< Jozuego 19 >

1 Potem padł los wtóry Symeonowi, pokoleniu synów Symeonowych według domów ich, a było dziedzictwo ich w pośród dziedzictwa synów Judowych.
Upigaji wa pili wa kura uliangukia kwa Simoni na waligawiwa kwa kila ukoo wao. Urithi wao ulikuwa katikati ya urithi ulikuwa ni mali ya kabila la Yuda.
2 A dostało się im w dziedzictwo ich Beerseba, i Seba, i Molada;
Urithi waliokuwa nao ni Beerisheba, Sheba, Molada,
3 I Hasersual, i Bala, i Asem;
Hazari Shuali, Bala, Ezemu,
4 I Etolat, i Betul, i Horma;
Elitoladi, Bethuli na Horma.
5 I Syceleg, i Bet Marchabot, i Hasersusa,
Simoni alikuwa pia na Ziklagi, Bethi Markabothi, Hazari Susa,
6 I Betlebaot, i Serohem, i trzynaście miast, i wsi ich;
Bethi Lebaothi, na Sharuheni. Kulikuwa na miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake. Vile vile
7 Ain, Remmon, i Atar, i Asan, miasta cztery, i wsi ich;
Simoni alimiliki Aini, Rimon, Etheri, na Ashani. Hii ilikuwa ni miji minne pamoja na vijiji vyake.
8 I wszystkie wsi, które były około tych miast, aż do Baalatbeer, i Ramat ku stronie południowej. Toć jest dziedzictwo pokolenia synów Symeonowych według domów ich.
Miji hii pamoja na vijiji vilivyoizunguka hata kufika Baalathi Beeri (ambao ndio Rama katika Negevu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simoni, waliopewa kwa koo zao.
9 Z działu synów Judowych dostało się dziedzictwo synom Symeonowym, bo dział synów Judowych był wielki dla nich; przetoż wzięli dziedzictwo synowie Symeonowi pośród dziedzictwa ich.
Urithi wa kabila la Simoni ulikuwa sehemu ya himaya ya kabila la Yuda. Hii ni kwasababu nchi waliyopewa kabila la Yuda ilikuwa ni kubwa kwao, na hivyo kabila la Simoni lilipokea urithi wao kutoka katika sehemu yao ya katikati.
10 Potem padł los trzeci synom Zabulonowym według domów ich, a jest granica dziedzictwa ich.
Upigaji wa kura ya tatu uliangukia kwa kabila la Zabuloni, na walipewa kwa koo zao. Mpaka wa urithi wao ulianzia huko Saridi.
11 A idzie granica ich morza Marala, i przychodzi do Debbaset, ciągnąc się aż do potoku, który jest przeciw Jeknoam.
Mpaka wao ulipanda upande wa magharibi kuelekea Marala na ukaigusa Dabeshethi, na kisha ukasonga kuelekea kijito kilichokuwa mkabala na Yokineamu.
12 I wraca się od Saryd na wschód słońca ku granicy Chasalek Tabor, a stamtąd bieży do Daberet, i ciągnie się do Jafije;
Kutoka Saridi mpaka ulizunguka upande wa mashariki kuelekea mashariki na ulienda hadi mpaka wa Kislothi Tabori. Kutoka hapo uliendelea hadi Daberathi na kisha ulipanda hata Yafia.
13 Potem stamtąd bieży na wschód słońca do Gethefer i do Itakasyn, a wychodzi w Rymmon, i kołem idzie do Nehy.
Kutoka hapo ulipita katika upande wa mashariki mwa Gathi Heferi, na kisha ukafika Ethikazini, baadaye ulienda hadi Rimoni na kisha ukageuka kuelekea Nea.
14 Idzie także kołem taż granica od północy ku Hannaton, a kończy się u doliny Jeftael.
Mpaka ulizunguka kueleka kaskazini ukafika Hanathoni na ulikomea katika bonde la Ifta Eli.
15 I Katet, i Nahalal, i Symeron, i Jedala, i Betlehem, miast dwanaście, i wsi ich.
Mkoa huu ulijumuisha miji ya Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala, na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake.
16 Toć jest dziedzictwo synów Zabulonowych według domów ich, te miasta i wsi ich.
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Zabuloni, waliopewa kwa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
17 Isascharowi też padł los czwarty, to jest, synom Isascharowym według domów ich.
Upigaji kura wa nne uliangukia kwa Isakari, na waligawiwa kufuatana na koo zao.
18 A była granica ich Jezreel, i Chasalot, i Sunem.
Eneo lao lilijumuisha Jezreelli, Kesuloothi, Shunemu,
19 I Hafaraim, i Seon, i Anaharat;
Hafaraimu, Shioni, na Anaharathi.
20 I Rabbot, i Cesyjom, i Abes;
Pia ilijumuisha miji ya Rabithi, Kishioni, Ebezi,
21 I Ramet, i Engannim, i Enhadda, i Betfeses.
Remethi, Enganimu, Enihada, na Bethipazezi.
22 A przychodzi granica ich do Taboru, i do Sehesyma, i do Betsemes, a kończą się granice ich u Jordanu, miast szesnaście, i wsi ich.
Mpaka wao ulifika Tabor, Shahazuma, na Bethi Shemeshi, na ukakomea katika Yordani. Ilikuwa ni miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
23 Toć jest dziedzictwo pokolenia synów Isascharowych według domów ich, te miasta i wsi ich.
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Isakari, na walipewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
24 Potem padł los piąty pokoleniu synów Asur według domów ich.
Upigaji wa kura ya tano uliangukia kwa kabila la Asheri, na walipewa kwa koo zao.
25 I była granica ich: Helkat, i Chali, i Beten, i Achsaf;
Eneo lao lilijumuisha miji ya Helikathi, Hali, Beteni, Akashafu,
26 I Elmelech, i Amaad, i Aessal, a idzie na Karmel do morza, i do Sychor, i Lobanat.
Alameleki, Amadi, na Mshali. Mpaka wa magharibi ulitanuka hadi Karmeli na Shihori Libnathi.
27 Stamtąd się obraca na wschód słońca ku Betdagon, i bieży aż do Zabulon, i do doliny Jeftach El na północy, Betemek i do Nehyjel, wychodząc do Kabul ku lewej stronie;
Kisha ulizunguka upande wa mashariki kueleka Bethi Dagoni na ukaenda hadi Zabuloni, na kisha ukafika katika bonde la ifutaheli, upande wa kaskazini mwa Bethemeki na Neieli. Baadaye uliendelea mbele hata Kabuli kueleka upande wa Kaskazini.
28 I do Hebronu, i Rohob, i Hamon, i Kana, aż do Sydonu wielkiego.
Na kisha ulienda hadi Ebroni, Rehobu, Hammoni, na Kana, hata kufika mji mkubwa wa Sidoni.
29 A wraca się ta granica od Rama aż do miasta Zor obronnego; stamtąd się obraca ta granica aż do Hosa, a kończy się u morza podle działu Achsyba.
Mpaka ulirudi nyuma kuelekea Rama, na kisha ukafika kwenye mji wa Tiro uliokuwa na ngome. Baada ya hapo mpaka ulizunguka kuelekea Hosa na ulikomea katika bahari, katika mkoa wa Akizibu,
30 I Amma, i Afek, i Rohob, miast dwadzieścia i dwa, i wsi ich.
Umma, Afeki, na Rehobu. Kulikuwa na miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
31 Toć jest dziedzictwo pokolenia synów Aser według domów ich; te miasta i wsi ich.
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Asheri, na waliopewa kwa koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
32 Potem synom Neftalimowym padł los szósty, synom Neftalimowym według domów ich.
Upigaji wa kura wa mara ya sita uliangukia kwa kabila la Nafutali, na walipewa kufuatana na koo zao.
33 I była granica ich od Helef, i od Helon, do Saannanim, i Adami, które jest Necheb, i Jebnael, aż ku Lekum, i kończy się u Jordanu.
Mpaka wao ulianzia Helefu, kutoka katika mwaloni huko Zaananimu, ulipanda hadi Adaminekebu na Yabneeli, umbali kama Lakumu; na ulikomea katka Yordani.
34 Potem się obraca ta granica ku morzu do Asanot Tabor; a stamtąd bieży ku Hukoka, i idzie do Zabulonu na południe, a do Asar przychodzi ku zachodu, a do Juda ku Jordanowi na wschód słońca.
Mpaka ule ulizunguka upande wa magharibi kuelekea Aznothi Tabori na ulipanda hadi Hukoki; uligusa Zabuloni katika upande wa kusini, na ulifika hata Asheri katika upande wa magharibi, na Yuda katika upande wa mashariki huko katika mto Yordani.
35 A miasta obronne są: Assedym Ser, i Emat, Rekat, i Cyneret;
Miji yenye ngome ilikuwa ni Zidimu, Zeri, Hammathi, Rakathi, Kinnerethi,
36 I Edama, i Arama, i Asor,
Adama, Rama, Hazori,
37 I Kiedes, i Edrej, i Enhasor;
Kedeshi, Edrei, na Eni Hazori.
38 I Jeron, i Magdalel, Horem, i Betanat, i Betsemes, miast dziewiętnaście, i wsi ich.
Pia kulikuwa na miji ya Yironi, Migdaleli, Horemu, Bethi Anathi, na Bethi Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa, pamoja na vijiji vyake.
39 Toć jest dziedzictwo pokolenia synów Neftalimowych według domów ich; te miasta i wsi ich.
Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Nafutali, na walipewa miji pamoja na vijiji vyake kufuatana na koo zao.
40 Potem pokoleń synów Dan według domów ich, padł los siódmy.
Upigaji wa kura ya saba uliangukia kwa kabila la Dani, na walipewa kufuatana na koo zao.
41 A była granica dziedzictwa ich: Saraa, i Estaol, i Isremes;
Eneo lao la urithi lilijumuisha miji ya Zora, Eshitaoli, Iri Shemeshi,
42 I Selebim, i Ajalon, i Jetela;
Shaalabini, Aijaloni, na Ithila.
43 I Elon, i Temnata, i Ekron;
Vile vile lilijumuisha miji ya Eloni, Timna, Ekroni,
44 I Eltekie, i Gebbeton i Baalat;
Eliteke, Gibethoni, Baalathi,
45 I Jehut, i Bane Barak, i Getremmon;
Yehudi, Bene - Beraki, Gathi Rimoni,
46 I Mehajarkon, i Rakon z granicą przeciwko Joppie.
Me -Yarkoni, na Rakoni sambamba na eneo la karibu na Yopa.
47 Ale granica synów Danowych była bardzo mała; przetoż wyszedłszy synowie Dan dobywali Lesem, i wzięli je, i wysiekli je ostrzem miecza, i wziąwszy je w dziedzictwo mieszkali w niem; i przezwali Lesem Dan według imienia Dana, ojca swego.
Ilitokea wakati mpaka wa kabila la Dani ulipowapotea, kabila la Dani waliishambulia Leshemu, wakapigana nao, na wakauteka. Waliua kila mtu kwa upanga, wakauchukua ukawa mali yao, na wakakaa ndani yake. Wakauita mji ule Dani jina la babu yao badala ya Leshemu.
48 Toć jest dziedzictwo pokolenia synów Danowych według domów ich; te miasta, i wsi ich.
Huu ulikuwa urithi wa kabila la Dani, waliopewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
49 A gdy przestali dzielić ziemię według granic jej, tedy dali synowie Izraelscy dziedzictwo Jozuemu, synowi Nunowemu, w pośród siebie.
Walipomaliza kugawana urithi wa nchi, watu wa Israeli walimpa urithi Yoshua mwana wa Nuni kutoka miongoni mwao.
50 Według rozkazania Pańskiego dali mu miasto, którego żądał, Tamnat Saraa na górze Efraim, gdzie zbudował miasto, i mieszkał w niem.
Kwa amri ya Yahweh walimpatia mji wa Timnathi Sera ambao aliuomba, ulikuwa katika nchi ya milima ya Efraimu. Aliujenga mji na akaishi huko.
51 Teć są dziedzictwa, które losem podzielili w osiadłość Eleazar kapłan, i Jozue, syn Nunów, i przedniejsi z ojców pokolenia synów Izraelskich w Sylo przed Panem, u drzwi namiotu zgromadzenia, i dokończyli podziału ziemi.
Na huu ndio urithi ambao Eliazari kuhani, na Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa makabila ya familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli, waligawa kwa kupiga kura huko Shilo, mbele za Yahweh katika mlango wa hema la kukutania. Na hivyo wakamaliza kuigawa nchi.

< Jozuego 19 >