< II Królewska 8 >

1 Potem Elizeusz rzekł do onej niewiasty, której był syna wskrzesił, mówiąc: Wstań a idź, ty i dom twój, a bądź gościem, kędy będziesz mogła być; bo zawołał Pan głodu, i przyjdzie na ziemię przez siedm lat.
Wakati huu, Elisha alikuwa amemwambia yule mwanamke ambaye mwanawe alikuwa amefufuliwa, “Ondoka wewe na jamaa yako ukaishi mahali popote unapoweza kwa kitambo kidogo, kwa sababu Bwana ameamuru njaa katika nchi hii ambayo itadumu kwa miaka saba.”
2 Wstała tedy ona niewiasta, i uczyniła według słowa męża Bożego; a poszła ona i dom jej, i była gościem w ziemi Filistyńskiej przez siedm lat.
Yule mwanamke akafanya kama vile yule mtu wa Mungu alivyosema. Yeye na jamaa yake wakaondoka na kwenda kuishi katika nchi ya Wafilisti kwa miaka saba.
3 I stało się po wyjściu siedmiu lat, że się wróciła ona niewiasta z ziemi Filistyńskiej, i poszła, aby wołała na króla o dom swój, i o rolę swoję.
Baada ya miaka saba, yule mwanamke akarudi kutoka nchi ya Wafilisti, akaenda kwa mfalme kumsihi kwa ajili ya nyumba yake na shamba lake.
4 A na ten czas król rozmawiał z Giezym, sługą męża Bożego, mówiąc: Powiedz mi proszę wszystkie zacne sprawy, które czynił Elizeusz.
Mfalme alikuwa anazungumza na Gehazi, mtumishi wa mtu wa Mungu, naye alikuwa amesema, “Hebu niambie mambo yote makuu yaliyofanywa na Elisha.”
5 A gdy on powiadał królowi, jako wskrzesił umarłego, oto niewiasta, której był wskrzesił syna, zawołała na króla o dom swój i o rolę swoję. I rzekł Giezy: Królu panie mój, tać to jest niewiasta, i ten syn jej, którego wskrzesił Elizeusz.
Wakati Gehazi alipokuwa akimweleza mfalme jinsi Elisha alivyomfufua mtu, yule mwanamke ambaye mwanawe alikuwa amefufuliwa na Elisha akaja ili amsihi mfalme kwa ajili ya nyumba yake na shamba lake. Gehazi akasema, “Huyu ndiye huyo mwanamke, bwana wangu mfalme, na huyu ndiye mwanawe ambaye Elisha alimfufua.”
6 I pytał król niewiasty, a ona mu powiedziała. I przydał jej król komornika jednego, mówiąc: Przywróć jej wszystko, co jej było, i wszystkie dochody z pola od onego dnia, którego opuściła ziemię, aż dotąd.
Mfalme akamuuliza yule mwanamke kuhusu mambo hayo, naye akamweleza. Ndipo akaamuru afisa ashughulikie shauri lake na kumwambia, “Mrudishie huyu mwanamke kila kitu kilichokuwa mali yake, pamoja na mapato yote yaliyotokana na shamba lake tangu siku alipoondoka nchini hadi sasa.”
7 Potem przyszedł Elizeusz do Damaszku, a Benadad, król Syryjski, chorował. I powiedziano mu, mówiąc: Przyszedł tu mąż Boży.
Elisha akaenda Dameski, naye Ben-Hadadi mfalme wa Aramu alikuwa mgonjwa. Mfalme alipoambiwa, “Mtu wa Mungu ametoka mbali akapanda hadi hapa,”
8 I rzekł król do Hazaela: Weźmij w rękę swą upominek, a idź przeciwko mężowi Bożemu, i pytaj się Pana przezeń, mówiąc: Wstanęli z tej choroby?
mfalme akamwambia Hazaeli. “Chukua zawadi na uende kumlaki huyo mtu wa Mungu. Muulize Bwana kupitia yeye, kwamba, ‘Je, nitapona ugonjwa huu?’”
9 Przetoż szedł Hazael przeciwko niemu, a wziąwszy upominek w rękę swą, i ze wszystkich dóbr Damaskich brzemion na czterdzieści wielbłądów. I przyszedł, a stanął przed nim, mówiąc: Syn twój Benadad, król Syryjski, posłał mię do ciebie, mówiąc: Wstanęli z tej choroby?
Hazaeli akaenda kumlaki Elisha, akiwa amechukua zawadi ya kila kitu kizuri kilichopatikana Dameski, mizigo iliyobebwa na ngamia arobaini. Akaingia ndani na kusimama mbele yake, akasema, “Mwanao Ben-Hadadi mfalme wa Aramu amenituma niulize, ‘Je, nitapona ugonjwa huu?’”
10 I odpowiedział mu Elizeusz: Idź, powiedz mu: Wprawdziebyści mógł żyć; wszakże okazał mi Pan, że pewnie umrzesz.
Elisha akajibu, “Nenda ukamwambie, ‘Hakika utapona’; lakini Bwana amenifunulia kwamba kweli atakufa.”
11 Wtem pokazał mu, i stawił twarz swoję smutną, i płakał mąż Boży.
Elisha akamkazia Hazaeli macho kwa nguvu mpaka akaona aibu. Kisha mtu wa Mungu akaanza kulia.
12 Któremu rzekł Hazael: Czemuż pan mój płacze? I odpowiedział: Iż wiem, co uczynisz złego synom Izraelskim. Twierdze ich popalisz ogniem, a młodzieńce ich mieczem pomordujesz, i dzieci ich poroztrącasz, i brzemienne ich porozcinasz.
Hazaeli akauliza “Kwa nini bwana wangu analia?” Elisha akajibu, “Kwa sababu najua mabaya utakayowatendea Waisraeli. Utachoma moto ngome zao, utawaua vijana wao kwa upanga, kuwatupa chini kwa nguvu watoto wachanga, na kuwatumbua wanawake wenye mimba.”
13 Tedy rzekł Hazael: Co? Izali sługa twój pies, żeby miał czynić tak wielką rzecz? I odpowiedział Elizeusz: Okazał mi Pan, że ty będziesz królem nad Syrią.
Hazaeli akasema, “Itawezekanaje mtumishi wako, aliye mbwa tu, kufanya tendo la ajabu namna hiyo?” Elisha akamjibu, “Bwana amenionyesha kuwa utakuwa mfalme wa Aramu.”
14 I odszedł od Elizeusza, a przyszedł do pana swego, który rzekł do niego: Cóż ci powiedział Elizeusz? A on rzekł: Powiedział mi, żebyś pewnie mógł żyć.
Kisha Hazaeli akamwacha Elisha na kumrudia bwana wake. Ben-Hadadi akamuuliza, “Elisha alikuambia nini?” Hazaeli akajibu, “Aliniambia kwamba hakika utapona.”
15 A nazajutrz wziął Hazael kołdrę i zamaczał ją w wodzie, i rozciągnął na twarzy jego. I umarł (Benadad), a Hazael królował miasto niego.
Lakini kesho yake Hazaeli akachukua nguo nzito, akailoweka ndani ya maji, akaitandaza juu ya uso wa mfalme, hivyo akafa. Kisha Hazaeli akaingia mahali pake kuwa mfalme wa Aramu.
16 A roku piątego Jorama, syna Achaba, króla Izraelskiego, i Jozafata króla Judzkiego, począł królować Joram, syn Jozafata, król Judzki.
Katika mwaka wa tano wa Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, wakati huo Yehoshafati akiwa mfalme wa Yuda, Yehoramu mwana wa Yehoshafati akaanza kutawala kama mfalme wa Yuda.
17 Trzydzieści i dwa lata miał, gdy królować począł, a ośm lat królował w Jeruzalemie.
Alikuwa na umri wa miaka thelathini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka minane.
18 Ale chodził drogami królów Izraelskich, sprawując się jako dom Achabowy; bo córkę Achabową miał za żonę, i czynił złe przed oczyma Pańskiemi.
Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa imefanya, kwa kuwa alimwoa binti wa Ahabu. Akatenda maovu machoni pa Bwana.
19 Wszakże nie chciał Pan wytracić Judy, dla Dawida, sługi swego, jako mu był powiedział, iż mu miał dać pochodnię między synami jego, po wszystkie dni.
Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi mtumishi wake, Bwana hakutaka kuiangamiza Yuda. Alikuwa ameahidi kuidumisha taa kwa ajili ya Daudi na wazao wake milele.
20 Za dni jego odstąpił Edom, aby nie był pod mocą Judy; i postanowili nad sobą króla.
Wakati wa Yehoramu, Edomu waliasi dhidi ya Yuda na kujiwekea mfalme wao wenyewe.
21 Przetoż przyciągnął Joram do Seiru, i wszystkie wozy z nim; a wstawszy w nocy poraził Edomczyki, którzy go byli otoczyli, i hetmany wozów, tak iż lud uciekał do namiotów swoich.
Basi Yehoramu akaenda Sairi pamoja na magari yake yote ya vita. Waedomu wakamzunguka yeye na majemadari wake wa magari yake ya vita, lakini akaondoka, akapenya usiku na kuwashambulia Waedomu. Hata hivyo, jeshi lake likatorokea nyumbani mwao.
22 Wszakże odstąpił Edom, aby nie był pod mocą Judy, aż do dnia tego. Odstąpiło także i Lobne onegoż czasu.
Hadi leo Edomu wameasi dhidi ya Yuda. Libna pia wakaasi wakati huo huo.
23 A inne sprawy Joramowe, i wszystko co czynił, izali nie jest napisane w kronikach o królach Judzkich?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Yehoramu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
24 I zasnął Joram z ojcami swymi, a pogrzebiony jest z ojcami swymi w mieście Dawidowem; i królował Ochozyjasz, syn jego, miasto niego.
Yehoramu akalala pamoja na baba zake, na akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Ahazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
25 Roku dwunastego Jorama, syna Achaba, króla Izraelskiego, począł królować Ochozyjasz, syn Jorama, króla Judzkiego.
Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda alianza kutawala.
26 We dwudziestu i dwóch latach był Ochozyjasz, gdy królować począł, a rok jeden królował w Jeruzalemie; a imię matki jego było Atalija, córka Amrego, króla Izraelskiego.
Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala katika Yerusalemu kwa mwaka mmoja. Mama yake aliitwa Athalia, mjukuu wa Omri mfalme wa Israeli.
27 Ten chodził drogą domu Achabowego, i czynił złe przed oczyma Pańskiemi, jako i dom Achabowy; bo był zięciem domu Achabowego.
Akaenenda katika njia za nyumba ya Ahabu, na kutenda maovu machoni pa Bwana, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa imefanya, kwa kuwa alikuwa ameoa kutoka nyumba ya Ahabu.
28 Przetoż wychadzał z Joramem, synem Achabowym, na wojnę przeciw Hazaelowi, królowi Syryjskiemu, do Ramot Galaadskiego; ale porazili Syryjczycy Jorama.
Ahazia akaenda vitani na Yoramu mwana wa Ahabu kupigana na Hazaeli mfalme wa Aramu huko Ramoth-Gileadi. Waaramu wakamjeruhi Yoramu.
29 A tak wrócił się król Joram, aby się leczył w Jezreelu na rany, które mu byli zadali Syryjczycy w Ramacie, gdy walczył z Hazaelem, królem Syryjskim. A Ochozyjasz, syn Jorama, króla Judzkiego, przyjechał nawiedzać Jorama, syna Achabowego, do Jezreela; bo tam chorował.
Hivyo Mfalme Yoramu akarudi Yezreeli ili apate kuuguza majeraha aliyojeruhiwa na Waaramu huko Ramothi alipopigana na Hazaeli mfalme wa Aramu. Ndipo Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akashuka kwenda Yezreeli kumtazama Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.

< II Królewska 8 >