< Nehemiasza 12 >

1 A oto kapłani i Lewici, którzy przybyli z Zorobabelem, synem Szealtiela, i z Jeszuą: Serajasz, Jeremiasz, Ezdrasz;
Hawa ndio makuhani na Walawi waliokuja pamoja na Zerubabeli mwana wa Shealueli, pamoja na Yoshua Seraya, Yeremia, Ezra,
2 Amariasz, Malluk, Chattusz;
Amaria, Maluki, Hatushi,
3 Szekaniasz, Rechum, Meremot;
Shekania, Harimu na Meremothi.
4 Iddo, Ginneton, Abiasz;
Kulikuwa na Iddo, Ginethoni, Abiya,
5 Mijamin, Maadiasz, Bilga;
Miyamini, Maazia, Bilgai,
6 Szemajasz, Jojarib, Jedajasz;
Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,
7 Sallu, Amok, Chilkiasz, Jedajasz. To [byli] przedniejsi z kapłanów i ze swoich braci za dni Jeszuy.
Salu, Amoki, Hilkia, na Yedaya. Hawa walikuwa wakuu wa makuhani na washirika wao katika siku za Yoshua.
8 A Lewici: Jeszua, Binnuj, Kadmiel, Szerebiasz, Juda i Mattaniasz, który wraz z braćmi kierował śpiewem [pieśni dziękczynnych].
Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na Matania, aliyekuwa akiongoza nyimbo za shukrani, pamoja na washirika wake.
9 A Bakbukiasz i Unni, ich bracia, [stali] naprzeciw nich w [swoich] służbach.
Bakbukia na Uno, washirika wao, walisimama pembeni yao wakati wa huduma.
10 Jeszua spłodził Jojakima, a Jojakim spłodził Eliasziba, a Eliaszib spłodził Jojadę;
Yoshua alikuwa babaye Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa babaye Yoyada,
11 Jojada spłodził Jonatana, a Jonatan spłodził Jadduę.
Yoyada alimzaa Yonathani, Yonathani akamzaa Yadua.
12 A za dni Jojakima naczelnikami rodu byli [następujący] kapłani: z Serajasza – Merajasz, z Jeremiasza – Chananiasz;
Katika siku za Yoyakimu hawa walikuwa makuhani, wakuu wa jamaa; Meraya alikuwa mkuu wa Seraya, Hanania alikuwa kiongozi wa Yeremia,
13 Z Ezdrasza – Meszullam, z Amariasza – Jehochanan;
Meshulam alikuwa kiongozi wa Ezra, Yehohanani alikuwa kiongozi wa Amaria,
14 Z Malluki – Jonatan, z Szebaniasza – Józef;
Yonathani alikuwa kiongozi wa Maluki, na Yusufu alikuwa kiongozi wa Shekania.
15 Z Charima – Adna, z Merajota – Chelkaj;
Ili kuendelea, Adna alikuwa kiongozi wa Harimu, Helkai kiongozi wa Meremothi,
16 Z Iddo – Zachariasz, z Ginneto – Meszullam;
Zekaria alikuwa kiongozi wa Ido, Meshulamu alikuwa kiongozi wa Ginethoni, na
17 Z Abiasza – Zikri, z Miniamina i Moadiasza – Piltaj;
Zikri alikuwa kiongozi wa Abia wa Miyaamini. Piltai alikuwa kiongozi wa Maazia.
18 Z Bilgi – Szammua, z Szemajasza – Jonatan;
Shamua alikuwa kiongozi wa Bilgai, Yehonathani alikuwa kiongozi wa Shemaya,
19 A z Jojariba – Mattenaj, z Jedajasza – Uzzi;
Matenai alikuwa kiongozi wa Yoyaribu, Uzi alikuwa kiongozi wa Yedaya,
20 Z Sallaj – Kallaj, z Amoka – Eber;
Kalai alikuwa kiongozi wa Salu, Eberi alikuwa kiongozi wa Amok,
21 Z Chilkiasza – Chaszabiasz, z Jedajasza – Netanaeel.
Hashabia alikuwa kiongozi wa Hilkia, na Nethanel alikuwa kiongozi wa Yedaya.
22 Za dni Eliasziba, Jojady, Jochanana i Jadduy Lewici zostali spisani jako naczelnicy rodów, a także kapłani, aż do panowania Dariusza Persa.
Katika siku za Eliashibu, Walawi Eliashibu, Yoyada, Yohana, na Yadua waliandikwa kama vichwa vya familia, na makuhani waliandikwa wakati wa utawala wa Dariyo wa Persia.
23 Synowie Lewiego, naczelnicy rodów, [zostali] spisani w księdze kronik aż do dni Jochanana, syna Eliasziba.
Wana wa Lawi na viongozi wao wa familia waliandikwa katika Kitabu cha tarehe hadi siku za Yohana mwana wa Eliashibu.
24 Naczelnikami Lewitów [byli]: Chaszabiasz, Szerebiasz, Jeszua, syn Kadmiela, i ich bracia, którzy stali naprzeciw nich, straż przy straży, aby chwalić i dziękować, według rozkazu Dawida, męża Bożego.
Wakuu wa Walawi walikuwa Hashabia, Sherebia, na Yeshua mwana wa Kadmieli, pamoja na washirika wao, waliokuwa wamesimama mbele yao kumtukuza na kumshukuru, akijibu sehemu kwa sehemu, kwa kutii amri ya Daudi, mtu wa Mungu.
25 Mattaniasz i Bakbukiasz, Obadiasz, Meszullam, Talmon i Akkub [jako] odźwierni trzymali straż przy składnicach u bram.
Matania, Bakbukia, Obadiya, Meshulamu, Talmoni na Akubu walikuwa walinzi wa malango waliokuwa wakiwa wamesimama katika vyumba vya hazina penye malango.
26 Ci [żyli] za dni Jojakima, syna Jeszuy, syna Jocadaka, i za dni namiestnika Nehemiasza i Ezdrasza, kapłana i uczonego w Piśmie.
Walitumika katika siku za Yoyakimu, mwana wa Yoshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za Nehemiya, gavana na Ezra kuhani na mwandishi.
27 I na poświęcanie muru Jerozolimy odszukano Lewitów ze wszystkich ich miejsc, aby ich przyprowadzić do Jerozolimy, by mogli obchodzić poświęcenie z radością, dziękczynieniem, przy śpiewaniu, cymbałach, cytrach i harfach.
Katika kujitolea kwa ukuta wa Yerusalemu, watu walitafuta Walawi popote walipokuwa wakiishi, wakawaleta Yerusalemu ili kusherehekea kujitolea kwa furaha, pamoja na shukrani na kuimba kwa ngoma, vinanda na vinubi.
28 Zgromadzili się więc synowie śpiewaków, z równin wokół Jerozolimy i ze wsi Netofatytów;
Ushirika wa waimbaji walikusanyika pamoja kutoka wilaya iliyozunguka Yerusalemu na kutoka vijiji vya Wanetofathi.
29 Także z domu Gilgal, z pól Geba i z Azmawet. Śpiewacy bowiem zbudowali sobie wsie wokół Jerozolimy.
Walikuja kutoka Beth-gilgali na kutoka katika mashamba ya Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji karibu na Yerusalemu.
30 Wtedy kapłani i Lewici oczyścili się, po czym oczyścili też lud, bramy i mur.
Makuhani na Walawi wakajitakasa, kisha wakawatakasa watu, milango na ukuta.
31 Następnie kazałem przełożonym Judy wstąpić na mur i ustawiłem dwa wielkie zespoły dziękczynne, z których [jeden] szedł po murze na prawo, w kierunku Bramy Gnojnej.
Kisha nilikuwa na viongozi wa Yuda kwenda juu ya ukuta, na mimi kuteua mikutano miwili mikubwa ya hao walioshukuru. Mmoja alienda upande wa kulia juu ya ukuta kuelekea lango la jaa.
32 Za nim szedł Hoszajasz i połowa przełożonych Judy;
Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda walimfuata,
33 Także Azariasz, Ezdrasz i Meszullam;
na baada yake akaenda Azaria, Ezra na Meshulamu,
34 Juda, Beniamin, Szemajasz i Jeremiasz;
Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia
35 Potem [szli] z trąbami niektórzy z synów kapłanów, [mianowicie]: Zachariasz, syn Jonatana, syna Szemajasza, syna Mattaniasza, syna Michajasza, syna Zakkura, syna Asafa;
na wana wa makuhani waliokuwa na tarumbeta, na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Mataniya, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu.
36 I jego bracia: Szemajasz, Azarel, Milalaj, Gilalaj, Maaj, Netaneel, Juda, Chanani z instrumentami muzycznymi Dawida, męża Bożego, a Ezdrasz, uczony w Piśmie, [szedł] przed nimi.
Na pia jamaa za Zekaria, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda, Hanani, pamoja na vyombo vya muziki vya Daudi mtu wa Mungu. Ezra mwandishi alikuwa mbele yao.
37 Następnie przy Bramie Źródlanej, która [była] naprzeciw nich, szli po schodach miasta Dawida, które prowadzą na mur, znad domu Dawida aż do Bramy Wodnej na wschodzie.
Na kwa Lango la Chemchemi walikwenda moja kwa moja na madaraja ya mji wa Daudi juu ya kupanda kwa ukuta, juu ya nyumba ya Daudi, kwenye lango la Maji upande wa mashariki.
38 A drugi zespół dziękczynny, a ja za nim, szedł po murze w lewo z drugą połową [przełożonych], od Wieży Pieców aż do Muru Szerokiego;
Na waimbaji wengine ambao walishukuru wakaenda upande mwingine. Niliwafuata juu ya ukuta pamoja na nusu ya watu, juu ya mnara wa vinyago, hadi kuta kubwa,
39 I znad Bramy Efraima, nad Bramą Starą, nad Bramą Rybną, obok Wieży Chananeela i Wieży Mea, aż do Bramy Owczej. I stanęli u Bramy Więziennej.
na juu ya lango la Efraimu, na mlango wa kale, na kwa lango la samaki na mnara wa Hananeli na mnara wa Hamea, kwa lango la Kondoo, na wakasimama kwenye mlango wa walinzi.
40 A tak stanęły oba zespoły dziękczynne w domu Bożym, a wraz z nimi ja i połowa przełożonych ze mną.
Kwa hiyo, mikutano miwili ya wale waliomshukuru walipata nafasi yao katika nyumba ya Mungu, na mimi pia nikachukua nafasi yangu na nusu ya viongozi pamoja nami.
41 Także kapłani: Eliakim, Maasejasz, Miniamin, Michajasz, Elioenaj, Zachariasz, Chananiasz, z trąbami;
Na makuhani wakachukua nafasi zao Eliakimu, Maaseya, Miyamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria, na Hanania wenye tarumbeta,
42 I Maasejasz, Szemajasz, Eleazar, Uzzi, Jehochanan, Malkiasz, Elam i Ezer. Śpiewacy głośno śpiewali, a Jizrachiasz był [ich] kierownikiem.
Maaseya, na Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu, Ezeri. Waimbaji waliimba na Yezrahia kama wasimamizi.
43 Tego dnia składali także wielkie ofiary i radowali się. Bóg bowiem dał im wielką radość. Również kobiety i dzieci radowały się, a radość Jerozolimy słychać było z daleka.
Walitoa dhabihu kubwa siku ile, wakafurahi, kwa sababu Mungu alikuwa amewafurahisha kwa furaha kubwa. Pia wanawake na watoto walifurahi. Hivyo furaha ya Yerusalemu ikasikiwa toka mbali.
44 W tym czasie ustanowiono mężczyzn nad składnicami dla skarbów, ofiar, pierwocin i dziesięcin, aby w nich zgromadzono dla kapłanów i Lewitów udziały przyznane im przez Prawo z pól miejskich. Juda bowiem cieszył się z powodu kapłanów i Lewitów pełniących służbę;
Siku hiyo watu waliteuliwa juu ya nyumba ya hazina kwa ajili ya michango, matunda ya kwanza, na zaka, ili kuzikusanya ndani yao sehemu zinazohitajika katika sheria za makuhani na Walawi. Kila mmoja aliteuliwa kufanya kazi mashambani karibu na miji. Kwa maana Yuda alifurahi juu ya makuhani na Walawi waliokuwa wamesimama mbele yao.
45 I śpiewacy i odźwierni pełnili służbę dla swego Boga i służbę oczyszczenia, według rozkazu Dawida [i] jego syna Salomona.
Walifanya utumishi wa Mungu wao, na huduma ya utakaso, kwa mujibu wa amri ya Daudi na ya mwanawe Sulemani, na hivyo
46 Już bowiem dawno, za dni Dawida i Asafa, [byli ustanowieni] przełożeni nad śpiewakami oraz [były ustalone] pieśni pochwalne i dziękczynienia dla Boga.
Zamani za kale, katika siku za Daudi na Asafu, kulikuwa na wasimamizi wa waimbaji, na kulikuwa na nyimbo za sifa na shukrani kwa Mungu.
47 Cały Izrael więc za dni Zorobabela i za dni Nehemiasza dawał porcje śpiewakom i odźwiernym na codzienne utrzymanie. Oddawali Lewitom to, co poświęcili, Lewici zaś oddawali [to] synom Aarona.
Katika siku za Zerubabeli na katika siku za Nehemia, Israeli wote walitoa sehemu za kila siku kwa waimbaji na walinzi wa mlango. Wakaweka pembeni sehemu ya Walawi, na Walawi waliweka sehemu ya wana wa Haruni.

< Nehemiasza 12 >