< II Kronik 32 >

1 Po tych sprawach i pewnem ich postanowieniu przyciągnął Sennacheryb, król Assyryjski, a wtargnąwszy do Judzkiej ziemi, położył się obozem przeciw miastom obronnym, a umyślił je sobie dobyć.
Baada ya yale yote aliyokuwa amefanya Hezekia kwa uaminifu mkubwa, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaja na kuvamia Yuda. Akaizunguka miji yenye ngome kwa jeshi, akifikiri kuiteka iwe yake.
2 A widząc Ezechyjasz, że przyciągnął Sennacheryb, a iż twarz swoję obrócił, aby walczył przeciw Jeruzalemowi:
Hezekia alipoona kuwa Senakeribu amekuja na kwamba alikusudia kufanya vita juu ya Yerusalemu,
3 Tedy wszedł w radę z książętami swymi i z rycerstwem swem, aby zatkali źródła wód, które były za miastem; i pomogli mu.
akafanya shauri na maafisa wake na mashujaa wake juu ya kuzuia maji kutoka chemchemi zilizo nje ya mji, nao wakamsaidia.
4 Bo zebrawszy się lud wielki zatkali wszystkie źródła, i potok, który płynął przez pośrodek ziemi, mówiąc: Czemużby przyszedłszy królowie Assyryjscy mieli znaleść tak wiele wód?
Umati mkubwa wa watu ukakusanyika na kuzuia chemchemi zote na vijito vilivyotiririka katika nchi yote, wakisema: “Kwa nini wafalme wa Ashuru waje na kukuta maji tele?”
5 A pokrzepiwszy się, pobudował wszystkie mury obalone, i nabudował wież, przytem zewnątrz drugi mur; i zmocnił Mello w mieście Dawidowem, i poczynił broni bardzo wiele, i tarczy.
Hezekia akafanya kazi kwa bidii kukarabati sehemu zote zilizokuwa zimebomoka za ukuta na kujenga minara juu yake. Akajenga ukuta mwingine nje ya ule uliokuwepo na kuimarisha Milo katika Mji wa Daudi. Akatengeneza pia silaha nyingi na ngao.
6 Postanowił też hetmanów wojennych nad ludem, których zgromadził do siebie na ulicę bramy miejskiej, i mówił łaskawie do nich, a rzekł:
Akaweka maafisa wa jeshi juu ya watu, wakawakutanisha mbele yake katika uwanja kwenye lango la mji, naye akawatia moyo kwa maneno haya:
7 Zmacniajcie się, i mężnie sobie poczynajcie; nie bójcie się, ani się lękajcie twarzy króla Assyryjskiego, ani twarzy wszystkiego mnóstwa, które jest z nim; bo większy jest z nami niżeli z nim.
“Kuweni hodari na wenye moyo mkuu. Msiogope, msifadhaike wala msikate tamaa kwa sababu ya mfalme wa Ashuru na hili jeshi kubwa lililo pamoja naye, kwa kuwa aliye pamoja nasi ni mkuu kuliko aliye pamoja naye.
8 Z nimi jest ramię cielesne; ale z nami jest Pan, Bóg nasz, aby nas ratował i odprawiał wojny nasze. Tedy spoległ lud na słowach Ezechyjasza, króla Judzkiego.
Kwake uko mkono wa mwili tu, bali kwetu yuko Bwana Mungu wetu kutusaidia na kutupigania vita vyetu.” Nao watu wakatiwa moyo kutokana na maneno aliyowaambia Hezekia mfalme wa Yuda.
9 Potem posłał Sennacheryb, król Assyryjski, sługi swe do Jeruzalemu, (a sam dobywał Lachis, a wszystka moc jego była z nim, ) do Ezechyjasza, króla Judzkiego, i do wszystkich z Judy, którzy byli w Jeruzalemie, mówiąc:
Hatimaye Senakeribu mfalme wa Ashuru na majeshi yake yote walipokuwa wameuzunguka Lakishi, akawatuma maafisa wake kwenda Yerusalemu wakiwa na ujumbe huu kwa Hezekia mfalme wa Yuda, na kwa watu wote wa Yuda waliokuwako humo, kusema:
10 Tak mówi Sennacheryb, król Assyryjski: W czemże wżdy ufacie, że siedzicie w murach Jeruzalemskich?
“Hili ndilo asemalo Senakeribu mfalme wa Ashuru: Je, mmeweka tumaini lenu wapi, hata mnaendelea kukaa katika Yerusalemu, hali mmezungukwa na jeshi?
11 Izali Ezechyjasz nie zwodzi was, aby was pomorzył głodem i pragnieniem, mówiąc: Pan, Bóg nasz, wyrwie nas z ręki króla Assyryjskiego?
Hezekia asemapo, ‘Bwana Mungu wetu atatuokoa kutokana na mkono wa mfalme wa Ashuru,’ anawapotosha ninyi, naye atawaacha mfe kwa njaa na kiu.
12 Izali nie ten Ezechyjasz zniósł wyżyny jego, i ołtarze jego, i rozkazał Judzie i Jeruzalemczykom, mówiąc: Przy jednym tylko ołtarzu kłaniać się będziecie, i na nim kadzić?
Je, si Hezekia mwenyewe aliyeondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake, akiwaambia Yuda wa Yerusalemu, ‘Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu moja na kuteketeza dhabihu juu yake’?
13 Izali nie wiecie, com uczynił ja i ojcowie moi wszystkim narodom ziemskim? Azaż jakim sposobem mogli bogowie narodów ziemskich wyrwać ziemię swoję z ręki mojej?
“Je, hamjui yale mimi na baba zangu tuliyoyafanya kwa mataifa yote ya nchi zingine? Je, miungu ya mataifa hayo iliweza kuokoa nchi zao kutoka mkononi mwangu?
14 Któż był ze wszystkich bogów onych narodów, które wytracili ojcowie moi, coby mógł wybawić lud swój z ręki mojej, aby też mógł Bóg wasz wyrwać was z ręki mojej?
Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya mataifa haya ambayo baba zangu waliyaangamiza ameweza kuwaokoa watu wake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Mungu wenu kuwaokoa mkononi mwangu?
15 Przetoż teraz niech was nie zwodzi Ezechyjasz, a niech was na to nie namawia, ani mu wierzcie. Jeźlić nie mógł żaden bóg wszystkich narodów i królestw wyrwać ludu swego z ręki mojej, i z ręki ojców moich, pogotowiu Bóg wasz nie wyrwie was z ręki mojej.
Sasa basi, msikubali Hezekia awadanganye na kuwapotosha namna hii. Msimwamini, kwa kuwa hakuna mungu wa taifa lolote wala wa ufalme wowote aliyeweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu au mkononi mwa baba zangu. Sembuse huyo mungu wenu atawaokoaje kutoka mkononi mwangu!”
16 Nadto jeszcze mówili słudzy jego przeciw Panu Bogu, i przeciwko Ezechyjaszowi słudze jego.
Maafisa wa Senakeribu wakaendelea kunena dhidi ya Bwana aliye Mungu na dhidi ya mtumishi wake Hezekia.
17 Listy też pisał, urągając Panu, Bogu Izraelskiemu, a mówiąc przeciwko niemu temi słowy: Jako bogowie narodów ziemskich nie wyrwali ludu swego z ręki mojej, tak nie wyrwie Bóg Ezechyjaszowy ludu swego z ręki mojej.
Mfalme pia aliandika barua akimtukana Bwana, Mungu wa Israeli na kusema haya dhidi yake: “Kama vile miungu ya mataifa ya nchi nyingine ilivyoshindwa kuwaokoa watu wao mkononi mwangu, vivyo hivyo Mungu wa Hezekia hataweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu.”
18 I wołali głosem wielkim po żydowsku przeciwko ludowi Jeruzalemskiemu, który był na murach, strasząc go i trwożąc go, aby tak miasto wzięli.
Kisha wakawaita kwa Kiebrania watu wa Yerusalemu waliokuwa juu ya ukuta ili kuwatisha na kuwatia hofu ili waweze kuuteka mji.
19 A mówili przeciw Bogu Jeruzalemskiemu, jako przeciw bogom narodów ziemskich, którzy są robotą rąk ludzkich.
Wakanena juu ya Mungu wa Yerusalemu kama vile walivyonena juu ya miungu ya mataifa mengine ya dunia ambayo ni kazi ya mikono ya wanadamu.
20 Tedy się modlił Ezechyjasz król, i Izajasz prorok, syn Amosa, dla tego, i krzyczeli ku niebu.
Mfalme Hezekia na nabii Isaya mwana wa Amozi wakalilia mbingu katika maombi kuhusu jambo hili.
21 I posłał Pan Anioła, który wytracił każdego mocarza w wojsku, i wodza, i hetmana w obozie króla Assyryjskiego. I wrócił się z pohańbieniem twarzy do ziemi swojej. A gdy wszedł do domu boga swego, ci, którzy wyszli z żywota jego, tam go zabili mie czem.
Naye Bwana akamtuma malaika ambaye aliangamiza wanajeshi wote, na viongozi na maafisa katika kambi ya mfalme wa Ashuru. Kwa hiyo, mfalme wa Ashuru akarudi nchini mwake kwa aibu. Naye alipokwenda katika hekalu la mungu wake, baadhi ya watoto wake wakamuua kwa upanga.
22 A tak wybawił Pan Ezechyjasza i obywateli Jeruzalemskich z rąk Sennacheryba, króla Assyryjskiego, i z rąk wszystkich, a sprawił im pokój zewsząd.
Hivyo Bwana akamwokoa Hezekia na watu wa Yerusalemu kutoka mkononi mwa Senakeribu mfalme wa Ashuru na kutoka mikononi mwa wengine wote. Bwana akawastarehesha kila upande.
23 Tedy wiele ich przynosiło Panu dary do Jeruzalemu i upominki kosztowne Ezechyjaszowi, królowi Judzkiemu; i wywyższony jest w oczach wszystkich narodów potem.
Watu wengi wakaleta sadaka Yerusalemu kwa ajili ya Bwana na zawadi za thamani kwa ajili ya Hezekia mfalme wa Yuda. Tangu hapo na kuendelea, Hezekia aliheshimiwa sana na mataifa yote.
24 W one dni zachorował Ezechyjasz aż na śmierć, i modlił się Panu; który mówił do niego, a dał mu znak.
Katika siku hizo, Hezekia akaugua, naye akawa karibu kufa. Akamwomba Bwana, ambaye alimjibu na kumpa ishara.
25 Ale nie według dobrodziejstw sobie uczynionych sprawował się Ezechyjasz, bo się wyniosło serce jego; przetoż powstał przeciw niemu gniew, i przeciw Judzie, i przeciw Jeruzalemowi.
Lakini moyo wa Hezekia ukajaa majivuno na hakuonyesha itikio kwa wema aliotendewa, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana ikawa juu yake na juu ya Yuda na Yerusalemu.
26 Ale gdy się upokorzył Ezechyjasz (bo się było wyniosło serce jego) on i obywatele Jeruzalemscy, nie przyszedł na nich gniew Pański za dni Ezechyjaszowych.
Ndipo Hezekia akatubu kwa ajili ya kiburi cha moyo wake, kama walivyofanya watu wa Yerusalemu, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana haikuja juu yao katika siku za Hezekia.
27 A miał Ezechyjasz bogactwa i sławę bardzo wielką; bo sobie zebrał skarby srebra i złota, i kamieni drogich, i rzeczy wonnych, i rynsztunku, i wszelakiego naczynia kosztownego.
Hezekia alikuwa na utajiri mwingi sana na heshima, naye akajifanyia hazina kwa ajili ya fedha yake na dhahabu na kwa ajili ya vito vyake vya thamani, vikolezi, ngao na aina zote za vyombo vya thamani.
28 Miał też szpichlerze dla urodzajów zboża i wina, i oliwy, i obory dla bydeł, i zwierzyniec dla rozmaitych zwierząt.
Akajenga pia maghala ya kuhifadhi mavuno ya nafaka, divai mpya na mafuta. Akatengeneza mabanda kwa ajili ya aina mbalimbali za mifugo, na mazizi kwa ajili ya kondoo na mbuzi.
29 Miasta też sobie pobudował, i miał stada owiec, i wołów mnóstwo; albowiem mu dał Bóg majętność bardzo wielką.
Akajenga vijiji na kujipatia idadi kubwa ya kondoo na mbuzi, pamoja na ngʼombe kwa kuwa Mungu alikuwa amempa utajiri mwingi sana.
30 Ten też Ezechyjasz zatkał źródło wód w Gichonie wyższe, a przywiódł je dołem na zachód słońca ku miastu Dawidowemu; i szczęściło się Ezechyjaszowi we wszystkich sprawach jego.
Ilikuwa ni Hezekia aliyeziba njia za kutolea maji za chemchemi za juu za Gihoni na kuyaelekeza maji kutiririkia upande wa magharibi wa Mji wa Daudi. Akafanikiwa katika kila kitu alichofanya.
31 A wszakże dla posłów książąt Babilońskich, którzy byli posłani do niego, aby go pytali o znak, który się był stał w ziemi, opuścił go Bóg, aby go kusił, a iżby wiedziano wszystko, co było w sercu jego.
Lakini wakati wajumbe walipotumwa na watawala wa Babeli kumuuliza juu ya ishara ambayo ilitokea katika nchi, Mungu alimwacha ili kumjaribu na kujua kila kitu kilichokuwa moyoni mwake.
32 Ale inne sprawy Ezechyjaszowe, i dobroczynności jego, napisane są w widzeniu Izajasza proroka, syna Amosowego, i w księgach królów Judzkich i Izraelskich.
Matukio mengine ya utawala wa Hezekia na matendo yake ya kujitoa kwa moyo yameandikwa katika maono ya nabii Isaya mwana wa Amozi kwenye kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
33 I zasnął Ezechyjasz z ojcami swymi, i pogrzebiony jest nad grobami synów Dawidowych. I wyrządzili mu wszystek Juda i obywatele Jeruzalemscy uczciwość przy śmierci jego. A królował Manases, syn jego, miasto niego.
Hezekia akalala na baba zake na akazikwa kwenye kilima mahali yalipo makaburi ya wazao wa Daudi. Yuda wote na watu wa Yerusalemu wakamheshimu alipofariki. Naye Manase mwanawe akawa mfalme baada yake.

< II Kronik 32 >