< Wyjścia 28 >

1 A ty weźmij do siebie Aarona, brata twego, i syny jego z nim, z pośrodku synów Izraelskich, aby mi urząd kapłański odprawowali, Aaron, Nadab i Abiu, Eleazar, i Itamar, synowie Aaronowi.
“Mtwae Aroni ndugu yako aliyeletwa kwako kutoka miongoni mwa Waisraeli, pamoja na wanawe Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
2 A sprawisz szaty święte Aaronowi, bratu twemu, na cześć i na ozdobę.
Mshonee Aroni ndugu yako mavazi matakatifu ili yampe ukuu na heshima.
3 Ty się też rozmówisz z każdym umiejętnym rzemieślnikiem, któregom napełnił Duchem mądrości, aby urobili szaty Aaronowi na poświęcenie jego, aby mi urząd kapłański odprawował.
Waambie mafundi stadi wote niliowapa hekima katika shughuli hiyo wamtengenezee Aroni mavazi hayo, ili awekwe wakfu, anitumikie katika kazi ya ukuhani.
4 A teć są szaty, które urobią: Napierśnik, i naramiennik, i płaszcz, i suknia haftowana, czapka i pas. I urobią te szaty święte Aaronowi bratu twemu i synom jego, aby mi kapłański urząd sprawowali.
Haya ndiyo mavazi watakayoshona: kifuko cha kifuani, kisibau, kanzu, joho lililorembwa, kilemba na mshipi. Mavazi haya yatashonwa kwa ajili ya ndugu yako Aroni na wanawe ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
5 I nabiorą złota, i hijacyntu, i szarłatu, i karmazynu dwa kroć farbowanego, i jedwabiu białego.
Waambie watumie dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani safi.
6 I uczynią naramiennik ze złota, i z hijacyntu, i z szarłatu, z karmazynu dwa kroć farbowanego, i z jedwabiu białego kręconego, robotą haftarską.
“Tengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa, kazi ya fundi stadi.
7 Dwa zwierzchne kraje zszyte mieć będzie na dwu końcach swych, a tak społu spięte będą.
Kitakuwa na vipande viwili vya mabegani vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kufungia kisibau.
8 A przepasanie naramiennika tego, które na nim będzie, podobne będzie robocie jego; będzie także ze złota, z hijacyntu, i z szarłatu, i z karmazynu dwa kroć farbowanego, i z jedwabiu białego kręconego.
Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi utafanana nacho: utakuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao utengenezwe kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri.
9 I weźmiesz dwa kamienie onychiny, i wyryjesz na nich imiona synów Izraelskich;
“Chukua vito viwili vya shohamu, na uchore juu yake majina ya wana wa Israeli
10 Sześć imion ich na jednym kamieniu, a imion sześć drugich na drugim kamieniu, według narodzenia ich.
kufuatana na walivyozaliwa: majina sita katika kito kimoja, na mengine sita katika kito kingine.
11 Robotą snycerzów, którzy kamienie rzezą, wyryjesz na obu kamieniach imiona synów Izraelskich, i osadzisz je we złote osadzenia.
Yachore majina ya wana wa Israeli juu ya vito hivyo viwili kama vile sonara anavyochonga muhuri. Kisha uvitie vito hivyo katika vijalizo vya dhahabu,
12 I położysz te obadwa kamienie na wierzchnich krajach naramiennika, kamienie pamiątki dla synów Izraelskich; i nosić będzie Aaron imiona ich przed Panem na obu ramionach swych na pamiątkę.
na uvifungie juu ya vipande vya mabega ya kisibau yawe kama vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli. Aroni atavaa majina hayo mabegani mwake kama kumbukumbu mbele za Bwana.
13 Uczynisz też haczyki złote.
Tengeneza vijalizo vya dhahabu
14 Dwa też łańcuszki ze złota szczerego jednostajne; uczynisz je robotą plecioną, i zawiesisz te łańcuszki plecione na haczykach.
na mikufu miwili ya dhahabu safi iliyosokotwa kama kamba, na uifunge mikufu hiyo kwenye vijalizo.
15 Uczynisz też napierśnik sądu robotą haftarską, według roboty naramiennika urobisz go; ze złota, z hijacyntu, i z szarłatu, i z karmazynu dwa kroć farbowanego, i z białego jedwabiu kręconego uczynisz go.
“Fanyiza kifuko cha kifuani kwa ajili ya kufanya maamuzi, kazi ya fundi stadi. Kitengeneze kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
16 Czworograniasty będzie i dwoisty, na piędzi długość jego, i na piędzi szerokość jego.
Kitakuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, na kikunjwe mara mbili.
17 I nasadzisz weń pełno kamienia, cztery rzędy kamienia, tym porządkiem: sardyjusz, topazyjusz i szmaragd w pierwszym rzędzie;
Kisha weka safu nne za vito vya thamani juu yake. Safu ya kwanza itakuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
18 W drugim zasię rzędzie: karbunkuł, szafir, i jaspis.
katika safu ya pili itakuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
19 A w trzecim rzędzie: linkuryjusz, achates, i ametyst.
safu ya tatu itakuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
20 A w czwartym rzędzie: chryzolit, onychin i berył; te będą wsadzone w złoto w rzędziech swoich.
na safu ya nne itakuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Yote yatiwe kwenye vijalizo vya dhahabu.
21 A tych kamieni z imionami synów Izraelskich będzie dwanaście według imion ich; tak jako rzezą pieczęci, każdy według imienia swego będą, dla dwunastu pokoleń.
Patakuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kwa jina mojawapo la wana wa Israeli, kila kimoja kichorwe kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
22 Uczynisz też do napierśnika łańcuszki jednostajne robotą plecioną ze złota szczerego.
“Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani, tengeneza mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
23 Uczynisz też do napierśnika dwa kolce złote, i przyprawisz te dwa kolce do obu krajów napierśnika.
Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili yake, uzifungie kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
24 I przewleczesz dwa łańcuszki złote przez oba kolce u krajów napierśnika.
Funga ile mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete zilizo katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
25 Drugie zasię dwa kolce dwu łańcuszków zawleczesz na dwa haczyki, i przyprawisz do wierzchnich krajów naramiennika na przodku.
nazo zile ncha nyingine za mkufu zifunge kwenye vile vijalizo viwili, na uzishikamanishe na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
26 Uczynisz też dwa kolce złote, które przyprawisz do dwu końców napierśnika na kraju jego, który jest od naramiennika ze spodku.
Tengeneza pete mbili za dhahabu, uzishikamanishe kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
27 Do tego uczynisz dwa drugie kolce złote, które przyprawisz na dwie strony naramiennika ze spodku na przeciwko spojeniu jego, z wierzchu nad przepasaniem naramiennika.
Tengeneza pete nyingine mbili za dhahabu, na uzishikamanishe sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
28 Tak zwiążą napierśnik ten kolce jego z kolcami naramiennika sznurem hijacyntowym, aby był nad przepasaniem naramiennika, żeby nie odstawał napierśnik od naramiennika.
Pete za kifuko cha kifuani zitafungwa kwenye pete zile za kisibau kwa kamba ya buluu, ziunganishwe na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau.
29 I będzie nosił Aaron imiona synów Izraelskich na napierśniku sądu, na piersiach swych, gdy będzie wchodził do świątnicy, na pamiątkę ustawiczną przed Panem.
“Wakati wowote Aroni aingiapo Mahali Patakatifu, atakuwa na yale majina ya wana wa Israeli moyoni mwake juu ya kile kifuko cha kifuani cha uamuzi kama kumbukumbu ya kudumu mbele za Bwana.
30 Położysz też na napierśniku sądu Urim i Tummim, które będą na piersiach Aaronowych, gdy wchodzić będzie przed Pana; i poniesie Aaron sąd synów Izraelskich na piersiach przed Panem ustawicznie.
Pia weka Urimu na Thumimu ndani ya kifuko cha kifuani, yawe juu ya moyo wa Aroni kila mara aingiapo mbele za Bwana. Kwa hiyo siku zote Aroni atakuwa na uwezo kufanya maamuzi kwa ajili ya wana wa Israeli mbele za Bwana.
31 Uczynisz też płaszcz pod naramiennik, wszystek z hijacyntu.
“Shona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu,
32 A na wierzchu w pośród jego będzie rozpór, który rozpór obwiedziesz bramą plecioną w pancerzowy wzór, aby się nie rozdzierał.
na katikati uweke nafasi ya kuingizia kichwa. Kutakuwa na utepe uliofumwa, unaofanana na ukosi kuizunguka nafasi hiyo, ili isichanike.
33 Uczynisz też na podołku jego jabłka granatowe z hijacyntu, i z szarłatu, i z karmazynu dwa kroć farbowanego na podołku jego w około, a dzwonki złote między niemi w około.
Tengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu kuzunguka pindo la hilo joho, na uweke pia vikengele vya dhahabu kati ya hayo makomamanga.
34 Dzwonek złoty a jabłko granatowe; i zaś dzwonek złoty i jabłko granatowe u podołka płaszcza w około.
Hivyo vikengele vya dhahabu na makomamanga vitapishana kuzunguka upindo wa joho lile.
35 A będzie to miał na sobie Aaron przy posługiwaniu, aby słyszany był dźwięk jego, gdy będzie wchodził do świątnicy przed Pana, i gdy zaś wychodzić będzie, żeby nie umarł.
Ni lazima Aroni alivae anapofanya huduma. Sauti ya hivyo vikengele itasikika anapoingia na kutoka Mahali Patakatifu mbele za Bwana, ili asije akafa.
36 Uczynisz też blachę ze złota szczerego, a wyryjesz na niej robotą tych, co pieczęci rzezą: Świętość Panu.
“Tengeneza bamba la dhahabu safi na uchore juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
37 Tę przywiążesz do sznuru hijacyntowego, i będzie na czapce; na przodku na czapce będzie.
Lifunge hilo bamba kwa kamba ya buluu kwenye kilemba, nalo ni lazima liwe mbele ya kilemba.
38 A ta będzie nad czołem Aaronowem, aby nosił Aaron nieprawość poświęconych rzeczy, które by poświęcali synowie Izraelscy przy wszystkich darach poświęconych rzeczy swych; a będzie nad czołem jego ustawicznie, aby im zjednał łaskę u Pana.
Aroni alivae bamba hilo kwenye paji la uso wake, naye atachukua hatia kuhusu sadaka takatifu za Waisraeli wanazoweka wakfu, sadaka za aina yoyote. Litakuwa kwenye paji la uso wa Aroni daima ili zikubalike kwa Bwana.
39 Sprawisz też szatę z białego jedwabiu dzianą; także uczynisz czapkę z jedwabiu białego, pas też uczynisz robotą haftarską.
“Fuma koti la kitani safi na ufanye kilemba cha kitani safi. Mshipi uwe ni kazi ya mtarizi.
40 Synom także Aaronowym poczynisz szaty; i poczynisz im pasy, i czapki im poczynisz na cześć i na ozdobę.
Watengenezee wana wa Aroni makoti, mishipi na kofia, ili kuwapa ukuu na heshima.
41 A ubierzesz w nie Aarona, brata twego, i syny jego z nim; i pomażesz je, a napełnisz ręce ich, i poświęcisz je, aby mi urząd kapłański sprawowali.
Baada ya kumvika Aroni ndugu yako pamoja na wanawe nguo hizi, watie mafuta na kuwabariki. Waweke wakfu ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
42 Urobisz im też ubiory lniane, dla zakrycia nagości ciała; od biódr aż do udów będą.
“Watengenezee nguo za ndani za kitani zitakazofunika mwili, kutoka kiunoni hadi mapajani.
43 A będą na Aaronie i na synach jego, gdy wchodzić będą do namiotu zgromadzenia, albo gdy będą przystępować do ołtarza, aby służyli w świątnicy, żeby niosąc nieprawość, nie pomarli. Ustawa to wieczna będzie jemu, i nasieniu jego po nim.
Aroni na wanawe ni lazima wavae haya kila wanapoingia katika Hema la Kukutania au wanaposogelea madhabahu wakati wa kutoa huduma katika Mahali Patakatifu, ili wasije wakafanya kosa wakafa. “Haya yawe maagizo ya kudumu kwa Aroni na vizazi vyake.

< Wyjścia 28 >