< Jeremiasza 19 >

1 Tak mówi Pan: Idź, a kup dzban gliniany od garncarza, a wziąwszy niektórych z starszych ludu i z starszych kapłanów;
Hili ndilo asemalo Bwana: “Nenda ukanunue gudulia la udongo kutoka kwa mfinyanzi. Wachukue baadhi ya wazee wa watu na wa makuhani
2 Wnijdź do doliny syna Hennomowego, która jest u wrót bramy wschodniej, a tam opowiadaj słowa, które do ciebie mówić będę.
na mtoke mwende mpaka kwenye Bonde la Ben-Hinomu, karibu na ingilio la Lango la Vigae. Huko tangaza maneno ninayokuambia,
3 A rzecz: Słuchajcie słowa Pańskiego, królowie Judzcy i obywatele Jeruzalemscy! Tak mówi pan zastępów, Bóg Izraelski: Oto Ja przywiodę złe na to miejsce, o którem ktokolwiek usłyszy, zabrzmi mu w uszach jego.
nawe useme, ‘Sikieni neno la Bwana, enyi wafalme wa Yuda na watu wa Yerusalemu. Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Sikilizeni! Nitaleta maafa mahali hapa, ambayo yatafanya masikio ya kila mmoja atakayesikia habari zake yawashe.
4 Przeto, że mię opuścili, a splugawili to miejsce, kadząc na niem bogom cudzym, których nie znali oni i ojcowie ich, i królowie Judzcy, i napełnili to miejsce krwią niewinnych;
Kwa kuwa wameniacha na kupafanya mahali hapa kuwa pa miungu ya kigeni. Wameiteketezea sadaka miungu ambayo wao wala baba zao wala wafalme wa Yuda kamwe hawakuijua, nao wamelijaza eneo hili kwa damu isiyo na hatia.
5 I pobudowali wyżyny Baalowi, aby palili synów swych ogniem na całopalenie Baalowi, czegom nie rozkazał, anim oto mówił, ani to wstąpiło na serce moje:
Wamejenga mahali pa juu pa kuabudia miungu pa Baali ili kuteketeza wana wao katika moto kama sadaka kwa Baali, kitu ambacho sikukiamuru wala kukitaja, wala hakikuingia akilini mwangu.
6 Dlatego oto dni idą, mówi Pan, w których nie będzie nazywane więcej to miejsce Tofet, ani doliną syna Hennomowego, ale doliną mordu.
Hivyo jihadharini, siku zinakuja, asema Bwana, wakati watu hawatapaita tena mahali hapa Tofethi ama Bonde la Ben-Hinomu, bali Bonde la Machinjo.
7 Bo wniwecz obrócę radę Judzką i Jeruzalemską na tem miejscu, a sprawię, że oni upadną od miecza przed twarzą nieprzyjaciół swoich, i od ręki szukających duszy ich; i dam trupy ich na pokarm ptastwu niebieskiemu, i zwierzowi ziemskiemu;
“‘Nitaiharibu mipango ya Yuda na Yerusalemu mahali hapa. Nitawafanya waanguke kwa upanga mbele ya adui zao, katika mikono ya wale watafutao uhai wao, nami nitaitoa mizoga yao kuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi.
8 Podam także to miasto na spustoszenie i na świstanie; każdy idący mimo nie zdumieje się, a świstać będzie nad wszystkiemi plagami jego.
Nitauharibu mji huu na kuufanya kitu cha kudharauliwa. Wote wapitao karibu watashangaa na kuudhihaki kwa sababu ya majeraha yake yote.
9 I sprawię to, że będą jeść ciała synów swoich, i ciała córek swoich, a każdy z nich ciało bliźniego swego jeść będzie w oblężeniu i w uciśnieniu, którem ich ucisną nieprzyjaciele ich, i ci, którzy szukają duszy ich.
Nitawafanya wao kula nyama ya wana wao na binti zao; kila mmoja atakula nyama ya mwenzake wakati wa dhiki ya kuzungukwa na jeshi lililowekwa juu yao na adui wanaotafuta uhai wao.’
10 Potem stłucz ten dzban przed oczyma mężów, którzy pójdą z tobą,
“Kisha livunje lile gudulia wale walio pamoja nawe wakiwa wanaangalia,
11 A rzecz do nich: Tak mówi Pan zastępów: Tak stłukę ten lud, i to miasto, jako gdy kto tłucze naczynie garncarskie, które więcej naprawione być nie może: a w Tofet pogrzebywać będą, iż miejsca inszego nie będzie ku pogrzebowi.
uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: Nitalivunja taifa hili na mji huu kama gudulia hili la mfinyanzi lilivyovunjwa, nalo haliwezi kutengenezeka tena. Watawazika waliokufa huko Tofethi hata isiwepo nafasi zaidi.
12 Tak uczynię temu miejscu, mówi Pan, i obywatelom jego, i postąpię sobie z tem miastem, tak jako z Tofet.
Hivi ndivyo nitakavyopafanya mahali hapa na kwa wale waishio ndani yake, asema Bwana. Nitaufanya mji huu kama Tofethi.
13 Bo będą domy Jeruzalemskie i domy królów Judzkich, jako to miejsce Tofet, nieczyste ze wszystkiemi domami temi, na których dachach kadzili wszystkiemu wojsku niebieskiemu, i sprawowali ofiary mokre bogom cudzym.
Nyumba zilizoko Yerusalemu na zile za wafalme wa Yuda zitatiwa unajisi kama mahali hapa, Tofethi: yaani nyumba zote ambazo walifukiza uvumba juu ya mapaa yake kwa jeshi lote la angani, na kumimina dhabihu za vinywaji kwa miungu mingine.’”
14 Tedy wróciwszy się Jeremijasz z Tofet, gdzie go był Pan posłał, aby tam prorokował, stanął w sieni domu Pańskiego, i rzekł do wszystkiego ludu:
Kisha Yeremia akarudi kutoka Tofethi, mahali ambapo Bwana alikuwa amemtuma kutoa unabii, akasimama katika ua wa Hekalu la Bwana na kuwaambia watu wote,
15 Tak mówi Pan zastępów, Bóg Izraelski: Oto Ja przywiodę na to miasto i na wszystkie miasto jego wszystko to złe, którem wyrzekł przeciw niemu; bo zatwardzili kark swój, aby nie słuchali słów moich.
“Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Sikilizeni! Nitaleta juu ya mji huu pamoja na vijiji vinavyouzunguka kila maafa niliyosema dhidi yake, kwa sababu wamekuwa na shingo ngumu, na hawakuyasikiliza maneno yangu.’”

< Jeremiasza 19 >