< 33 >

1 Portanto, Jó, ouve, por favor, meus dizeres, e dá ouvidos a todas as minhas palavras.
“Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
2 Eis que já abri minha boca; minha língua já fala debaixo do meu céu da boca.
Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
3 Meus dizeres pronunciarão a integridade do meu coração, e o puro conhecimento dos meus lábios.
Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
4 O Espírito de Deus me fez, e o sopro do Todo-Poderoso me deu vida.
Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
5 Se puderes, responde-me; dispõe-te perante mim, e persiste.
Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
6 Eis que para Deus eu sou como tu; do barro também eu fui formado.
Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
7 Eis que meu terror não te espantará, nem minha mão será pesada sobre ti.
Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
8 Certamente tu disseste a meus ouvidos, e eu ouvi a voz de tuas palavras,
“Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
9 [Que diziam]: Eu sou limpo e sem transgressão; sou inocente, e não tenho culpa.
‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
10 Eis que [Deus] buscou pretextos contra mim, [e] me tem por seu inimigo.
Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
11 Ele pôs meus pés no tronco, e observa todas as minhas veredas.
Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
12 Eis que nisto não foste justo, eu te respondo; pois Deus é maior que o ser humano.
“Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
13 Por que razão brigas contra ele por não dar resposta às palavras do ser humano?
Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
14 Contudo Deus fala uma ou duas vezes, ainda que [o ser humano] não entenda.
Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
15 Em sonho [ou em] visão noturna, quando o sono profundo cai sobre as pessoas, [e] adormecem na cama.
Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
16 Então o revela ao ouvido das pessoas, e os sela com advertências;
anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
17 Para desviar ao ser humano de sua obra, e do homem a soberba.
ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
18 Para desviar a sua alma da perdição, e sua vida de passar pela espada.
kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
19 Também em sua cama é castigado com dores, com luta constante em seus ossos,
Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
20 De modo que sua vida detesta [até] o pão, e sua alma a comida deliciosa.
kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
21 Sua carne desaparece da vista, e seus ossos, que antes não se viam, aparecem.
Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
22 Sua alma se aproxima da cova, e sua vida dos que causam a morte.
Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
23 Se com ele, pois, houver algum anjo, algum intérprete; um dentre mil, para anunciar ao ser humano o que lhe é correto,
“Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
24 Então [Deus] terá misericórdia dele, e [lhe] dirá: Livra-o, para que não desça à perdição; [já] achei o resgate.
kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
25 Sua carne se rejuvenescerá mais do que era na infância, [e] voltará aos dias de sua juventude.
ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
26 Ele orará a Deus, que se agradará dele; e verá sua face com júbilo, porque ele restituirá ao ser humano sua justiça.
Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
27 Ele olhará para as pessoas, e dirá: Pequei, e perverti o [que era] correto, o que de nada me aproveitou.
Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
28 [Porém] Deus livrou minha alma para que eu não passasse à cova, e [agora] minha vida vê a luz!
Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
29 Eis que Deus faz tudo isto duas [ou] três vezes com o ser humano,
“Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
30 Para desviar sua alma da perdição, e o iluminar com a luz dos viventes.
ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
31 Presta atenção, Jó, e ouve-me; cala-te, e eu falarei.
“Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
32 Se tiveres o que dizer, responde-me; fala, porque eu quero te justificar.
Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
33 E se não, escuta-me; cala-te, e eu ensinarei sabedoria.
Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”

< 33 >