< Gálatas 5 >

1 Para a liberdade Cristo nos libertou; portanto, estai firmes, e não volteis a vos prender com o jugo da escravidão.
Ni kwa sababu Kristo alitupa uhuru ili tuwe huru. Hivyo, simameni imara wala msinaswe tena katika kongwa la utumwa.
2 Eis que eu, Paulo, vos digo, que se vos deixardes circuncidar, Cristo vos será útil em nada.
Tazama, Mimi Paulo, ninawaambia kwamba ikiwa mtatahiriwa, Kristo hatawafaidia kwa njia yoyote ile.
3 E de novo atesto que todo homem que se deixar circuncidar está obrigado a obedecer a toda a Lei.
Tena, namshuhudia kila mwanaume aliyetahiriwa kwamba anapaswa kuwajibika kwa sheria yote.
4 Desligados estais de Cristo, vós que [quereis] ser justos pela Lei; da graça caístes.
Mmetengwa mbali na Kristo, wale wote “mnaohesabiwa haki” kwa sheria. Mmeanguka mbali na neema.
5 Pois, por meio do Espírito, pela fé, aguardamos a esperança da justiça;
Maana kwa njia ya Roho, kwa imani tunasubiri ujasiri wa haki.
6 porque, em Cristo Jesus, nem a circuncisão nem a incircuncisão tem valor algum; mas sim a fé, que opera por meio do amor.
Katika Kristo Yesu kutahiriwa au kutokutahiriwa hakuna maana yoyote. Ni imani pekee inayofanya kazi kupitia upendo ndiyo humaanisha kitu.
7 Estáveis correndo bem; quem vos impediu de obedecerdes à verdade?
Mlikuwa mnapiga mbio vizuri. Nani aliwazuia kutokuitii kweli?
8 Esta persuasão não parte daquele que vos chama.
Ushawishi wa kufanya hivyo hautoki kwake yeye anayewaita ninyi.
9 Um pouco de fermento leveda toda a massa.
Chachu kidogo huathiri donge zima.
10 Acerca de vós, confio no Senhor de que não mudareis a vossa mentalidade; mas aquele que vos perturba, seja quem for, sofrerá o julgamento.
Nina matumaini na ninyi katika Bwana kwamba hamtafikiri kwa njia nyingine yoyote. Yeyote yule atakayewapotosha atabeba hukumu yake yeye mwenyewe, yeyote yule.
11 Mas se eu, irmãos, ainda prego a circuncisão, por que, então, sou perseguido? Então a ofensa da cruz está anulada!
Ndugu, kama naendelea kutangaza tohara, kwanini bado ninateswa? Kwa suala hilo kile ambacho ni kizuizi cha msalaba kitaweza kuharibiwa.
12 Gostaria que aqueles que estão vos perturbando castrassem a si mesmos.
Ni matakwa yangu kuwa wale wanaowaongoza vibaya watajihasi wenyewe.
13 Pois vós, irmãos, fostes chamados para a liberdade. Somente não [useis] a liberdade como oportunidade para a carne; em vez disso, servi-vos uns aos outros pelo amor.
Mungu amewaiteni ninyi, ndugu, kwenye uhuru. Ila msiutumie uhuru wenu kama fursa kwa mwili. Badala yake kwa upendo mhudumiane ninyi kwa ninyi.
14 Pois toda a Lei se cumpre em uma só regra, que é: Amarás ao teu próximo como a ti mesmo.
Kwa kuwa sheria yote imekamilika katika amri moja; nayo ni “Ni lazima umpende jirani yako kama wewe mwenyewe.”
15 Se, porém, mordeis e devorais uns aos outros, cuidado para não vos destruirdes mutuamente.
Lakini kama mkiumana na kulana, jiangalieni kwamba msijiharibu ninyi kwa ninyi.
16 Mas eu digo: andai no Espírito, e não executeis o mau desejo da carne.
Nasema, tembeeni kwa roho, na wala hamtazitimiza tamaa za mwili.
17 Pois a carne deseja contra o Espírito, e o Espírito contra a carne; pois estes se opõem mutuamente, para que não façais o que quereis.
Kwa kuwa mwili una tamaa kubwa dhidi ya Roho, na Roho ina tamaa kubwa dhidi ya mwili. Hizi zinapingana kila moja na nyingine. Matokeo ni kwamba hamfanyi vitu mnavyotamani kuvifanya.
18 Mas, se sois guiados pelo Espírito, não estais debaixo da Lei.
Lakini kama Roho anawaongoza ninyi, hamko chini ya sheria.
19 As obras da carne são evidentes. São elas: pecado sexual, impureza, devassidão,
Sasa matendo ya mwili yanaonekana. Nayo ni uasherati, uchafu, ufisadi,
20 idolatria, feitiçaria, inimizades, brigas, ciúmes, iras, rivalidades egoístas, desavenças, facções,
ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, husuda, kuwaka hasira, ushindani, faraka, mgawanyiko wa madhehebu,
21 invejas, bebedices, orgias, e coisas semelhantes a essas, das quais eu havia vos dito anteriormente; assim como eu também haviavos dito antes que os que praticam tais coisas não herdarão o Reino de Deus.
wivu, ulevi, ulafi na mambo mengine kama haya. Nawaonya ninyi, kama nilivyowaonya mwanzoni, kwamba wale wanaofanya mambo kama hayo hawataurithi ufalme wa Mungu.
22 Mas o fruto do Espírito é: amor, alegria, paz, paciência, benignidade, bondade, fidelidade,
Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, ukarimu, utu wema, imani,
23 mansidão, domínio próprio. Contra essas coisas não há lei.
upole, na kiasi. Hakuna sheria dhidi ya mambo kama hayo.
24 Os que são de Cristo Jesus crucificaram a carne com as paixões e os maus desejos.
Wale walio wa Kristo Yesu wameusulubisha mwili pamoja na shauku na tamaa zao mbaya.
25 Se vivemos no Espírito, também no Espírito andemos.
Kama tukiishi kwa Roho, pia tutembee kwa Roho.
26 Não nos tornemos presunçosos, irritando uns aos outros, e invejando uns aos outros.
Tusiwe wa kujivuna, tusichokozane kila mmoja na mwenzake, wala tusioneane wivu.

< Gálatas 5 >