< Jakuba 1 >

1 Jakób, sługa Boży i Pana Jezusa Chrystusa, dwunastu pokoleniom, które są w rozproszeniu, zdrowia życzy.
Yakobo, mtumwa wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo, kwa makabila kumi na mbili yaliyotawanyika, salaam.
2 Za największą radość miejcie, bracia moi! gdy w rozmaite pokusy wpadacie,
Hesabuni kuwa ni furaha zaidi, ndugu zangu, mnapopita katika matatizo mbali mbali,
3 Wiedząc, iż doświadczenie wiary waszej sprawuje cierpliwość;
mkijua kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huwapa uvumilivu.
4 A cierpliwość niech ma doskonały uczynek, żebyście byli doskonali i zupełni, którym by na niczem nie schodziło.
Acheni uvumilivu uikamilishe kazi yake, kwamba muweze kukomaa kikamilifu, bila kupungukiwa katika lolote.
5 A jeźli komu z was schodzi na mądrości, niech prosi u Boga, który ją szczerze wszystkim daje, a nie wymawia; i będzie mu dana.
Lakini kama mtu kati yenu anahitaji hekima, aiombe kutoka kwa Mungu, ambaye hutoa kwa ukarimu na pasipo kukemea kwa wote wamwombao, na atawapa hekima.
6 Ale niech prosi z wiarą, nic nie wątpiąc; albowiem kto wątpi, jest podobny wałowi morskiemu, który od wiatru pędzony i miotany bywa.
Lakini omba kwa imani, bila shaka, kwa kuwa mwenye kutia shaka ni kama mawimbi katika bahari, huchukuliwa na upepo na kutupwa huku na huko.
7 Bo niechaj nie mniema ten człowiek, aby co miał wziąć od Pana.
Kwa hakika mtu huyu asifikirie kwamba atapokelewa ombi lake kutoka kwa Bwana;
8 Mąż umysłu dwoistego jest niestateczny we wszystkich drogach swoich.
mtu huyu ana nia mbili, si imara katika njia zake zote.
9 A niech się chlubi brat niskiego stanu w wywyższeniu swojem,
Ndugu maskini anapaswa kujivuna katika kusimama kwake juu,
10 A bogaty w poniżeniu swojem; bo jako kwiat trawy przeminie.
wakati huo huo ndugu tajiri katika unyenyekevu wake, kwa sababu atatoweka kama ua la kondeni katika shamba analopita.
11 Albowiem jako słońce, kiedy weszło z gorącością, ususzyło trawę, a kwiat jej opadł i zginęła ona śliczność kształtu jego, tak i bogaty w drogach swoich uwiędnie.
Jua huchomoza na joto la kuunguza kukausha mimea, na maua huanguka na uzuri wake hufa. Vivyo hivyo watu matajiri watachakaa katikati ya kazi zao.
12 Błogosławiony mąż, który znosi pokuszenie; bo gdy będzie doświadczony, weźmie koronę żywota, którą obiecał Pan tym, którzy go miłują.
Amebarikiwa mtu yule anayevumilia majaribu, kwa kuwa baada ya kushinda jaribu hilo, atapokea taji ya uzima, ambayo imeahidiwa kwa wale wampendao Mungu.
13 Żaden, gdy bywa kuszony, niech nie mówi: Od Boga kuszony bywam; bo Bóg nie może kuszony być we złem, a sam nikogo nie kusi.
Mtu yeyote hapaswi kusema anapojaribiwa, “Jaribu hili linatoka kwa Mungu,” kwa sababu Mungu hajaribiwi na uovu, na Mungu mwenyewe hamjaribu yeyote.
14 Ale każdy bywa kuszony, gdy od swoich własnych pożądliwości bywa pociągniony i przynęcony.
Kila mtu hujaribiwa na tamaa zake mbaya zinazomshawishi na kumvuta mbali.
15 Zatem pożądliwość począwszy, rodzi grzech, a grzech będąc wykonany, rodzi śmierć.
Ndipo baada ya tamaa ya dhambi kubeba mimba, dhambi huzaliwa, na baada ya dhambi kukomaa sawasawa, huishia katika mauti.
16 Nie błądźcież, bracia moi mili!
Ndugu zangu wapendwa, msidanganyike.
17 Wszelki datek dobry i wszelki dar doskonały z góry jest, zstępujący od Ojca światłości, u którego nie masz odmiany, ani zaćmienia na wstecz się wracającego.
Kila zawadi iliyo nzuri na kila zawadi iliyokamilika hutoka juu, hushuka chini kutoka kwa Baba wa nuru. Kamwe habadiliki kama kivuli kibadilikavyo.
18 Który, przeto że chciał, porodził nas słowem prawdy ku temu, żebyśmy byli niejakiemi pierwiastkami stworzenia jego.
Mungu alichagua kutupa sisi uzima kwa Neno la kweli, ili kwamba tuweze kuwa kama uzao wa kwanza miongoni mwa viumbe vyake.
19 A tak, bracia moi mili! niech będzie każdy człowiek prędki ku słuchaniu, ale nierychły ku mówieniu i nierychły ku gniewowi.
Mnajua hili, ndugu zangu wapendwa. Kila mmoja anapaswa kuwa mwepesi wa kusikia, siyo mwepesi wa kuongea wala kukasirika,
20 Bo gniew męża nie sprawuje sprawiedliwości Bożej.
kwa kuwa hasira ya mwanadamu haiwezi kutenda haki ya Mungu.
21 A tak odrzuciwszy wszelakie plugastwo i zbytek złości, z cichością przyjmijcie słowo wszczepione, które może zbawić dusze wasze.
Kwa hiyo wekeni mbali uchafu wa dhambi na ubaya wote ulio mahali popote, na kwa unyenyekevu lipokeeni neno lililopandwa ndani yenu, ambalo lina uwezo wa kuokoa roho zenu.
22 A bądźcie czynicielami słowa, a nie słuchaczami tylko, oszukiwającymi samych siebie.
Litiini neno, msilisikie tu, mkijidanganya nafsi zenu wenyewe.
23 Albowiem jeźli kto jest słuchaczem słowa a nie czynicielem, ten podobny jest mężowi przypatrującemu się obliczu narodzenia swego we zwierciadle;
Kwa kuwa kama yeyote alisikiaye neno bila kulitendea kazi ni sawa na mtu ajiangaliaye uso wake halisi katika kioo.
24 Bo samego siebie obejrzał i odszedł, a wnet zapomniał, jakim był.
Hujitathimini uso wake, na huenda zake na baada ya muda mfupi husahau anavyofanana.
25 Ale kto by wejrzał w on doskonały zakon wolności i zostawałby w nim, ten nie będąc słuchaczem zapamiętliwym, ale czynicielem uczynku, ten błogosławionym będzie w uczynku swoim.
Bali mtu yule anayeiangalia kwa uangalifu sheria kamili, sheria ya uhuru, na kuendelea kuitii, si kwa sababu yeye ni msikilizaji anayesahau, huyu mtu atabarikiwa anapoitenda.
26 Jeźli kto między wami zda się być nabożnym, nie kiełznając języka swego, ale zwodząc serce swe, tego nabożeństwo próżne jest.
Ikiwa mtu yeyote atafikiri mwenyewe kuwa ni mtu wa dini, lakini hawezi kuutawala ulimi wake, huudanganya moyo wake na dini yake ni bure.
27 Nabożeństwo czyste i niepokalane u Boga i Ojca to jest: Nawiedzać sieroty i wdowy w ucisku ich i zachować samego siebie niepokalanym od świata.
Dini iliyo safi na isiyoharibiwa mbele za Mungu wetu na Baba ni hii: kuwasaidia yatima na wajane katika mateso yao, na kujilinda wenyewe na ufisadi wa dunia.

< Jakuba 1 >