< Rzymian 9 >

1 Prawdę mówię w Chrystusie, a nie kłamię, w czem mi poświadcza sumienie moje przez Ducha Świętego:
Nasema ukweli mtupu; nimeungana na Kristo nami sisemi uongo. Dhamiri yangu ikiongozwa na Roho Mtakatifu inanithibitishia jambo hili pia.
2 Że mam wielki smutek i nieustawający ból w sercu mojem.
Nataka kusema hivi: nina huzuni kubwa na maumivu yasiyopimika moyoni mwangu
3 Albowiem żądałbym sam, abym się stał odłączonym od Chrystusa za braci moich, za pokrewnych moich według ciała.
kwa ajili ya watu wangu, walio damu moja nami! Kama ingekuwa kwa faida yao, ningekuwa radhi kulaaniwa na kutengwa na Kristo.
4 Którzy są Izraelczycy, których jest przysposobienie synowskie i chwała, i przymierza, i zakonu danie, i służba Boża, i obietnice;
Hao ndio watu wa Israeli ambao Mungu aliwateua wawe watoto wake, akawashirikisha utukufu wake; aliagana nao, akawapa Sheria yake, imani ya kweli na ahadi zake.
5 Których są ojcowie i z których poszedł Chrystus ile według ciała, który jest nad wszystkimi Bóg błogosławiony na wieki. Amen. (aiōn g165)
Wao ni wajukuu wa mababu, naye Kristo, kadiri ya ubinadamu wake, ametoka katika ukoo wao. Mungu atawalaye juu ya yote, na atukuzwe milele! Amina. (aiōn g165)
6 Lecz nie można, żeby miało upaść słowo Boże; albowiem nie wszyscy, którzy są z Izraela, są Izraelem;
Sisemi kwamba ahadi ya Mungu imebatilika; maana si watu wote wa Israeli ni wateule wa Mungu.
7 Ani iż są nasieniem Abrahamowem, wszyscy są dziećmi; ale rzeczono: W Izaaku będzie tobie nazwane nasienie;
Wala, si wazawa wote wa Abrahamu ni watoto wake wa kweli. Ila, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Wazao wake watatokana na Isaka.”
8 To jest, nie dzieci ciała są dziećmi Bożymi; ale dzieci obietnicy bywają w nasienie policzone.
Nido kusema, wale waliozaliwa kimaumbile ndio watoto wa Mungu, bali wale waliozaliwa kutokana na ahadi ya Mungu ndio watakaoitwa watoto wake.
9 Albowiem obietnicy słowo to jest: O tym właśnie czasie przyjdę, a Sara będzie miała syna;
Maana ahadi yenyewe ni hii: “Nitakujia wakati maalum, naye Sara atapata mtoto.”
10 A nie tylko to, ale i Rebeka, gdy z jednego ojca naszego Izaaka brzemienną została.
Tena si hayo tu ila pia Rebeka naye alipata mapacha kwa baba mmoja, yaani Isaka, babu yetu.
11 Gdy się jeszcze były dziatki nie narodziły, ani co dobrego albo złego uczyniły, aby się ostało postanowienie Boże według wybrania, nie z uczynków, ale z tego, który powołuje,
Lakini, ili Mungu aonekane kwamba anao uhuru wa kuchagua, hata kabla wale ndugu hawajazaliwa na kabla hawajaweza kupambanua jema na baya,
12 Rzeczono jej, że większy będzie służył mniejszemu;
Rebeka aliambiwa kwamba yule mtoto wa kwanza atamtumikia yule wa nyuma. Hivyo uchaguzi wa Mungu unategemea jinsi anavyoita mwenyewe, na si matendo ya binadamu.
13 Jako napisano: Jakóbam umiłował, alem Ezawa miał w nienawiści.
Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Yakobo nilimpenda, lakini Esau nilimchukia.”
14 Cóż tedy rzeczemy? Jestże niesprawiedliwość u Boga? Nie daj tego Boże!
Basi, tuseme nini? Je, Mungu amekosa haki? Hata kidogo!
15 Albowiem do Mojżesza mówi: Zmiłuję się, nad kim się zmiłuję; a zlituję się, nad kim się zlituję.
Maana alimwambia Mose: “Nitamhurumia mtu yeyote ninayetaka kumhurumia; nitamwonea huruma mtu yeyote ninayetaka.”
16 A przetoż nie zależy na tym co chce, ani na tym, co bieży, ale na Bogu, który się zmiłowywa.
Kwa hiyo, yote hutegemea huruma ya Mungu, na si bidii au mapenzi ya mtu.
17 Albowiem mówi Pismo do Faraona: Na tom cię samo wzbudził, abym okazał moc moję na tobie, a iżby opowiadane było imię moje po wszystkiej ziemi.
Maana Maandiko Matakatifu yasema hivi kwa Farao: “Nilikufanya mfalme ili kwa njia yako, uwezo wangu ujulikane, na jina langu litangazwe popote duniani.”
18 A tak nad kim chce, zmiłowywa się, a kogo chce, zatwardza.
Ni wazi, basi, kwamba Mungu humhurumia yeyote anayetaka kumhurumia, na akipenda kumfanya mtu awe mkaidi, hufanya hivyo.
19 Ale mi rzeczesz: Przeczże się jeszcze uskarża? bo któż się sprzeciwił woli jego?
Labda utaniuliza: “Ikiwa mambo yako hivyo, Mungu anawezaje kumlaumu mtu? Nani awezaye kuyapinga mapenzi yake?”
20 I owszem, o człowiecze! któżeś ty jest, który spór wiedziesz z Bogiem? Izali lepianka rzecze lepiarzowi: Przeczżeś mię tak uczynił?
Lakini, ewe binadamu, u nani hata uthubutu kumhoji Mungu? Je, chungu chaweza kumwuliza mfinyanzi wake: “Kwa nini umenitengeneza namna hii?”
21 Izali nie ma mocy garncarz nad gliną, żeby z tejże gliny uczynił jedno naczynie ku uczciwości, a drugie ku zelżywości?
Mfinyanzi anaweza kuutumia udongo apendavyo na kufinyanga vyungu viwili kwa udongo uleule; kimoja kwa matumizi ya heshima, na kingine kwa matumizi ya kawaida.
22 A jeźliż Bóg chcąc okazać gniew i znajomą uczynić możność swoję, znosił w wielkiej cierpliwości naczynia gniewu na zginienie zgotowane,
Hivyo ndivyo ilivyo kwa Mungu. Alitaka kuonyesha ghadhabu yake na kujulisha uwezo wake, Basi, alikuwa na saburi sana, akiwavumilia wale ambao walikuwa lengo la ghadhabu yake, ambao walistahili kuangamizwa.
23 A iżby znajome uczynił bogactwo chwały swojej nad naczyniem miłosierdzia, które zgotował ku chwale;
Alitaka pia kudhihirisha wingi wa utukufu wake ambao alitumiminia sisi tulio lengo la huruma yake; sisi ambao alikwisha kututayarisha kuupokea utukufu wake.
24 Których i powołał, to jest nas, nie tylko z Żydów, ale i z poganów.
Maana sisi ndio hao aliowaita, si tu kutoka miongoni mwa Wayahudi bali pia kutoka kwa watu wa mataifa mengine.
25 Jako też u Ozeasza mówi: Nazwię lud, który nie był moim, ludem moim, a onę, która nie była umiłowaną, nazwię umiłowaną.
Maana ndivyo asemavyo katika kitabu cha Hosea: “Wale waliokuwa Si watu wangu nitawaita: Watu wangu! Naye Sikupendi ataitwa: Mpenzi wangu!
26 I stanie się, że na tem miejscu, gdzie im mawiano: Nie jesteście wy ludem moim, tam nazwani będą synami Boga żywego.
Na pale walipoambiwa: Ninyi si wangu hapo wataitwa: Watoto wa Mungu hai.”
27 A Izajasz woła nad Izraelem, mówiąc: Choćby liczba synów Izraelskich była jako piasek morski, ostatki zachowane będą.
Naye nabii Isaya, kuhusu Israeli anapaaza sauti: “Hata kama watoto wa Israeli ni wengi kama mchanga wa pwani, ni wachache tu watakaookolewa;
28 Albowiem sprawę skończy i skróci w sprawiedliwości; sprawę zaiste skróconą uczyni Pan na ziemi.
maana, Bwana ataitekeleza upesi hukumu yake kamili juu ya ulimwengu wote.”
29 I jako przedtem powiedział Izajasz: By nam był Pan zastępów nie zostawił nasienia, bylibyśmy się stali jako Sodoma i Gomorze bylibyśmy podobni.
Ni kama Isaya alivyosema hapo awali: “Kama Bwana Mwenye Nguvu asingalituachia baadhi ya watoto wa Israeli, tungalikwisha kuwa kama Sodoma, tungalikwisha kuwa ma Gomora.”
30 Cóż tedy rzeczemy? To, iż poganie, którzy nie szukali sprawiedliwości, dostąpili sprawiedliwości, a sprawiedliwości, która jest z wiary.
Basi, tuseme nini? Ni hivi: watu wa mataifa ambao hawakutafuta kukubaliwa kuwa waadilifu, wamekubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani,
31 A Izrael szukając zakonu sprawiedliwości, nie doszedł zakonu sprawiedliwości.
hali watu wa Israeli waliokuwa wakitafuta Sheria iletayo kukubaliwa kuwa waadilifu, hawakuipata.
32 Dlaczegoż? Iż nie z wiary, ale jako z uczynków zakonu jej szukali; albowiem się obrazili o kamień obrażenia,
Kwa nini? Kwa sababu walitegemea matendo yao badala ya kutegemea imani. Walijikwaa juu ya jiwe la kujikwaa
33 Jako napisano: Oto kładę w Syonie kamień obrażenia i opokę otrącenia, a wszelki, który w niego wierzy, nie będzie pohańbiony.
kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: “Tazama! Naweka huko Sioni jiwe likwazalo, mwamba utakaowafanya watu waanguke. Mtu atakayemwamini yeye aliye hilo jiwe, hataaibishwa!”

< Rzymian 9 >