casas de seus pais, conforme a conta dos nomes, de vinte anos acima, todos os que podiam sair à guerra;
Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
27 Os contados deles, da tribo de Judá, setenta e quatro mil e seiscentos.
Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
28 Dos filhos de Issacar, por suas gerações, por suas famílias, pelas casas de seus pais, conforme a conta dos nomes, de vinte anos acima, todos os que podiam sair à guerra;
Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
29 Os contados deles, da tribo de Issacar, cinquenta e quatro mil e quatrocentos.
Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
30 Dos filhos de Zebulom, por suas gerações, por suas famílias, pelas casas de seus pais, conforme a conta de seus nomes, de vinte anos acima, todos os que podiam sair à guerra;
Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
31 Os contados deles, da tribo de Zebulom, cinquenta e sete mil e quatrocentos.
Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
32 Dos filhos de José: dos filhos de Efraim, por suas gerações, por suas famílias, pelas casas de seus pais, conforme a conta dos nomes, de vinte anos acima, todos os que podiam sair à guerra;
Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
33 Os contados deles, da tribo de Efraim, quarenta mil e quinhentos.
Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
34 Dos filhos de Manassés, por suas gerações, por suas famílias, pelas casas de seus pais, conforme a conta dos nomes, de vinte anos acima, todos os que podiam sair à guerra;
Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
35 Os contados deles, da tribo de Manassés, trinta e dois mil e duzentos.
Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
36 Dos filhos de Benjamim, por suas gerações, por suas famílias, pelas casas de seus pais, conforme a conta dos nomes, de vinte anos acima, todos os que podiam sair à guerra;
Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
37 Os contados deles, da tribo de Benjamim, trinta e cinco mil e quatrocentos.
Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
38 Dos filhos de Dã, por suas gerações, por suas famílias, pelas casas de seus pais, conforme a conta dos nomes, de vinte anos acima, todos os que podiam sair à guerra;
Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
39 Os contados deles, da tribo de Dã, sessenta e dois mil e setecentos.
Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
40 Dos filhos de Aser, por suas gerações, por suas famílias, pelas casas de seus pais, conforme a conta dos nomes, de vinte anos acima, todos os que podiam sair à guerra.
Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
41 Os contados deles, da tribo de Aser, quarenta e um mil e quinhentos.
Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
42 Dos filhos de Naftali, por suas gerações, por suas famílias, pelas casas de seus pais, conforme a conta dos nomes, de vinte anos acima, todos os que podiam sair à guerra;
Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
43 Os contados deles, da tribo de Naftali, cinquenta e três mil e quatrocentos.
Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
44 Estes foram os contados, os quais contaram Moisés e Arão, com os príncipes de Israel, que eram doze, um por cada casa de seus pais.
Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
45 E foram todos os contados dos filhos de Israel pelas casas de seus pais, de vinte anos acima, todos os que podiam sair à guerra em Israel;
Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
46 Foram todos os contados seiscentos três mil quinhentos e cinquenta.
Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
47 Porém os levitas não foram contados entre eles segundo a tribo de seus pais.
Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
48 Porque falou o SENHOR a Moisés, dizendo:
Bwana alikuwa amemwambia Mose:
49 Somente não contarás a tribo de Levi, nem tomarás a conta deles entre os filhos de Israel:
“Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
50 Mas tu porás aos levitas no tabernáculo do testemunho, e sobre todos os seus utensílios, e sobre todas as coisas que lhe pertencem: eles levarão o tabernáculo e todos os seus utensílios, e eles servirão nele, e assentarão suas tendas ao redor do tabernáculo.
Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
51 E quando o tabernáculo partir, os levitas o desarmarão; e quando o tabernáculo parar, os levitas o armarão: e o estranho que se chegar, morrerá.
Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
52 E os filhos de Israel assentarão suas tendas cada um em seu esquadrão, e cada um junto à sua bandeira, por suas tropas;
Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
53 Mas os levitas assentarão as suas ao redor do tabernáculo do testemunho, e não haverá ira sobre a congregação dos filhos de Israel: e os levitas terão a guarda do tabernáculo do testemunho.
Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
54 E fizeram os filhos de Israel conforme todas as coisas que mandou o SENHOR a Moisés; assim o fizeram.
Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.

< Números 1 >