< Księga Sędziów 5 >

1 I śpiewała Debora i Barak, syn Abinoemów, dnia onego, mówiąc:
Ndipo Debora na Baraka mwana wa Abinoamu wakaimba wimbo huu:
2 Dla pomsty uczynionej w Izraelu, a iż się na to dobrowolnie lud ofiarował, błogosławcie Pana.
“Wakuu katika Israeli wanapoongoza, wakati watu wanapojitoa kwa hiari yao wenyewe: mhimidini Bwana!
3 Słuchajcie królowie, bierzcie w uszy książęta, ja, ja Panu zaśpiewam, śpiewać będę Panu, Bogu Izraelskiemu.
“Sikieni hili, enyi wafalme! Sikilizeni, enyi watawala! Nitamwimbia Bwana, nitaimba; kwa wimbo nitamhimidi Bwana, Mungu wa Israeli.
4 Panie, gdyś wyszedł z Seir, a przechodziłeś przez pole Edom, ziemia się wzruszyła, nieba też kropiły, a obłoki wydawały wody.
“Ee Bwana, ulipotoka katika Seiri, ulipopita katika mashamba ya Edomu, nchi ilitetemeka, mbingu nazo zikamwaga, naam, mawingu yakamwaga maji.
5 Góry się rozpłynęły od oblicza Pańskiego, a góra Synaj od oblicza Pana, Boga Izraelskiego.
Milima ilitetemeka mbele za Bwana, hata ule wa Sinai, mbele za Bwana, Mungu wa Israeli.
6 Za dni Samgara, syna Anatowego, i za dni Jaeli zaginęły ścieżki, a którzy szli w drogę, chodzili ścieżkami krzywemi.
“Katika siku za Shamgari mwana wa Anathi, katika siku za Yaeli, barabara kuu hazikuwa na watu; wasafiri walipita njia za kando.
7 Spustoszały wsi w Izraelu, spustoszały, ażem powstała ja Debora, ażem powstała matką w Izraelu.
Mashujaa walikoma katika Israeli, walikoma mpaka mimi, Debora, nilipoinuka, nilipoinuka kama mama katika Israeli.
8 Gdy Izrael obierał sobie bogi nowe, tedy bywała wojna w bramach; tarczy jednak nie było widać, ani drzewca między czterdziestą tysięcy w Izraelu.
Walipochagua miungu migeni, vita vilikuja katika malango ya mji, hapakuonekana ngao wala mkuki miongoni mwa mashujaa 40,000 katika Israeli.
9 Serce moje nakłonione do książąt Izraelskich. Ochotni z ludu błogosławcież Pana.
Moyo wangu u pamoja na wakuu wa Israeli, pamoja na wale wanaojitoa wenyewe kwa hiari yao miongoni mwa watu. Mhimidini Bwana!
10 Którzy jeździcie na oślicach białych, i zasiadacie na sądach, i którzy chodzicie po drogach, rozmawiajcie z sobą,
“Nanyi mpandao punda weupe, mkiketi juu ya matandiko ya thamani, nanyi mtembeao barabarani, fikirini
11 Że ucichł trzask strzelców między miejscami, gdzie czerpią wodę; tam niech opowiadają sprawiedliwości Pańskie, sprawiedliwości we wsiach jego w Izraelu; tedy zstąpi do bram lud Pański.
juu ya sauti za waimbaji mahali pa kunyweshea maji. Wanasimulia matendo ya haki ya Bwana, matendo ya haki ya mashujaa wake katika Israeli. “Ndipo watu wa Bwana walipoteremka malangoni pa mji.
12 Powstań Deboro, powstań, powstań, a zaśpiewaj pieśń; powstań Baraku, a pojmaj więźnie twoje, synu Abinoemów.
‘Amka, amka! Debora! Amka, amka, uimbe! Ee Baraka! Inuka, chukua mateka wako uliowateka, ee mwana wa Abinoamu.’
13 Teraz panować będzie potłoczony nad możnymi z ludu; Pan dopomógł mi panować nad mocarzami.
“Ndipo mabaki ya watu wakashuka dhidi ya wenye nguvu, watu wa Bwana, wakashuka dhidi ya mashujaa wenye nguvu.
14 Z Efraima wyszedł korzeń ich przeciw Amalekowi, za tobą (Efraimie, ) Benjamin między ludem twoim; z Machyru wyszli zakonodawcy, a z Zabulonu pisarze.
Kutoka Efraimu wakaja watu, ambao chimbuko lao ni Amaleki; Benyamini akiwa miongoni mwa watu waliokufuata. Kutoka Makiri wakashuka viongozi, na kutoka Zabuloni wale washikao fimbo ya jemadari.
15 Książęta też Isaschar były z Deborą; Isaschar też jako i Barak w dolinę posłan jest pieszo; ale w dziale Rubenitów byli ludzie wysokich myśli.
Wakuu wa Isakari walikuwa pamoja na Debora; naam, Isakari alikuwa pamoja na Baraka, wakija nyuma yake kwa mbio wakielekea bondeni. Katika jamaa za Reubeni, palikuwa na kujihoji kukubwa moyoni.
16 Czemuś siedział między dwiema oborami, słuchając wrzasku trzód? w dziale Rubenitów byli ludzie wysokich myśli.
Kwa nini ulikaa katikati ya mazizi ya kondoo kusikiliza sauti ya filimbi zinazoita makundi? Kwa jamaa za Reubeni, palikuwa na kujihoji kukubwa moyoni.
17 Galaad za Jordanem odpoczynął, a Dan przecz się bawił okrętami? Aser czemu siedział na brzegu morskim, a w skałach swoich mieszkał?
Gileadi alikaa ngʼambo ya Yordani. Naye Dani, kwa nini alikaa kwenye merikebu siku nyingi? Asheri alikaa kwa utulivu ufuoni mwa bahari, akikaa kwenye ghuba zake ndogo.
18 Zabulon jest lud, który wydał duszę swą na śmierć, także i Neftalim, a to na wysokich polach.
Watu wa Zabuloni walihatarisha maisha yao, vilevile nao watu wa Naftali.
19 Przyszli królowie, walczyli; na ten czas walczyli królowie Chananejscy w Tanach u wód Magieddo, jednak korzyści srebra nie odnieśli.
“Wafalme walikuja na kufanya vita; wafalme wa Kanaani walipigana huko Taanaki karibu na maji ya Megido, lakini hawakuchukua fedha wala nyara.
20 Z nieba walczono: gwiazdy z miejsc swoich walczyły z Sysarą.
Kutoka mbinguni nyota zilipigana, nyota kutoka njia zake zilipigana na Sisera.
21 Potok Cyson porwał je, potok Kiedumim, potok Cyson; podeptałaś, o duszo moja, możne.
Mto wa Kishoni uliwasomba, ule mto wa zamani, mto wa Kishoni. Songa mbele, ee nafsi yangu, kwa ujasiri!
22 Tedy się popadały kopyta końskie od wielkiego tąpania mocarzów jego.
Ndipo kwato za farasi zikafanya mshindo: farasi wake wenye nguvu huenda mbio kwa kurukaruka.
23 Przeklinajcie Meroz, rzekł Anioł Pański, przeklinajcie przeklinając obywatele jego; albowiem nie przyszli na ratunek Panu, na ratunek Panu z mocarzami.
Malaika wa Bwana akasema, ‘Merozi alaaniwe. Walaaniwe watu wake kwa uchungu, kwa kuwa hawakuja kumsaidia Bwana, kumsaidia Bwana dhidi ya hao wenye nguvu.’
24 Błogosławiona między niewiastami Jael, żona Hebera Cynejczyka; nad niewiasty w namiocie mieszkające błogosławiona będzie.
“Yaeli abarikiwe kuliko wanawake wote, mkewe Heberi, Mkeni, abarikiwe kuliko wanawake wote waishio kwenye mahema.
25 Prosił o wodę, a ona mleka dała, a na przystawce książęcej przyniosła masła.
Aliomba maji, naye akampa maziwa; kwenye bakuli la heshima akamletea maziwa mgando.
26 Lewą rękę swą do gwoździa ściągnęła, a prawicę swoję do młota kowalskiego, i uderzyła Sysarę, przebiła głowę jego, i przeraziła, i przekłuła skronie jego.
Akanyoosha mkono wake akashika kigingi cha hema, mkono wake wa kuume ukashika nyundo ya fundi. Akampiga Sisera kwa nyundo, akamponda kichwa chake, akamvunjavunja na kumtoboa paji lake la uso.
27 U nóg jej skurczył się, padł, leżał; u nóg jej skurczył się, padł; kędy się skurczył, tam upadł zabity.
Aliinama miguuni pa Yaeli, akaanguka; akalala hapo. Pale alipoinama miguuni pake, alianguka; pale alipoinamia, ndipo alipoanguka, akiwa amekufa.
28 Oknem wyglądała, a wołała matka Sysary przez kratę: Przeczże omieszkiwa wrócić się wóz jego? przecz się nie spieszą nogi woźników jego?
“Kupitia dirishani mamaye Sisera alichungulia; nyuma ya dirisha alilia, akasema, ‘Mbona gari lake linachelewa kufika? Mbona vishindo vya magari yake vimechelewa?’
29 Przedniejsze i mędrsze niewiasty odpowiedziały, jako też i sama sobie odpowiadała:
Wanawake wenye busara kuliko wengine wote wakamjibu; naam, husema moyoni mwake,
30 Snać trafili na łup, i dzielą go? Panienka jedna albo dwie dostaną się mężowi jednemu; łupy rozlicznych barw oddawają Sysarze, a łupy pstro haftowane, i łupy pstro z obu stron tkane dostawają się na szyję łupy biorących.
‘Je, hawapati na kugawanya nyara: msichana mmoja au wawili kwa kila mtu, mavazi ya rangi mbalimbali kwa Sisera kuwa nyara, mavazi ya rangi mbalimbali yaliyotariziwa, mavazi yaliyotariziwa vizuri kwa ajili ya shingo yangu: yote haya yakiwa nyara?’
31 Tak niechaj zginą wszyscy nieprzyjaciele twoi, Panie, a ci, którzy ciebie miłują, niech będą jako słońce, gdy wschodzi w mocy swojej. I była w pokoju ziemia przez czterdzieści lat.
“Adui zako wote na waangamie, Ee Bwana! Bali wote wakupendao na wawe kama jua lichomozavyo kwa nguvu zake.” Hivyo nchi ikawa na amani kwa miaka arobaini.

< Księga Sędziów 5 >