< Księga Sędziów 10 >

1 Po Abimeleku powstał, aby bronić Izraela, Tola, syn Puy, syna Doda, mężczyzna z [pokolenia] Issachara. Mieszkał on w Szamir, na górze Efraim.
Baada ya Abimeleki, Tola mwana wa Pua mwana wa Dodo, mtu wa Isakari, aliyeishi huko Shamiri, katika nchi ya vilima ya Efraimu, akainuka kuokoa Israeli.
2 Sądził on Izraela przez dwadzieścia trzy lata, po czym umarł i został pogrzebany w Szamir.
Akaamua Israeli kwa miaka ishirini na mitatu. Ndipo akafa, naye akazikwa huko Shamiri.
3 A po nim powstał Jair Gileadczyk, który sądził Izraela przez dwadzieścia dwa lata.
Baada yake akafuatiwa na Yairi, Mgileadi, ambaye aliamua Israeli kwa miaka ishirini na miwili.
4 Miał on trzydziestu synów, którzy jeździli na trzydziestu oślętach, a mieli trzydzieści miast zwanych do dziś Chawot-Jair, a [są one] w ziemi Gilead.
Alikuwa na wana thelathini waliopanda punda thelathini. Nao walikuwa na miji thelathini iliyoko Gileadi, inayoitwa Hawoth-Yairi mpaka leo.
5 Umarł Jair i został pogrzebany w Kamon.
Yairi akafa, naye akazikwa huko Kamoni.
6 A synowie Izraela znowu czynili to, co złe w oczach PANA, służąc Baalom i Asztartom, bogom Syrii, bogom Sydonu, bogom Moabu, bogom synów Ammona i bogom filistyńskim, a opuścili PANA i nie służyli mu.
Wana wa Israeli wakatenda tena maovu machoni pa Bwana. Wakaabudu Mabaali na Maashtorethi, miungu ya Aramu, miungu ya Sidoni, miungu ya Moabu, miungu ya Waamoni na miungu ya Wafilisti. Kwa kuwa Waisraeli walimwacha Bwana wala hawakuendelea kumtumikia,
7 Dlatego gniew PANA zapłonął przeciw Izraelowi i wydał ich w ręce Filistynów oraz w ręce synów Ammona.
hivyo hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Israeli, naye akawatia mikononi mwa Wafilisti na Waamoni,
8 Oni trapili i uciskali synów Izraela od tego roku przez osiemnaście lat – wszystkich synów Izraela, którzy byli za Jordanem w ziemi Amorytów, która jest w Gileadzie.
ambao waliwaonea na kuwatesa mwaka ule. Kwa miaka kumi na minane wakawatesa Waisraeli wote upande wa mashariki ya Mto Yordani katika Gileadi, nchi ya Waamori.
9 Synowie Ammona przeprawili się też za Jordan, aby walczyć z Judą i Beniaminem, a także z domem Efraima, i Izrael był bardzo uciskany.
Waamoni nao wakavuka Yordani ili kupigana na Yuda, Benyamini na nyumba ya Efraimu, nayo nyumba ya Israeli ikawa katika taabu kubwa.
10 Wtedy synowie Izraela wołali do PANA: Zgrzeszyliśmy przeciw tobie, bo opuściliśmy naszego Boga, a służyliśmy Baalom.
Ndipo Waisraeli wakamlilia Bwana wakasema, “Tumetenda dhambi dhidi yako, kumwacha Mungu wetu na kutumikia Mabaali.”
11 I PAN powiedział do synów Izraela: Czy [nie wybawiłem] was od Egipcjan, od Amorytów, od synów Ammona i od Filistynów?
Bwana akawaambia, “Wakati Wamisri, Waamori, Waamoni, Wafilisti,
12 I od Sydończyków, Amalekitów i Mahanitów, którzy was gnębili? Gdy wołaliście do mnie, czy nie wybawiłem was z ich rąk?
Wasidoni, Waamaleki na Wamaoni walipowaonea na ninyi mkanililia na kuomba msaada, je, sikuwaokoa kutoka mikononi mwao?
13 Lecz wy mnie opuściliście i służyliście obcym bogom. Dlatego już was więcej nie wybawię.
Lakini ninyi mmeniacha mimi na kutumikia miungu mingine, kwa hiyo sitawaokoa tena.
14 Idźcie i wołajcie do bogów, których sobie wybraliście. Niech oni was wybawią w czasie waszego ucisku.
Nendeni mkaililie ile miungu mlioichagua. Hiyo miungu na iwaokoe mnapokuwa katika taabu!”
15 Synowie Izraela odpowiedzieli PANU: Zgrzeszyliśmy. Uczyń z nami, co wydaje się dobre w twoich oczach, tylko wybaw nas, prosimy, dzisiaj.
Lakini Waisraeli wakamwambia Bwana, “Tumetenda dhambi. Ututendee lile unaloona kuwa jema kwako, lakini twakusihi utuokoe sasa.”
16 Wyrzucili więc obcych bogów spośród siebie i służyli PANU, a [PAN] wzruszył się niedolą Izraela.
Nao wakaiondoa hiyo miungu migeni katikati yao nao wakamtumikia Bwana. Naye akahuzunika kwa sababu ya taabu ya Israeli.
17 Tymczasem synowie Ammona zebrali się i rozbili obóz w Gileadzie. Także synowie Izraela zebrali się i rozbili obóz w Mispie.
Ndipo Waamoni wakaitwa vitani na kupiga kambi huko Gileadi, Waisraeli wakakusanyika na kupiga kambi huko Mispa.
18 Wtedy lud i przełożeni Gileadu mówili między sobą: Kto pierwszy podejmie walkę z synami Ammona, ten stanie na czele wszystkich mieszkańców Gileadu.
Viongozi wa watu wa Gileadi wakaambiana wao kwa wao, “Yeyote yule atakayeanzisha mashambulizi dhidi ya Waamoni atakuwa kiongozi wa wote wakaao Gileadi.”

< Księga Sędziów 10 >