< Hioba 20 >

1 A odpowiadając Sofar Naamatczyk rzekł:
Ndipo Sofari, Mnaamathi alijibu na kusema,
2 Do tego mię myśli moje przywodzą, abym odpowiedział; przetożem się pospieszył.
“Mawazo yangu yananifanya mimi nijibu kwa haraka kwa sababu ya mashaka yaliyomo ndani yangu mimi.
3 Słyszałem mnie hańbiącą naganę; ale duch wyrozumienia mego odpowie za mię.
Mimi ninasikia kukemewa ambako kunaniondolea heshima mimi, lakini roho kutoka katika ufahamu wangu hunijibu mimi.
4 Izaż nie wiesz, że to jest od wieku, od tego czasu, jako postawił Bóg człowieka na ziemi?
Je, unafahamu kwamba ukweli huu kutoka enzi za kale, wakati Mungu alipomweka mwanadamu juu ya nchi:
5 Iż chwała niepobożnych krótka jest, a wesele obłudnika na mgnienie oka?
ushindi wa mtu mwovu ni mfupi, na furaha ya mtu asiyemcha Mungu hudumu kwa kitambo tu?
6 By też wstąpiła aż do nieba hardość jego, a obłoku się dotknęła głowa jego:
Ingawa urefu wake yeye hufikia juu kwenye mbingu, na kichwa chake yeye kufikia kwenye mawingu,
7 A wszakże na wieki zginie jako gnój jego, a ci, którzy go widzieli, rzeką: Gdzież się podział?
bado mtu huyo atapotea siku zote kama mavi yake yeye mwenyewe; wale waliokuwa wamemuona yeye watasema, 'Yuko wapi yeye'?
8 Uleci jako sen, a nie znajdą go; bo uciecze, jako widzenie nocne.
Yeye atapaa mbali kama ndoto na hataonekana; ndivyo ilivyo, yeye atakuwa amefukuzwa mbali kama ono la
9 Oko, które go widziało, nie ogląda go więcej, i nie ujrzy go więcej miejsce jego.
usiku. Jicho ambalo lilimuona yeye halitamuona yeye tena; mahali pake hapatamuona yeye tena.
10 Synowie jego będą się korzyć ubogim; bo ręce jego muszą wracać, co wydarł.
Watoto wake wataomba msamaha kwa watu maskini, mikono yake itaweza kurudisha utajiri wake.
11 Kości jego napełnione są grzechami młodości jego, a w prochu z nim leżeć będą.
Mifupa yake imejaa nguvu za ujanani, lakini zitalala naye chini katika mavumbi.
12 A choć złość słodnieje w ustach jego, i tai ją pod językiem swoim;
Japokuwa uovu ni mtamu katika mdomo wake yeye, japokuwa yeye anauficha chini ya ulimi wake yeye,
13 Kocha się w niej, a nie opuszcza jej, zatrzymywając ją w pośrodku podniebienia swego:
japokuwa anaushikilia pale na hauruhusu kwenda lakini bado huushikilia katika mdomo wake yeye -
14 Wszakże pokarm jego we wnętrznościach jego odmieni się; żółcią padalcową stanie się w trzewach jego.
chakula katika koromeo lake yeye hugeuka kuwa uchungu; hugeuka kuwa sumu ya majoka ndani yake yeye.
15 Bogactwa, które pożarł, zwróci, a z brzucha jego wyżenie je Bóg.
Yeye humeza chini utajiri, lakini yeye atautapika tena; Mungu atautoa nje kutoka katika tumbo lake yeye.
16 Głowę padalcową ssać będzie; zabije go język jaszczurczy.
Yeye atamumunya sumu ya majoka; ulimi wa nyoka mwenye sumu utamwua yeye.
17 Nie ogląda źródeł rzek, strumieni mówię miodu i masła.
Yeye hatafurahia vijito vya maji, wingi wa asali na siagi.
18 Wróci pracę cudzą, a nie zażyje jej; i choć znowu nabędzie wielkich majętności, nie ucieszy się niemi.
Yeye atayarudisha matunda ya kazi yake na hataweza kuyala; yeye hatafurahia utajiri alioupata kwa biashara zake yeye.
19 Bo ubogich dręczył i opuszczał, złupił dom, którego nie budował; przetoż nic spokojnego nie poczuje w żywocie swoim,
Kwa kuwa yeye amewakandamiza na kuwasahau watu maskini; yeye kwa uonevu, amezichukua mbali nyumba ambazo hakuzijenga yeye.
20 Ani rzeczy swych wdzięcznych nie będzie mógł zatrzymać.
Kwa sababu yeye mwenyewe hakujua utoshelevu wowote, yeye hataweza kuokoa kitu chochote katika kile ambacho alijifurahisha.
21 Nic nie zostanie z pokarmów jego, ani się rozmnoży dobro jego.
Hakuna chochote kilichoachwa ambacho yeye hakukimeza; kwa hiyo mafanikio yake yeye hayatakuwa ya kudumu.
22 Choćby i nazbyt miał wszystkiego, ściśniony będzie; wszelka ręka trapiących oburzy się nań.
katika wingi wa utajiri wake yeye ataanguka katika mahangaiko; mkono wa kila mmoja ambaye yuko katika umaskini utakuja kinyume chake yeye.
23 Choć będzie miał czem napełnić brzuch swój, przecież nań Bóg puści popędliwość gniewu swego, którą jako deszcz spuści nań, i na pokarmy jego.
Wakati akiwa katika kulijaza tumbo lake, Mungu atatupa hasira ya ghadhabu yake juu yake yeye; Mungu ataunyeshea chini juu yake yeye wakati yeye anakula.
24 Gdy uciekać będzie przed bronią żelazną, przebije go łuk hartowny.
Ingawa mtu huyo atakimbia kutoka katika silaha ya chuma, upinde wa shaba utampiga yeye.
25 Wyjęta będzie strzała z sajdaku wypuszczona, a grot przeniknie żółć jego; a gdy uchodzić będzie, ogarną go strachy.
Mshale utatoboa kupitia mgongoni mwake na utatokezea; ni dhahiri, ncha inayong'ra itatokezea nje kupitia ini lake yeye; watesi huja tena juu yake.
26 Wszystkie nieszczęścia zasadziły się nań w tajemnych miejscach jego, a pożre go ogień nierozdymany: pozostały w przybytku jego utrapiony będzie.
Giza lliilo kamilika limetunzwa kwa akiba zake; moto usiopulizwa utamla yeye kwa haraka; utameza kile kilichoachwa katika hema yake.
27 Odkryją niebiosa złość jego, a ziemia powstanie przeciwko niemu.
Mbingu zitauweka wazi uovu wake, na nchi itainuka juu dhidi yake yeye kama shahidi.
28 Przeniesie się urodzaj domu jego; dobra jego rozpłyną się w dzień gniewu jego.
Utajiri wa nyumba yake utatoweka; bidhaa zake zitamwagika mbali siku ya ghadhabu ya Mungu.
29 Tenci jest dział człowieka niepobożnego od Boga, to dziedzictwo naznaczone mu od Boga.
Hii ndiyo sehemu ya mtu mwovu kutoka kwa Mungu, urithi uliotunzwa akiba na Mungu kwa ajili yake yeye.”

< Hioba 20 >