< Lucas 21 >

1 E, olhando ele, viu os ricos lançarem as suas ofertas na arca do tesouro;
Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
2 E viu também uma pobre viúva lançar ali duas pequenas moedas;
Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
3 E disse: Em verdade vos digo que lançou mais do que todos esta pobre viúva;
Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
4 Porque todos aqueles deitaram para as ofertas de Deus, do que lhes sobeja; mas esta, da sua pobreza, deitou todo o sustento que tinha.
Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
5 E, dizendo alguns a respeito do templo, que estava ornado de formosas pedras e dádivas, disse:
Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
6 Quanto a estas coisas que vêdes, dias virão em que se não deixará pedra sobre pedra, que não seja derribada.
“Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
7 E perguntaram-lhe, dizendo: Mestre, quando serão pois estas coisas? E que sinal haverá quando estas coisas estiverem para acontecer?
Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
8 Disse então ele: vede não vos enganem, porque virão muitos em meu nome, dizendo: Eu sou o Cristo, e já o tempo está próximo; não vades portanto após eles.
Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
9 E, quando ouvirdes de guerras e sedições, não vos assusteis. Porque é necessário que estas coisas aconteçam primeiro, mas o fim não será logo.
Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
10 Então lhes disse: levantar-se-a nação contra nação, e reino contra reino;
Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
11 E haverá em vários lugares grandes terremotos, e fomes e pestilências; haverá também coisas espantosas, e grandes sinais do céu.
Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
12 Mas antes de todas estas coisas lançarão mão de vós, e vos perseguirão, entregando-vos às sinagogas e às prisões, e conduzindo-vos à presença de reis e presidentes, por amor do meu nome.
“Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
13 E sobrevir-vos-a isto para testemunho.
Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
14 Proponde pois em vossos corações não premeditar como haveis de responder,
Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
15 Porque eu vos darei boca e sabedoria a que não poderão contradizer nem resistir todos quantos se vos opuserem.
Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
16 E até pelos pais, e irmãos, e parentes, e amigos sereis entregues; e matarão alguns de vós.
Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
17 E por todos sereis aborrecidos por amor do meu nome.
Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
18 Mas não perecerá nem um cabelo da vossa cabeça.
Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
19 Na vossa paciência possui as vossas almas.
Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
20 Porém, quando virdes Jerusalém cercada de exércitos, sabei então que já é chegada a sua assolação.
“Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
21 Então, os que estiverem na Judeia, fujam para os montes; e, os que estiverem no meio dela, saiam: e, os que nos campos, não entrem nela.
Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
22 Porque dias de vingança são estes, para que se cumpram todas as coisas que estão escritas.
Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
23 Mas ai das grávidas, e das que criarem naqueles dias! porque haverá grande aperto na terra, e ira sobre este povo.
Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
24 E cairão ao fio da espada, e para todas as nações serão levados cativos; e Jerusalém será pisada pelos gentios, até que os tempos dos gentios se completem.
Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
25 E haverá sinais no sol, e na lua e nas estrelas; e na terra aperto das nações em perplexidade, pelo bramido do mar e das ondas;
“Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
26 Homens desmaiando de terror, na expectação das coisas que sobrevirão ao mundo. Porque as virtudes do céu serão abaladas.
Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
27 E então verão vir o Filho do homem numa nuvem, com poder e grande glória.
Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
28 Ora, quando estas coisas começarem a acontecer, olhai para cima, e levantai as vossas cabeças, porque a vossa redenção está próxima.
Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
29 E disse-lhes uma parábola: olhai para a figueira, e para todas as árvores;
Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
30 Quando já tem brotado, vós sabeis por vós mesmos, vendo-as, que perto está já o verão.
Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
31 Assim também vós, quando virdes acontecer estas coisas, sabei que o reino de Deus está perto.
Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
32 Em verdade vos digo que não passará esta geração até que tudo aconteça.
“Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
33 Passará o céu e a terra, mas as minhas palavras não hão de passar.
Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
34 E olhai por vós, não aconteça que os vossos corações se carreguem de glutonaria, embriaguez, e dos cuidados desta vida, e venha sobre vós de improviso aquele dia.
“Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
35 Porque virá como um laço sobre todos os que habitam sobre a face de toda a terra.
Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
36 Vigiai pois em todo o tempo, orando, para que sejais havidos por dignos de evitar todas estas coisas que hão de acontecer, e de estar em pé diante do Filho do homem.
Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
37 E de dia ensinava no templo, e à noite, saindo, ficava no monte chamado das Oliveiras.
Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
38 E todo o povo ia ter com ele ao templo, de manhã cedo, para o ouvir.
Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.

< Lucas 21 >