< Deuteronômio 23 >

1 O quebrado de quebradura, e o castrado, não entrará na congregação do Senhor.
Mwanamume aliyejeruhiwa kwa kupondwa au kukatwa haruhusiwi kuingia katika kusanyiko la Yahwe.
2 Nenhum bastardo entrará na congregação do Senhor: nem ainda a sua decima geração entrará na congregação do Senhor.
Mwana haramu haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe; kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake, hakuna kati yao anatakiwa kuwa kwenye kusanyiko la Yahwe.
3 Nenhum ammonita nem moabita entrará na congregação do Senhor: nem ainda a sua decima geração entrará na congregação do Senhor eternamente.
Muamori au Mmoabu haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe; kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake, hakuna kati yao anatakiwa kuwa kwenye kusanyiko la Yahwe.
4 Porquanto não sairam com pão e agua, a receber-vos no caminho, quando saíeis do Egypto; e porquanto alugou contra ti a Balaão, filho de Beor, de Pethor, de Mesopotamia, para te amaldiçoar.
Hii ni kwa sababu hawakukutana nanyi kwa mkate na maji barabarani mlipokuwa mmetoka nje ya Misri, na kwa sababu walimkodisha Balaamu mwana wa Beoro kutoka Pethoro kule Aramu Naharaimu, awalaani.
5 Porém o Senhor teu Deus não quiz ouvir Balaão: antes o Senhor teu Deus trocou em benção a maldição; porquanto o Senhor teu Deus te amava.
Lakini Yahwe Mungu wako hakumsikiliza Balaamu; badala yake, Yahwe Mungu wako aligeuza laana kuwa baraka kwenu, kwa sababu Yahwe Mungu wako aliwapenda.
6 Não lhes procurarás nem paz nem bem em todos os teus dias para sempre.
Hamtakiwi kutafuta amani au mafanikio yao, katika siku zenu zote.
7 Não abominarás o edumeo, pois é teu irmão: nem abominarás o egypcio; pois estrangeiro foste na sua terra.
Hutakiwi kumchukia Muedomi, kwa maana ni kaka yako; hutakiwi kumchukia Mmisri, kwa maana ulikuwa mgeni katika nchi yake.
8 Os filhos que lhes nascerem na terceira geração, cada um d'elles entrará na congregação do Senhor.
Wazawa wa kizazi cha tatu wanaozaliwa kwao wanaweza kuwa katika kusanyiko la Yahwe.
9 Quando o exercito sair contra os teus inimigos, então te guardarás de toda a coisa má.
Utakapotembea kijeshi dhidi ya maadui zako, basi unapaswa kujitenga na kila aina ya uovu.
10 Quando entre ti houver algum que por algum accidente de noite não estiver limpo, sairá fóra do exercito; não entrará no meio do exercito.
Iwapo miongoni mwenu kuna mwanamume ambaye sio msafi kwa sababu ya jambo lililofanyika kwake usiku, basi anatakiwa atoke nje ya kambi ya jeshi; hatakiwi kurudi kambini.
11 Porém será que, declinando a tarde, se lavará em agua; e, em se pondo o sol, entrará no meio do arraial.
Jioni ikifika, anatakiwa ajiogeshe kwa maji; na jua likizama atarudi ndani kambini.
12 Tambem terás um logar fóra do arraial; e ali sairás fóra.
Pia unatakiwa kuwa na eneo nje ya kambi ambayo utakwenda;
13 E entre as tuas armas terás uma pá; e será que, quando estiveres assentado fóra, então com ella cavarás, e, virando-te, cobrirás aquillo que saiu de ti.
na utakuwa na kitu katika zana zako cha kuchimbia; utakapochuchumaa kujisaidia, unapaswa kuchimbia nacho na kisha kurudishia udongo na kufunika kile kilichotoka kwako.
14 Porquanto o Senhor teu Deus anda no meio do teu arraial, para te livrar, e entregar os teus inimigos diante de ti: pelo que o teu arraial será sancto: para que elle não veja coisa feia em ti, e se torne atraz de ti.
Kwa maana Yahwe Mungu wako anatembea miongoni mwa kambi yenu kuwapa ushindi na kuwapa maadui zenu mkononi mwenu. Kwa hiyo kambi yenu lazima iwe takatifu, ili kwamba asione kitu chochote kichafu miongoni mwenu na kuwaacha.
15 Não entregarás a seu senhor o servo que se acolner a ti de seu senhor;
Hutakiwi kumrudishia bwana mtumwa aliyetoroka kwake.
16 Comtigo ficará no meio de ti, no logar que escolher em alguma das tuas portas, onde lhe estiver bem: não o opprimirás.
Mruhusu aishi pamoja nawe, katika mji wowote atakaochagua. Usimuonee.
17 Não haverá rameira d'entre as filhas d'Israel; nem haverá sodomita d'entre os filhos d'Israel.
Hapatakiwi kuwa na kahaba wa kidhehebu miongoni mwa mabinti wa Israeli, na wala hapatakiwi kuwa na kahaba wa kidhehebu miongoni mwa wana wa kiume wa Israeli.
18 Não trarás salario de rameira nem preço de cão á casa do Senhor teu Deus por qualquer voto: porque estes ambos são egualmente abominação ao Senhor teu Deus.
Hautakiwi kuleta mshahara wa kahaba au mshahara wa mbwa katika nyumba ya Yahwe Mungu wako kwa kiapo chochote; kwa maana vyote hivi na machukizo mbele ya Yahwe Mungu wako.
19 A teu irmão não emprestarás á usura, nem á usura de dinheiro, nem á usura de comida, nem á usura de qualquer coisa que se empreste á usura.
Hutakiwi kumkopesha Muisraeli mwenzako kwa riba – riba ya fedha, riba ya chakula, au riba ya kitu chochote kinachokopeshwa kwa riba.
20 Ao estranho emprestarás á usura, porém a teu irmão não emprestarás á usura: para que o Senhor teu Deus te abençoe em tudo no que pozeres a tua mão, na terra a qual vaes a possuir.
Kwa mgeni unaweza kukopesha kwa riba; lakini kwa Muisraeli mwenzako haupaswi kukopesha kwa riba, ili kwamba Yahwe Mungu wako aweze kukubariki katika kila jambo uwekalo mkono wako, katika nchi ambayo mnaenda kumiliki.
21 Quando votares algum voto ao Senhor teu Deus, não tardarás em pagal-o; porque o Senhor teu Deus certamente o requererá de ti, e em ti haverá peccado.
Unapofanya kiapo kwa Yahwe Mungu wako, haupaswi kukawia kuikamilsha, kwa maana Yahwe Mungu wako hakika atadai kiapo hicho; itakuwa dhambi kako usipokamilisha.
22 Porém, abstendo-te de votar, não haverá peccado em ti
Lakini iwapo utajizuia kutoa kiapo, haitakuwa dhambi kwako.
23 O que saiu da tua bocca guardarás, e o farás; trazendo a offerta voluntaria, assim como votaste ao Senhor teu Deus, o que declaraste pela tua bocca.
Kile ambacho kimetoka kinywani mwako unapaswa kukifuata na kukitekeleza; kulingana na kiapo ulichotamka kwa Yahwe Mungu wako, chochote ulichotamka kwa hiari kwa kinywa chako.
24 Quando entrares na vinha do teu proximo, comerás uvas conforme ao teu desejo até te fartares, porém não as porás no teu vaso
Utakapokwenda katika shamba la mizabibu la jirani yako, unatakiwa kula mizabibu idadi yoyote unayotaka, lakini hautakiwi kuhifadhi yoyote katika kikapu chako.
25 Quando entrares na seara do teu proximo, com a tua mão arrancarás as espigas; porém não metterás a foice na seara do teu proximo.
Utakapokwenda katika shamba la zao lililoiva la jirani yako, unaweza kuvuna kichwa cha mavuno kwa mkono wako, lakini haupaswi kutumia mundu kuvuna zao lililoiva la jirani yako.

< Deuteronômio 23 >