< Êxodo 28 >

1 Depois tu farás chegar a ti teu irmão Aarão, e seus filhos com elle, do meio dos filhos de Israel, para me administrarem o officio sacerdotal: a saber, Aarão, Nadab e Abihu, Eleazar e Ithamar, os filhos de Aarão.
“Mtwae Aroni ndugu yako aliyeletwa kwako kutoka miongoni mwa Waisraeli, pamoja na wanawe Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
2 E farás vestidos sanctos a Aarão teu irmão, para gloria e ornamento.
Mshonee Aroni ndugu yako mavazi matakatifu ili yampe ukuu na heshima.
3 Fallarás tambem a todos os que são sabios de coração, a quem eu tenho enchido do espirito da sabedoria, que façam vestidos a Aarão para sanctifical-o; para que me administre o officio sacerdotal.
Waambie mafundi stadi wote niliowapa hekima katika shughuli hiyo wamtengenezee Aroni mavazi hayo, ili awekwe wakfu, anitumikie katika kazi ya ukuhani.
4 Estes pois são os vestidos que farão: um peitoral, e um ephod, e um manto, e uma tunica bordada, uma mitra, e um cinto: farão pois sanctos vestidos a Aarão teu irmão, e a seus filhos, para me administrarem o officio sacerdotal.
Haya ndiyo mavazi watakayoshona: kifuko cha kifuani, kisibau, kanzu, joho lililorembwa, kilemba na mshipi. Mavazi haya yatashonwa kwa ajili ya ndugu yako Aroni na wanawe ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
5 E tomarão o oiro, e o azul, e a purpura, e o carmezim, e o linho fino,
Waambie watumie dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani safi.
6 E farão o ephod de oiro, e de azul, e de purpura, e de carmezim, e de linho fino torcido, de obra esmerada.
“Tengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa, kazi ya fundi stadi.
7 Terá duas hombreiras, que se unam ás suas duas pontas, e assim se unirá.
Kitakuwa na vipande viwili vya mabegani vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kufungia kisibau.
8 E o cinto de obra esmerada do seu ephod, que estará sobre elle, será da sua mesma obra, do mesmo, de oiro, de azul, e de purpura, e de carmezim, e de linho fino torcido.
Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi utafanana nacho: utakuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao utengenezwe kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri.
9 E tomarás duas pedras sardonicas, e lavrarás n'ellas os nomes dos filhos de Israel,
“Chukua vito viwili vya shohamu, na uchore juu yake majina ya wana wa Israeli
10 Seis dos seus nomes n'uma pedra, e os outros seis nomes na outra pedra, segundo as suas gerações;
kufuatana na walivyozaliwa: majina sita katika kito kimoja, na mengine sita katika kito kingine.
11 Conforme á obra do lapidario, como o lavor de sêllos lavrarás estas duas pedras, com os nomes dos filhos de Israel: engastadas ao redor em oiro as farás.
Yachore majina ya wana wa Israeli juu ya vito hivyo viwili kama vile sonara anavyochonga muhuri. Kisha uvitie vito hivyo katika vijalizo vya dhahabu,
12 E porás as duas pedras nas hombreiras do ephod, por pedras de memoria para os filhos de Israel: e Aarão levará os seus nomes sobre ambos os seus hombros, para memoria diante do Senhor.
na uvifungie juu ya vipande vya mabega ya kisibau yawe kama vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli. Aroni atavaa majina hayo mabegani mwake kama kumbukumbu mbele za Bwana.
13 Farás tambem engastes de oiro,
Tengeneza vijalizo vya dhahabu
14 E duas cadeiasinhas de oiro puro: de egual medida, de obra de fieira as farás: e as cadeiasinhas de fieira porás nos engastes.
na mikufu miwili ya dhahabu safi iliyosokotwa kama kamba, na uifunge mikufu hiyo kwenye vijalizo.
15 Farás tambem o peitoral do juizo de obra esmerada, conforme á obra do ephod o farás: de oiro, de azul, e de purpura, e de carmezim, e de linho fino torcido o farás.
“Fanyiza kifuko cha kifuani kwa ajili ya kufanya maamuzi, kazi ya fundi stadi. Kitengeneze kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
16 Quadrado e dobrado, será de um palmo o seu comprimento, e de um palmo a sua largura;
Kitakuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, na kikunjwe mara mbili.
17 E o encherás de pedras de engaste, com quatro ordens de pedras: a ordem de uma sardia, de um topazio, e de um carbunculo: esta será a primeira ordem:
Kisha weka safu nne za vito vya thamani juu yake. Safu ya kwanza itakuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
18 E a segunda ordem será de uma esmeralda, de uma saphira, e de um diamante:
katika safu ya pili itakuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
19 E a terceira ordem será de um jacinto, de uma agatha, e de uma amethista:
safu ya tatu itakuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
20 E a quarta ordem será de uma turqueza, e de uma sardonica, e de um jaspe; engastadas em oiro serão nos seus engastes.
na safu ya nne itakuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Yote yatiwe kwenye vijalizo vya dhahabu.
21 E serão aquellas pedras segundo os nomes dos filhos de Israel, doze segundo os seus nomes: serão esculpidas como sêllos, cada uma com o seu nome, para as doze tribus.
Patakuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kwa jina mojawapo la wana wa Israeli, kila kimoja kichorwe kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
22 Tambem farás ao peitoral cadeiasinhas de egual medida da obra de trança de oiro puro.
“Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani, tengeneza mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
23 Tambem farás ao peitoral dois anneis de oiro, e porás os dois anneis nas extremidades do peitoral.
Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili yake, uzifungie kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
24 Então metterás as duas cadeiasinhas de fieira d'oiro nos dois anneis, nas extremidades do peitoral:
Funga ile mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete zilizo katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
25 E as duas pontas das duas cadeiasinhas de fieira metterás nos dois engastes, e as porás nas hombreiras do ephod, defronte d'elle.
nazo zile ncha nyingine za mkufu zifunge kwenye vile vijalizo viwili, na uzishikamanishe na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
26 Farás tambem dois anneis d'oiro, e os porás nas duas extremidades do peitoral, na sua borda que estiver junto ao ephod por dentro.
Tengeneza pete mbili za dhahabu, uzishikamanishe kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
27 Farás tambem dois anneis d'oiro, que porás nas duas hombreiras do ephod, abaixo, defronte d'elle, defronte da sua juntura, sobre o cinto d'obra esmerada do ephod.
Tengeneza pete nyingine mbili za dhahabu, na uzishikamanishe sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
28 E ligarão o peitoral com os seus anneis aos anneis do ephod por cima com um cordão d'azul, para que esteja sobre o cinto d'obra esmerada do ephod; e nunca se separará o peitoral do ephod.
Pete za kifuko cha kifuani zitafungwa kwenye pete zile za kisibau kwa kamba ya buluu, ziunganishwe na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau.
29 Assim Aarão levará os nomes dos filhos d'Israel no peitoral do juizo sobre o seu coração, quando entrar no sanctuario, para memoria diante do Senhor continuamente.
“Wakati wowote Aroni aingiapo Mahali Patakatifu, atakuwa na yale majina ya wana wa Israeli moyoni mwake juu ya kile kifuko cha kifuani cha uamuzi kama kumbukumbu ya kudumu mbele za Bwana.
30 Tambem porás no peitoral do juizo Urim e Thummim, para que estejam sobre o coração de Aarão, quando entrar diante do Senhor: assim Aarão levará o juizo dos filhos de Israel sobre o seu coração diante do Senhor continuamente.
Pia weka Urimu na Thumimu ndani ya kifuko cha kifuani, yawe juu ya moyo wa Aroni kila mara aingiapo mbele za Bwana. Kwa hiyo siku zote Aroni atakuwa na uwezo kufanya maamuzi kwa ajili ya wana wa Israeli mbele za Bwana.
31 Tambem farás o manto do ephod, todo azul.
“Shona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu,
32 E o collar da cabeça estará no meio d'elle: este collar terá uma borda d'obra tecida ao redor: como collar de saia de malha será n'elle, para que se não rompa.
na katikati uweke nafasi ya kuingizia kichwa. Kutakuwa na utepe uliofumwa, unaofanana na ukosi kuizunguka nafasi hiyo, ili isichanike.
33 E nas suas bordas farás romãs d'azul, e de purpura, e de carmezim, ao redor das suas bordas; e campainhas d'oiro no meio d'ellas ao redor.
Tengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu kuzunguka pindo la hilo joho, na uweke pia vikengele vya dhahabu kati ya hayo makomamanga.
34 Uma campainha d'oiro, e uma romã, outra campainha d'oiro, e outra romã, haverá nas bordas do manto ao redor,
Hivyo vikengele vya dhahabu na makomamanga vitapishana kuzunguka upindo wa joho lile.
35 E estará sobre Aarão quando ministrar, para que se ouça o seu sonido, quando entrar no sanctuario diante do Senhor, e quando sair, para que não morra.
Ni lazima Aroni alivae anapofanya huduma. Sauti ya hivyo vikengele itasikika anapoingia na kutoka Mahali Patakatifu mbele za Bwana, ili asije akafa.
36 Tambem farás uma lamina d'oiro puro, e n'ella gravarás á maneira de gravuras de sellos: Sanctidade ao Senhor.
“Tengeneza bamba la dhahabu safi na uchore juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
37 E atal-a-has com um cordão d'azul, de maneira que esteja na mitra; sobre a frente da mitra estará.
Lifunge hilo bamba kwa kamba ya buluu kwenye kilemba, nalo ni lazima liwe mbele ya kilemba.
38 E estará sobre a testa de Aarão, para que Aarão leve a iniquidade das coisas sanctas, que os filhos d'Israel sanctificarem em todas as offertas de suas coisas sanctas; e estará continuamente na sua testa, para que tenham acceitação perante o Senhor.
Aroni alivae bamba hilo kwenye paji la uso wake, naye atachukua hatia kuhusu sadaka takatifu za Waisraeli wanazoweka wakfu, sadaka za aina yoyote. Litakuwa kwenye paji la uso wa Aroni daima ili zikubalike kwa Bwana.
39 Tambem farás tunica de linho fino: tambem farás uma mitra de linho fino: mas o cinto farás d'obra de bordador.
“Fuma koti la kitani safi na ufanye kilemba cha kitani safi. Mshipi uwe ni kazi ya mtarizi.
40 Tambem farás tunicas aos filhos de Aarão, e far-lhes-has cintos: tambem lhes farás tiaras, para gloria e ornamento.
Watengenezee wana wa Aroni makoti, mishipi na kofia, ili kuwapa ukuu na heshima.
41 E vestirás com elles a Aarão teu irmão, e tambem seus filhos: e os ungirás e consagrarás, e os sanctificarás, para que me administrem o sacerdocio.
Baada ya kumvika Aroni ndugu yako pamoja na wanawe nguo hizi, watie mafuta na kuwabariki. Waweke wakfu ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
42 Faze-lhes tambem calções de linho, para cobrirem a carne nua: serão dos lombos até ás pernas.
“Watengenezee nguo za ndani za kitani zitakazofunika mwili, kutoka kiunoni hadi mapajani.
43 E estarão sobre Aarão e sobre seus filhos, quando entrarem na tenda da congregação, ou quando chegarem ao altar para ministrar no sanctuario, para que não levem iniquidade, e morram; isto será estatuto perpetuo para elle e para a sua semente depois d'elle.
Aroni na wanawe ni lazima wavae haya kila wanapoingia katika Hema la Kukutania au wanaposogelea madhabahu wakati wa kutoa huduma katika Mahali Patakatifu, ili wasije wakafanya kosa wakafa. “Haya yawe maagizo ya kudumu kwa Aroni na vizazi vyake.

< Êxodo 28 >